Mbeya long time kitambo

Hivi pale town uhindini naskia soko liliungua sijui watu wakahama? Is it true
Yea liliungua 2012 kama sikosei siku hizi ni kiwanja tu pale kimezungushwa mabati. Nilikua huko miezi kadhaa iliyopita bado hapajajengwa
 
daah mwalimu Manase kafariki.
Duh, RIP mwl Manase. Alinifundisha hisabati std 5 mwaka 1991.Alikuwa mwl mzuri wa hisabati kipindi cha uhai wake. Nakumbuka alikuwa akiishi maghorofani jirani na stendi ya mabasi ya kwenda mkoani.
 
We wa home kabisaaaa
Niliishi jirani na familia ya Mapugilo pale kiwanja mpaka. True kabisa walikiwa watata hawa ndugu sio michezo. Ila Ibu alifariki ktk tukio la ujambazi nje ya Mbeya.
 
Bujibuji hapo namba sita umenikumbusha mbali sana. Mt. Livingstone ilikuwa bomba sana misosi yao babu kubwa na dining room yao ilikuwa inavutia sana. Disco lao pia lilikuwa bomba sana sijapita mitaa hiyo kipindi sasa.
 
Sina hakika lakini, za Bhanji ziliandikwa TRANS HIGHWAY CO. LTD
Huyo Bhanji ni mchumba tu, logistics company ya zamani ni Kanji Lalji Ltd wako pale jirani na Sisimba na pia wana yard yao kubwa Sinde jirani na Idara ya maji
 
Boss chipsi 300?watu tumeanza chips 100 ukinunua za 150 unakula wawili mpaka watatu na zinabaki
Usinikumbushe umetoka shule umechoka unanunua chipsi za mia unashushia na ulanzi
 
Hahahah loleza aka Loz watoto whiteee iyunga tuliwafaidi wakati Wa pini enzi zile.

Enzi zile ukivaa suruali ya khaki na tai nyeusi wanajua we Wa iyunga full heshima Kitaa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…