Mbio za Mwenge zinaenda kuwaumbua

Mbio za Mwenge zinaenda kuwaumbua

Inabidi tutumie akili magufuli ananafasi gani ya kuzuia ccm kubana matumizi?
Yeye anabana matumizi ndani ya serikali KWENYE chama huko wapo wanaowajibina,

Swali

Chedema.wanazunguka nchi nzima. Je wao.hawabani matumizi ?
Je wanapoeleza kuwa na wao wanataka kubana matumizi wakipewa Dora je wanasubili waende ikulu ndo wajifunze au wanajua hata kabla hawaenda ikulu?
Wanapoishauri serikali ibane matumizi je wao wanachokisema.wanaweza kukionyesha kwa vitendo?
Acha kupinga tumia weredi kufanya uchambuzi
kutumia gari la serikali mpaka singida kwenye sherehe za chama kuanzia rais mpaka waziri mkuu na mawaziri je!sio ufujaji wa kodi za walalahoi?
 
Inabidi tutumie akili magufuli ananafasi gani ya kuzuia ccm kubana matumizi?
Yeye anabana matumizi ndani ya serikali KWENYE chama huko wapo wanaowajibina,

Swali

Chedema.wanazunguka nchi nzima. Je wao.hawabani matumizi ?
Je wanapoeleza kuwa na wao wanataka kubana matumizi wakipewa Dora je wanasubili waende ikulu ndo wajifunze au wanajua hata kabla hawaenda ikulu?
Wanapoishauri serikali ibane matumizi je wao wanachokisema.wanaweza kukionyesha kwa vitendo?
Acha kupinga tumia weredi kufanya uchambuzi
Asante kwa points zako. Wakati wa kampeni CHADEMA waliitisha harambee ya wafanyabiashara kwa ajili ya kuongeza uwezo wa kufanya kampeni, kwa hiyo CHADEMA kuchangisha fedha kwa ajili ya shughuli za chama sio kosa, ila CCM wakichangishana fedha ni kosa na ni chanzo cha ufisadi. Upinzani una siasa nyepesi sana, yaani ukiwa na uwezo wa kupinga hoja bila hata kuishughulisha akili japo kufikiri kidogo, basi wewe unafaa kuwa mpinzani.
 
Ndiyo maana mm CHICHIEM wakiongea yanaingilia huku na kupitia huku...
 
Vijana wa dot com ndio hawajui umuhimu wa mwenge...

Mwenge sio tu lile litaa linalowaka...think big...

Mwenge ni zaidi ya hapo...rudi kwenye dhana yenyewe ya mwenge kuwa ni uhuru, ni taa ya matumaini na inachoma maadui zetu...

Mwenge hauna tofauti na ziara za Lowassa anazopanga kufanya nchi nzima...lengo lake ni kuhamasisha wafuasi wake kwa lengo fulani pamoja na kukijenga chama chake...

Vivyohivyo Mwenge lengo lake ni kufikisha ujumbe kwa wananchi kuhusu kuongeza jitihada katika mapambano dhidi ya UKIMWI, vita dhidi ya rushwa na ufisadi, vita dhidi ya dawa za kulevya na umuhimu wa kuitunza amani tulionayo...

Ndugu zangu...wanasiasa wanatuaminisha mambo mengi ya hovyo hasa wale wenye elimu ya hapa na pale ili wajinufaishe binafsi bila kuueleza ukweli...

Nimekuwa nikiona wananchi wanahamasika pale Mwenge wa uhuru unapokaribia kufika maeneo yao kwa kuchangia na kukamilisha miradi mbalimbali ya maendeleo ili izinduliwe na Mwenge...nimekuwa nikiona miradi kama zahanati, barabara na vituo vya afya ikikamilishwa haraka ili izinduliwe na Mwenge. Miradi hio unakuta isingekamilishwa kwa wakati na Halmashauri ila kama wanakuwa hawana miradi mizuri itakayozinduliwa au kuwekewa mawe ya msingi hupewa alama mbovu na hutakiwa baadae kujieleza...

Kupitia mbio za mwenge wa uhuru wanachi wananufaika sana...

Pia maendeleo ni gharama na Mwenge hugharimiwa kukimbizwa lakini gharama hizo sio kuuubwa kama tunavyoaminishwa kiaso cha kuona ni anasa...wananchi wenyewe huchangia kwa kuweka utaratibu wa namna ya kukimbiza mwenge katika maeneo yao...wakimbiza mwenge kitaifa hugharamiwa chakula na mafuta kwenye halmashauri husika wanapokabidhiwa...sio kwamba kuna mabilioni hutengwa na serikali kuu...hapana...
Ulichoeleza hapo juu ni tofauti na uhalisia unaojidhihirisha kwenye mikesha ya mwenge. Kwa lugha sahihi kinachofanyika kwenye mikesha ya mwenge ni kinyume na ulichokiandika. Kwenye mikesha ya mwenge hutawala ulevi wa kupindukia na ngono ambayo ndio chanzo cha maambukizi ya UKIMWI.
 
Ccm ni ccm na serikali ni serikali acheni kujitoka uj
ingà
Kwanini unasema ccm ni ccm, na serikali ni serikali! Rais na msafara wake mreeeefu walisafiri kwa magari ya chama au magari ya serikali? Mafuta yaliyotumika kwenye magari yaligaramiwa na chama au serikali? Acha kujitoa faham au kujifanya hujitambui.
 
Ccm ni ccm na serikali ni serikali acheni kujitoka uj
ingà
Nini unachokisema hapa?....Magu anasema amepata urais kwa sababu ya ccm. Anaongeza kusema wakuu wa mikoa na wilaya watekeleze irani ya ccm, wavae kijani kama alivyovaa kijani....fikiri mara mbili kabla ya kuposit....hii ndo ccm ya maigizo.

Umeona mchezo wa ccm zanzibar?
 
Back
Top Bottom