Mbinguni ni wapi?

Mbinguni ni wapi?

Da'Vinci

JF-Expert Member
Joined
Dec 1, 2016
Posts
36,007
Reaction score
108,557
Salute comrades,

Wakuu, naomba kufahamishwa, Mbinguni anapoishi Mungu ni wapi?

Ukisoma Biblia, Katekisimu etc zinasema Mungu yupo Mbinguni na mahali pote duniani. Je Mbinguni ni wapi?

Ni kule juu angani kwenye mawingu? Qur'an inasema zipo Mbingu saba na Mungu anaishi Mbingu ya saba, je Mbingu hiyo iko sehemu gani?

Pia tunaambiwa Nimrod na wenzie walijenga mnara ulikua unakaribia kufika Mbinguni kwa Mungu, je huko Mbinguni ni kule juu angani?

Kama Mbinguni ni huko juu angani mbona sasa hivi kuna vifaa mbalimbali ambavyo vinapita huko angani kwenda sayari zingine?

Mbona Mungu hayazuii kama alivyowazuia kujenga mnara wa Babeli sababu wanapita huko angani inaposadikika ndio Mbinguni.


Da'Vinci
 
Soma UFUNUO WA YOHANA 21:1--27.
Hayo yaliyomo humo hayajibu hayo maswali yangu mkuu halafu wengi hua hamkielewi huchi kitabu vuzuri nikipita wasaa nitakichambua...
1 Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya; kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza zimekwisha kupita, wala hapana bahari tena.
Ufunuo wa Yohana 21 :1

2 Nami nikauona mji ule mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, umewekwa tayari, kama bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa mumewe.
Ufunuo wa Yohana 21 :2

3 Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao.
Ufunuo wa Yohana 21 :3
 
MJUKUU WANGU MASWALI MENGINE NI YA KITAALAMU MNO.KUNA MASWALI MENGINE HUWA TUNAYAITA maswali ya milele HAYANA MAJIBU YA KUELEWEKA.
Wacha kudumaza ubongo hakuna kitu kisicho wezekana ukiweka nia thabiti...
 
mimi mwenyew na subiri majibu ya swali lako ...

maana tunasikia tu mbinguni mbinguni lakini hatujuibkuwa niwapi ..mbaya zaidi sehemu kubwa ya Jamii ambayo IPO mtaani inadhani kuwa mbingu nihuo mwanga wa jua wa blue tunaouona angani daily ...hata mimi zamani nilikiwa najua kuwa ile ndio mbingu na kwakuwa waislam wanasema kuwa mbingu ziko 7 nami nilikuwa nadhani kuwa baada ya ile Rangi ya blue tuionayo angani ambayo Jamii huwa inadhani kuwa ni mbingu basi juu yake patakuwa na mbingu nyingine 7
 
Salute comrades,

Wakuu, naomba kufahamishwa, Mbinguni anapoishi Mungu ni wapi?

Ukisoma Biblia, Katekisimu etc zinasema Mungu yupo Mbinguni na mahali pote duniani. Je Mbinguni ni wapi?

Ni kule juu angani kwenye mawingu? Qur'an inasema zipo Mbingu saba na Mungu anaishi Mbingu ya saba, je Mbingu hiyo iko sehemu gani?

Pia tunaambiwa Nimrod na wenzie walijenga mnara ulikua unakaribia kufika Mbinguni kwa Mungu, je huko Mbinguni ni kule juu angani?

Kama Mbinguni ni huko juu angani mbona sasa hivi kuna vifaa mbalimbali ambavyo vinapita huko angani kwenda sayari zingine?

Mbona Mungu hayazuii kama alivyowazuia kujenga mnara wa Babeli sababu wanapita huko angani inaposadikika ndio Mbinguni.


Da'Vinci
Samahani eee wakikwambia unishtue ni wapi mbinguni kwa Baba
 
Mbona mtoa mada unachanganya kati ya mbingu na universe

sayari zote,nyota,jua,Galax, mawe na vitu vyote vilivyo kwenye space kiujumla inaitwa THE UNIVERSE sasa katika iyo universe ndipo mwanadamu anao uwezo wa kwenda katika kila kimoja kasoro vitu vyenye changamoto ya kusogelewa kama jua

NB: katika vitu vinavyotengeneza The universe mbingu haipo ata kidogo kwaiyo unaposema binadamu anauwezo wa kwenda angani ni kusavei katika hii universe lakini sio mbinguni ambapo kwenda huko kunaitaji roho na mwili
 
Wacha kudumaza ubongo hakuna kitu kisicho wezekana ukiweka nia thabiti...
Ina maana wewe huna nia thabiti mbona hujaweza hayo maswali?. Acha kujifanya unaelewa kila kitu lkn Mungu hachunguziki....ok sasa wote hawataweza kujibu hayo maswali yako juu ya uchokonozi kwa Mungu sijui ndio utasema wote hatuna nia thabiti au dumedumaza ubongo?
 
Ina maana wewe huna nia thabiti mbona hujaweza hayo maswali?. Acha kujifanya unaelewa kila kitu lkn Mungu hachunguziki....ok sasa wote hawataweza kujibu hayo maswali yako juu ya uchokonozi kwa Mungu sijui ndio utasema wote hatuna nia thabiti au dumedumaza ubongo?
MAda yangu haileng kumchunguza Mungu bali mbingu
 
Mbingu ni ya blue ambayo huwa tunaiona kila siku
 
Back
Top Bottom