Oxpower
JF-Expert Member
- Jan 15, 2012
- 2,179
- 3,103
- Thread starter
- #61
Pole sana mkuuNi kweli pale pamekaa complicated sana, mimi kuna siku nilikuwa naenda huku Mbezi Maramba Mawili kwenye msiba natokea njia ya Goba, nilishazoea ukifika pale Mbezi mwisho baada ya round about unanyoosha moja kwa moja unavuka unaendelea na safari.
Nilivyofika pale kucheki pamezibwa kabisa, ikabidi nizunguke ile round about nielekee kama naenda stand ya Magufuli, shida nikaja nikaingia kwenye hili daraja la kwanza pale ambalo linaelekea stand ya daladala. Baada ya kuvuka tu kuna round about nyingine pale nikazunguka kama mara 3 hivi najaribu kutafuta exit ya kuelekea maramba mawili sioni, nikaona kuna entry moja inakuja toka uelekeo huo na haishuki, nyingine inaenda stand ya daladala, na moja inarudi barabara kubwa.
Ikabidi tu nirudi hadi barabara kubwa alafu ninyooke mpk kwa Yusuph ndiyo nikunje kushoto nitembee. Kifupi pale hapana maelekezo ya kutosha na yanachanganya kinoma, na traffic wamejaa pale wanasubiri ujichanganye wale kichwa. Nilivyofika kuwauliza wenyeji wangu wakanielekeza vizuri ambapo kimsingi nilitakiwa kuvuka kwenye daraja la pili baada ya kupita stand ya Magufuli ukiwa unatokea uelekeo wa Goba.
Sent using Jamii Forums mobile app

