Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,768
- 218,389
Akizungumza mbele ya Maelfu ya Wananchi wa Kata ya Igawilo , Mwenyekiti wa Chadema Mbeya Mjini John Mwambigija , Amedai kwamba , Kufanya vibaya kwa timu ya soka ya Mbeya City kumechangiwa na tamaa ya viongozi wa Halmashauri hiyo ya kutafuna posho za wachezaji kwa lengo la kujigharamia wao kwenye safari zote za Timu hiyo.
Huku akishangiliwa na wananchi hao , Mwambigija anadai kwamba kuna kundi kubwa la madiwani na viongozi wa Halmashauri wanaoambata na timu hiyo kila inapokwenda kama sehemu ya kula bata , huku wakiambatana na mahawara zao , amesema timu inashuka daraja kwa sababu viongozi waliopaswa kuihudumia wameamua kutumbua hela za Timu .
Mwambigija amempongeza Mbunge wa zamani wa jimbo hilo Joseph Mbilinyi kwa kujitolea kununua kila goli ambalo Mbeya city watashinda kwa Tshs mil 1
Sent from my SM-J500H using JamiiForums mobile app
Huku akishangiliwa na wananchi hao , Mwambigija anadai kwamba kuna kundi kubwa la madiwani na viongozi wa Halmashauri wanaoambata na timu hiyo kila inapokwenda kama sehemu ya kula bata , huku wakiambatana na mahawara zao , amesema timu inashuka daraja kwa sababu viongozi waliopaswa kuihudumia wameamua kutumbua hela za Timu .
Mwambigija amempongeza Mbunge wa zamani wa jimbo hilo Joseph Mbilinyi kwa kujitolea kununua kila goli ambalo Mbeya city watashinda kwa Tshs mil 1
Sent from my SM-J500H using JamiiForums mobile app