Mbeya kuna nini leo? JWTZ watanda mji mzima

Mbeya kuna nini leo? JWTZ watanda mji mzima

chalantai

Senior Member
Joined
May 20, 2013
Posts
121
Reaction score
29
Jamaa wana operation maalum leo vyombo vyote vya usafiri vinakaguliwa.

IMG-20150621-WA0000.jpg IMG-20150621-WA0001.jpg IMG-20150621-WA0003.jpg

Kama kichwa nimepata taarifa kinavyojieleza mbeya leo kuna wajeda mji mzima na kila gari linakaguliwa hata abiria wa daladala

Mwenye taarifa zaidi tafadhali!


 
Usihofu ni mazoezi tu ya kukabiliana na Ugaidi mazoezi kama hayo yalishafanywa hata huko SONGEA Raia wengi endeleeni na kazi kama kawaida vijana wenu wako kazini.
 
Mbongo mbona hamna ugaidi, au tumeumiss tunauita
 
Nimewaona hapa kwa mbilinyi, jirani na stendi ya nanenane nilihisi labda kuna magaidi wanatafutwa.
 
Kwa nini hili zoezi lifanyike kwenye mwaka wa uchaguzi? Hii isije ikawa ni mbinu ya kutia raia hofu

Raia wanapataje hofu mkuu.ninavyojua kipindi kuelekea uchaguzi huwa kuna pilipilika nyingi na ndo mana kipindi hicho mpaka rais mpya anapoapishwa matukio mengi kama vile ujambazi huwa yanatokea kwa wingi najua hapo jeshi letu linajiweka sawa pia kwa kushirikiana na polisi ili mambo yaende sawa
 
Kutisha tu wananchi, kwa nini wasifanye 2012 huko wanakuja kufanya leo karibu na uchaguzi
 
Raia wanapataje hofu mkuu.ninavyojua kipindi kuelekea uchaguzi huwa kuna pilipilika nyingi na ndo mana kipindi hicho mpaka rais mpya anapoapishwa matukio mengi kama vile ujambazi huwa yanatokea kwa wingi najua hapo jeshi letu linajiweka sawa pia kwa kushirikiana na polisi ili mambo yaende sawa

kama jwtz wanakagua ugaidi na ujambazi bac polisi waende wakalinde mipaka ya nchi
 
Kutisha tu wananchi, kwa nini wasifanye 2012 huko wanakuja kufanya leo karibu na uchaguzi

maandalizi ya 100% army standby. Maadui wanaongezeka.Sio lazima maadui wa nje LA hasha hata wa ndani.Echolima anajua.
 
Wakimbizi wanaingiza silaha za kivita kule Kigoma hawalioni, wao wanakagua wanawake wanaokwenda sokoni kwenye dala dala.
 
kama jwtz wanakagua ugaidi na ujambazi bac polisi waende wakalinde mipaka ya nchi

Mkuuwote tunajua polisi hata vituoni tu hawatoshi.kuna vituo unakuta polisi mmoja tu kituo kizima wengine wote ni polisi jamii.na kama nilivyosema awal wakati wa uchanguz kuna pilipilika nyingi polisi na kipindi polisi wanakuwa hawatoshi kabisa
 
kama jwtz wanakagua ugaidi na ujambazi bac polisi waende wakalinde mipaka ya nchi

Nadhani hufahamu vyema majukumu ya Jwtz, ngoja nikusimulie kua jeshi wanamajukumu ya kulinda nchi dhidi ya maadui wa ndani na nje,PIA wanajukumu la kusaidia mamlaka za kiraia ktk majanga na mahitajio mbalimbali pindi ikihitajika kufanya hivyo.
Reffer to;majanga ya mafuriko yaliowahi kutokea.
 
Kutisha tu wananchi, kwa nini wasifanye 2012 huko wanakuja kufanya leo karibu na uchaguzi

Mazoezi ya kijeshi yanafanyika kulingana na wakati stahki.tukio kubwa lililo mbele yetu ni uchaguzi.nchi nyingi zimeingia kwenye machafuko kupitia chaguzi zao.sio ubaya wa jeshi kujiwekea utayari
 
Back
Top Bottom