Mbinu za motisha kwa Walimu, kuajiri Walimu kutoka shule binafsi na kambi za kitaaluma zapelekea Simiyu chini ya RC Mtaka kuendelea kielimu

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,808
11,973
MTAKA AELEZA NAMNA MIKAKATI YA KUKUZA ELIMU SIMIYU ILIVYOZAA MATUNDA

1606377399434.png


Sekta ya Elimu Mkoani Simiyu imekuwa ikifanya vizuri katika kipindi hiki cha karibuni. Katika matokeo ya darasa la saba Mwaka huu 2020 Mkoa wa Simiyu umetoa shule 8 katika orodha ya shule zilizoongeza ufaulu kwa kiasi kikubwa kitaifa kwa muda wa miaka 3 mfululizo. Hii imepelekea Jamii Forums kufanya mahojiano na Mkuu wa Mkoa huo ili kutambua mikakati iliyotumika kuendeleza Elimu Mkoani hapo.

Akizungumza na Jamii Forums, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Antony Mtaka ameeleza mikakati mbalimbli iliyoweza kukuza Sekta ya Elimu Mkoani hapo.

Mtaka ameeleza kuwa ajenda ya kuipa Sekta ya Elimu kipaumbele ndiyo iliyopelekea kukuza ufaulu kwa madarasa yote Mkoani Simiyu. Amesema, Sekta ya Elimu ikiendelezwa itapelekea kukuza Sekta nyingine zote kama Kilimo, Ufugaji, Afya na Viwanda.

Ameeleza mazingira ya Mkoa wa Simiyu kwa Wanafunzi kuwa na changamoto mbalimbali ikiwemo Wazazi walio katika hali duni kutamani Watoto wao waache shule ili kuwapunguzia gharama. Hii upelekea Wazazi kuwaonya Watoto wao wakienda kufanya mtihani wa Taifa wahakikishe hawatofaulu.

Ameongeza kuwa Walimu wamekuwa wakifanya kazi tatu. Kazi ya kumjenga Mzazi atoe hamasa kwa Mtoto ili asome, kazi ya kumjenga Mtoto aweze kusoma na kazi ya kuhakikisha Mtoto anasoma na kufaulu.

Amesema, Mkoa wa Simiyu ni tofauti na sehemu nyingine kama Dar es Salaam ambapo Mtoto anapoanza darasa la kwanza anakuwa ameshasoma pre-nursery, ama akienda kuanza kidato cha kwanza anakuwa ameshasoma pre-form one. Hivyo basi kwa Simiyu inahitajika mikakati maalumu ambayo itamsaidia Mtoto kusoma.

Vilevile amesema Walimu walishapoteza matumaini kutokana na mazingira yaliyopo. Muda mwingine kunakuwa na mambo ya kimila ambayo wanakuwa wanafanyiwa Walimu. Hivyo ni lazima haya makundi matatu, Mzazi, Mwalimu na Mwanafunzi yaweze kuletwa pamoja na kushirikiana.

Amesema 2016 Simiyu ilikuwa ya mwisho kwa mitihani ya Taifa darasa la nne na la saba, kidato cha pili, cha nne na cha sita. Hivyo basi waliweka mikakati ya miaka mitano ambayo ingeweza kuwatoa kutoka hapo walipo hadi kufika namba moja.

Aidha Mtaka ameeleza kuwa mkakati wa kwanza ulikuwa ni kuleta motisha kwa Walimu kwani wamekuwa wakifanya kazi ambayo jamii haiwaungi mkono. Amesema Viongozi hawapaswi kuwa sehemu ya jamii hiyo, hivyo ni lazima walete nuru kwa Walimu ili waweze kufanya kazi yao katika mazingira mazuri.

Mkakati mwingine ni kuandaa kambi za kitaaluma ili kuhakikisha Wanafunzi walio katika kipindi cha mitihani kuhakikishiwa wanapata mazingira mazuri ya kusoma. Wanafunzi wamekuwa wakitumia madarasa kuweka kambi hizo baada ya muda wa kawaida wa masomo. Hii imesaidia kuwaepusha Wanafunzi na shughuli mbalimbali za nyumbani zinazowazuia kujisomea kipindi cha mitihani.

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa huyo amesema kuwa waliweza kufanya utafiti kwa kufuatilia shule binafsi zinazofanya vizuri namna zinavyojiendesha. Na kubaini kuwa Mwanafunzi wa sekondari kabla ya kufanya mtihani wa Taifa anakuwa ameshafanya mitihani ya kujiandaa zaidi ya 50-100, kwa shule ya msingi anakuwa amefanya wastani wa maswali si chini ya 6000. Hii ni tofauti kwa shule za Serikali, ambapo Mwanafunzi anakuwa amefanya mitihani si zaidi ya 7 kabla ya mtihani wa Taifa.

Vilevile ili kuweza kukuza ufaulu kwa Wanafunzi wanaofanya vibaya darasani mkakati mwingine ulikuwa ni kuwaajiri Walimu wazuri kutoka katika shule zinazofanya vizuri, kwa miezi mwili hadi mitatu. Walimu hao ni kwa ajili kuboresha matokeo kwa Wanafunzi.

Aidha ili kuongeza motisha ulianzishwa utaratibu wa kutoa tuzo kwa Walimu na Wanafunzi waliofanya vizuri. Ikipatikana A kwenye somo la kidato cha nne Mwalimu anapata 30,000, ikipatikana B anapata 10,000. Kwa kidato cha sita ikipatikana A Mwalimu anapata 50,000 na Mwanafunzi anapata 100,000.

Aidha Mtaka ametoa shukrani kwa Viongozi wote wa Mkoa Simiyu kwa ushirikiano wanaotoa katika kuendeleza Mkoa huo. Vilevile ametoa wito kwa Viongozi kutoa hamasa kwa Walimu na kuepuka kutoa kauli za kuwakatisha tamaa. Amesema lugha chafu kwa Walimu huwafanya wakate tamaa na kazi yao, na kupelekea kutofanya kwa ufasaha shughuli zao.

1606378069688.png
 
Huyu wa Mbeya yeye kila siku ni kuropoka tu

Kumbe huyu jamaa ni mdogo hivi!
 
I see,,sasa mbona anaonekana wa 70? au umbo linamfanya aonekane mkubwa?
 
Huyo ndiye MKUU WA MKOA KIJANA ambaye mh.Rais JPM alimtaja kuwa very dedicated,focused and Zealout....

Sishangai kwa mambo makubwa ayafanyajo kaka na kijana mwenzetu mh.Anthony Mtakachiganga....

Ninamtakia heri,baraka,afya njema,ulinzi mkuu wa Mungu Mwenyezi na mafanikio zaidi ya aliyoyafanya,aaamin aaamin.

Kudos Kamarade Anthony.


MAENDELEO HAYANA VYAMA
 
Huku Dar makonda alisema atawatandika viboko hasa wakiomba maslah yao! Simiyu walimu walikuwa wanapewa motisha! utafkiri ni Serikali mbili tofauti! hili kwa kweli halikuwa jambo zuri! mwisho wa siku analalamikiwa Rais wakati kuna watu hawawajibiki inavyotakiwa
 
HONGERA SANA ...SANA , MH. ANTHONY MTAKA ( RC - SIMIYU)

1.Natambua vema kuwa ,wewe ni kiongozi wangu usiyependa sana kupongezwa lakini naomba ukubali kuwa kupongezwa ni motisha( motivation)hasa pale mtu anapokuwa amefanya jambo lenye tija kwake binafsi na kwa jamii yake.

2.Naomba ukubali pia kuwa mimi si mtu si wa kwanza kupongeza utendaji wako uliotukuka na wenye matokeo chanya. Naomba ninukuu viongozi wangu wakuu wa Kitaifa waliopata kutoa pongezi kwako,

Kwanza, Mhe Rais Magufuli

" Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka ndio Mkuu wa Mkoa anayefanya kazi vizuri kutokana na ripoti niliyopewa na watu wangu .Wakati nikijaribu kutafuta wakuu wa wilaya na wakuu wa mikoa, walisema Mtaka hafai hata kuwa Mkuu wa Wilaya ila nilimpa ukuu wa Mkoa. Nimeuliza tena, hebu niletee ripoti ya wakuu wa mikoa wanaofanya kazi vizuri, wakaleta Mtaka ndio namba moja"

Wa pili, Dkt. Bashiru Ally, Katibu Mkuu wa C.C.M Taifa akiwa Mkoani Simiyu , Sherehe za NaneNane 2018, na Ziara ya kikazi Januari 05, 2019 ,alipongeza kuwa Mkoa wa Simiyu ndio unaoongoza kati ya mikoa yote kwa kufanya vizuri, kutokana na kuwapo kwa ushirikiano mzuri kati ya viongozi wa serikali na Chama Cha C.C.M.

Nami sasa naomba upokee pongezi zangu

3.Nakupongeza sana Mhe. Mtaka kama kiongozi uliyepokea kijiti cha kuongoza Mkoa kutoka kwa watangulizi wako wawili Mhe. Mabiti na Mhe. Mbwilo.Mkoa wenye miaka 8 tu toka kuanzishwa kwake kwa GN. Na 72 ya Machi 02, 2012 . Umekuwa dreva mzuri uliyefanikiwa kuhakikisha wananchi wako wote katika Mkoa wanakalia Kiti cha dereva. ( You put your customers on the driver's seat)

4. Baada ya kuteuliwa na Mhe . Rais Magufuli kuwa Mkuu wa Mkoa tarehe 13 Machi, 2016 na baada ya kuapishwa haraka sana ulifika katika Mkoa wako kesho yake majira ya saa 11 jioni na Ulifanya kikao kifupi cha dk 15 na viongozi wa Mkoa waliokupokea ,lkn maneno yako ya msisitizo yalikuwa,

" Nataka tufanye kazi kwa kukimbia sio kutembea. Kama mtu hana spidi ya kutatua changamoto za Mkoa huu, na spidi ya kuongoza maendeleo ya watu, tutamuacha njiani" Na kweli baada ya pale kila kitu umekuwa ukifanya sio kwa kutembea...ni mchakamchaka. Kila mmoja ni shuhuda.

5.Ulisema lazima Mkoa uwe na Strategic Plan(SP) .Tujue Mkoa uko wapi sasa na tunataka kwenda wapi. Ikawa hivyo.. Mkoa wa Simiyu una STRATEGY- The means to achieve the end. Mkoa una rubani anayejua ni nini mwelekeo- direction ya kule tunakokwenda na kuwa tutafika salama. Mkoa una nahodha anayeelewa vizuri meli inakwenda kutia nanga wapi.

6. Mwaka 2017 ulifanya kikao kikubwa cha wadau wa elimu katika Mkoa. Ulialika hata Wanazuoni na wabobezi wa masuala ya Elimu na taaluma na hata wazazi , kujadili ni kwa nini Mkoa unafanya vibaya katika Elimu , na kuwa tunafanya nini kuleta mabadiliko. Uliongoza strategies mbalimbali. Leo Simiyu ni moja ya mikoa kumi inayofanya vizuri Kitaifa katika taaluma. Matokeo ya mitihani ya wanafunzi msingi na Sekondari ni just performance indicators. Hongera sana team captain wetu.

7.Ni wewe, uliyehangaika kutafuta wafadhili ili kuwezesha kuandaa MWONGOZO WA UWEKEZAJI SIMIYU ili kuibua kitaalamu fursa za kiuchumi Simiyu. Ukafanikiwa ukishirikiana na viongozi wenzako wa Mkoa kupitia UNDP na ESRF Fursa za kulimo, biashara, utalii, uvuvi, viwanda na biashara ziliibuliwa.Fursa hizi zinatangazwa na wawekezaji wa ndani na nje tayari wamejitokeza na baadhi wameshawekeza. Hongera Sana, Mhe. Mtaka.

8.Umehamasisha ajira kwa vijana hasa kupitia kilimo cha umwagiliaji. Mradi Mkubwa wa Umwagiliaji ktk kijiji cha Mwasubuya ni mfano tosha. Mradi una eneo la ekari 514. Kampuni ya Agricom kwa juhudi yako imekubali kutoa mkopo wa zaidi ya milioni 200 ili kutoa machine za kupandia, kupalilia na kuvuna mpunga kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya kwa wakulima wapatao 198. Matarajio ni kuvuma kati ya magunia 30 na 42 kwa ekari. This is really Agricultural Revolution. Hongera sana bosi wangu Mtaka.

9 . Umeshawishi kuanzishwe Chuo Kikubwa cha Ufundi VETA Mkoani. Umehakikisha eneo la kutosha ekari 81.85 limepatikana, limepimwa na kupewa hati. Ujenzi unaanza muda wowote kutoka sasa. HONGERA KWA KAZI.

10. Unaendelea kusukuma na kuishawishi Serikali ijenge uwanja wa Ndege Simiyu.Eneo lilishaandaliwa katika kijiji cha Igegu, Kata ya Sapiwi- Bariadi.Usanifu wa awali na upembuzi yakinifu umekwishafanyika. Makadirio ya awali yanaonesha, ujenzi wa uwanja wa Ndege utagharimu bilioni 95. Uwanja huu hakika utaifungua Simiyu kiuchumi ikiwemo kuendeleza na kukuza utalii katika Mbuga ya Wanyama ya Serengeti.HONGERA SANA.

11.Umehakikisha Stendi ya Mabasi ya kisasa inajengwa Bariadi Simiyu yenye thamani ya shilingi bilioni 7.2 kwa ufadhili wa benki ya Dunia kwa ushirikiano na Serikali ya Mhe. Rais Magufuli. Stendi hii itaongeza ajira rasmi na zisizo rasmi na pia ni chanzo cha mapato ya Halmashauri ya Mji .HONGERA SANA MHE. MTAKA.

12 .Umesukuma, kwa kushirikiana na Serikali na Simiyu imepata bilioni 330 kwa ajili ya Mradi Mkubwa wa Maji kutoka ziwa Victoria. Huu ni Mradi Mkubwa wa Maji. Ifikapo mwaka 2025 wananchi wa Simiyu watakuwa wanapata maji safi na salama kwa asilimia 95. HONGERA SANA.

13. Umefanya ushawishi kwa nchi mbalimbali kupitia Balozi zao hapa nchini kuja kuwekeza Mkoani Simiyu.Balozi wa Indonesia nchini Prof. Ratlan Pardede ni alikuja Simiyu May 2018. Alioneshwa fursa zote za kilimo cha pamba, usafirishaji na viwanda. Alihakikishiwa kuwa uongozi wa Serikali za vijiji uko tayari kutoa ardhi buree ili kuvutia UWEKEZAJI. Wadau mbalimbali, wafanyabiashara kutoka nje na ndani wamefika Simiyu kwa minajili hii.Matunda ya hamasa hii yameanza kuonekana. HONGERA SANA MHE MTAKA. Balozi Prof. Ratlan aliahidi kufanyia kazi fursa hizo.

14. Umewezesha mazingira ya Mafunzo ya Matumizi ya mfumo wa IMIS ( INSURANCE MANAGEMENT INFORMATION SYSTEM) kwa wataalamu walioteuliwa kutoka Wilaya zote za Mkoa wa Simiyu. Sasa wanachama wote wa CHF Mkoa wa Simiyu wataweza kupata huduma popote nchini tofauti na awali ambapo walipata huduma katika vituo waliposajiliwa tuu. HONGERA SANA MHE.

15.Kunajengwa / kumejengwa viwanda vikubwa 3 vyenye uwezo wa kuajiri wafanyakazi 2000, kiwanda cha chaki, kiwanda cha vifungashio na kiwanda cha bidhaa 18 za Afya zitokanazo na pamba, achilia mbali viwanda vidogo 111 na vya kati 18 ambavyo vinaendelea kufanya kazi.HONGERA SANA

16 Zimejengwa nyumba za watumishi wa afya 345. Jumla ya watumishi 685 wanaishi kwenye nyumba hizi. This is unbelievable!!! HONGERA SANA MHE. MTAKA

17.Mkoa umejenga hospitali mpya 3. Itilima, Busega, na Bariadi. Vituo vya Afya 5 na zahanati 40 Zimejengwa kati ya 2015 na 2020. HONGERA SANA MHE MTAKA

18. Natamani watu wajue kazi na bidii yako katika kuujenga Mkoa wa Simiyu. Najua si bidii yako peke yako lakini lazima tukubali kuwa umekuwa ENGINE ya kufua umeme ili kufanya mifumo mingine ya gari ( Mkoa) ifanye kazi vizuri. Kazi uliyoifanya kwa miaka minne / mitano si ya kubeza bali kupongezwa ili upate ARI na MOTISHA ya kufanya vizuri hapo ulipo au hata kumsaidia Mhe . Rais Magufuli katika majukumu Makubwa zaidi ikimpendeza. INSHA'ALLAH MUNGU ATATENDA.

19 .Mara kadhaa ulitumia maneno ya Sr. M.D Ben Carson kuhamasisha watumishi wa Umma kunoa bongo zao na kuiwazia ufanisi Simiyu nje ya boksi. Ulipenda kitabu chake THINK BIG. Mie ni mmoja ya walioazima kitabu hicho kwako na kukisoma. Kama Ben aliweza kuwa daktari Bingwa from the scratch basi nasi twaweza kuifanya Simiyu kuwa TUNAVYOTAKA yaani kuipaisha kimaendeleo.

Pia, ulitumia maneno na falsafa ya Prof. Lumumba ,kuwa ukiweza kushinda katika kubadili mtazamo (ATTITUDE) hasi katika utendaji na utafutaji basi unaweza kuyafanya maisha yakutii wewe na si wewe kuyatii maisha.Ulihimiza na
Ulihamasisha wakati wote, wafanyakazi wa Umma kubadilika kifikra na kufanya kazi kwa bidii na kwa matokeo.

20. Pongezi sana kwa Mama Merciana Magati na Mzee John Mtaka Chiganga Kwa kukupa zawadi ya kukupokea duniani mwaka 1983. Mafanikio yako yamekuwa matunda ya bidii yako na MTAZAMO WAKO kuhusu dunia hii .

Ndimi

Kamara Beda
AFISA TAWALA
0769 587747
 
Back
Top Bottom