MBEYA: Madiwani 3 wa CHADEMA wavuliwa uanachama

Kwa kifupi CHADEMA ni wanafiki sana walisema madiwani wao waunge mkono wakiwa huko huko bila kuhama vyama leo hii wameunga mkono juhudi za awamu ya tano za kuwaletea maendeleo wananchi wanait2a wasaliti!
Mimi hata siwaelewi elewi hawa jamaa.
 
Jaman hizi chaguzi zinamaliza hela.
Ni bora washindi wapili wao kipindi cha uchaguzi wapewe vijiti wamalizie muda uliobaki. Madaraja huku hatupewi wala madai yetu kazi mauchaguzi tu yasioisha.
Wanasiasa ni wabinafsi sana aiseh
Siasa za vyama ni pasua kichwa, sijui kwanini hawataki kuruhusu mgombea binafsi!
 
Kajigili hata mimi mwenyewe ningemvua uanachama , Msaliti kama yule katika kipindi kama hiki ambacho chadema inatendewa unyama ambao haumo hata kwenye filamu ya Sarafina , unawezaje kushirikiana na ccm ?

Halafu hapaswi kufukuzwa tu , inatakiwa ihamasishwe Mbeya yote atengwe na jamii , unawezaje kushirikiana na wauaji waliopanga hukumu ya Sugu hotelini ?
Mbona Meya Mh. Mwita huku dar hafukuzwi wkt kila siku anashirikiana na Kina Makonda tena Makonda anasema kabisaa tuko na mh. Mwita hapa amekuja kuiunga mkono serikali ya awamu ya 5 siasa za vurugu huko kwny chama chake hazipendi na ziara zote za Magu za uzinduzi hapo dar lazima Mwita awepo pia.
 
mbeya kimenuka. hizo kata zote ni za ccm.hapo wagombea wa upinzani watawekewa zengwe wote. hapo ni mwanzo wa mbeya kuangukia ccm.
 
Ktk kipindi chadema walitakiwa waonekane ni watu smart ni ktk utawala huu mgumu sana wa jpm.Lkn kwakua ni chama dhaifu na kilitegemea udhaifu wa awam iliyopita kujijenga kisiasa tunaona Chama kilivyo,yani kipo kipo tu.Huko chadema hakuna simba wa kupiga kelele serikal ilatikisika.Hali hii lzm itokee tu coz chama na wafuas wao saiz hawaendeshi na Sera,itikadi wala agenda yyt zaid ni kuvizia vitwt vya akina fatuma,zito,sarungi na mahasim wa ccm ndan ya chama ndio ziwe agenda.Chama hakieleweki kinasimamia nini na nini msimamo wao.Kwanini Madiwan na wabunge wasifike bei?Hakuna uzalendo tena huko chadema zaid ya watu kufanya siasa za kujitafutia umaarufu na maslai yao binafsi.

Utawala huu upinzani UTAPATA TABU SANA
 
unamuonea Mwaipalu bure , CCM imewanunua hawa siku nyingi tu kwa ahadi ya kuwarudisha kugombea , kama una akili kidogo tu rudia kumuangalia Kajigili kwenye mkutano ule wa Tulia , utajua kwamba alishajipanga kitambo tu , mimi ni miongoni mwa watu wa chadema tunaofuatilia mpango wa ccm mbeya , ninakuambia huku nikielewa vizuri mipango yote , Kuna ngazi hata ya kanda mbona hawakupeleka malalamiko huko ?

Katika chama chochote diwani ni mtu mdogo sana , hawezi kujipa kiburi kama cha Kajigili , kingine ni kwamba diwani anahusika kwenye kata yake , Muulize kajigili kama kata yake ilitengwa na jiji ambalo liko mikononi mwa chadema ?
Acheni kupiga ramli na kujifanya intelejensia yenu ilikua na taarifa.Kama mliyajua toka mwanzo mbona hamkumwaga hadharani?Leo wanaondoka na mzaanza kujifanya mlijua.
 
Si mchezo mgeni ndani ya siasa, bali ni mchezo uliozoeleka!
 
Dawa yake hiyohiyo ,ukipata tu taarifa ya mtu anataka kuacha uongozi,kuhama chama.unamuwahi unamtimua
 
Kajigili ni mshamba na mchumia tumbo wa hatari sana ! kapewa bia mbili tu na Dr Tulia kasahau tulikomuokota na kumpa udiwani , fukuza kabisa huyo
Afadhali wamemfukuza tu, kiukweli awamu hii hawa jamaa wamezidi kuendekeza Njaa! Basi tu, ila dawa ilitakiwa ndiyo watekwe na watu wasiojulikana!
 
Hivi hawa manahodha wa MV CHADEMA kengele yenye kuashiria kuwa chombo chazama hawaisikii tu,wamekula cha arusha hawa.
 
Aliyevuliwa uanachama ni Geofrey Kajigili wa Sisimba(hata barua ya yeye kuondolewa imesambaa mtandaoni)..Hakuna barua ya kuwavua uanachama Ngalawa na Mwatujobe..Hao wengine ni uzushi..Hata huyo Kajigili hakuna kikao cha chama kilichoazimia kuwavua uanachama..Ni utashi/maelekezo ya mtu mmoja tu...

Chadema jiji la Mbeya inaelekea kubomoka...
Ushafeli tayari kama unawaza chadema kubomoka Mbeya
 
Balantanda ,

..inaeleweka kwamba Dr.Tulia anataka kupora jimbo la Mbeya Mjini toka kwa Mh.Sugu.

..Je, huoni kwamba inaleta ukakasi Diwani wa CDM anapompa ushirikiano Dr.Tulia?

..sidhani kama Dr.Tulia angekuwa mwanachama wa CDM, angepata ushirikiano wa wana-CCM ktk jambo lolote.

..Na hao madiwani inapofika mahala wachague kati ya Dr.Tulia na CDM, wameamua kuchagua upande wa Dr.Tulia.

..Demokrasia yetu itaendelea kuwa na changamoto mpaka pale CCM itakapopoteza absolute majority iliyonayo ktk bunge la Jamhuri.
 
Back
Top Bottom