Mbeya: Jiji au Kijiji kikubwa?

Mbeya: Jiji au Kijiji kikubwa?

watu tunaangalia mapato habari za magolofa ndo useme jiji ilo hapana siku hizi kushangaa magolofa au majengo utaonekana kama mshamba
 
City Pub wana Chakula kizuri tuu na maeneo mengi wanayopika Chakula huko Soweto, Mafiati pale na mbele yake kama unaenda Mzumbe huko maswala ya lishe wapo vizuri maana miji mingi ina wageni ambao wanajikita na upishi na mambo mengine sio kweli kuwa wafanyabiashara wa Mbeya wote ni wenyeji wa Mbeya...
 
Nimefika Mbeya nimechoka mwenyewe. Nyumba nyingi siyo nzuri. Chakula kwenye migahawa usiseme. Yaani hamna kitu kwa kweli. Kazi ya ziada inahitajika. Bado saaaana
Kuna gorofa moja la angalau. Ni kijiji kikubwa kwangu!
 
mbeya haikuwa na hadhi ya kuitwa jiji sema kuna mhuni mmoja alikua na ushawishi kipindi hicho akatumia ushawishi wake kuita mbeya jiji wakati hata sehem za kula hamna. Ukitaka kula lazima uende city pub pekee otherwise jiandae kula kitimoto.
 
Nimefika Mbeya nimechoka mwenyewe. Nyumba nyingi siyo nzuri. Chakula kwenye migahawa usiseme. Yaani hamna kitu kwa kweli. Kazi ya ziada inahitajika. Bado saaaana
Kwani we ndugu yangu uliwahi kusafiri kwenda abroad mfano Bangkok, Shanghai Guangzhou, Singapore, Dubai, Kuala Lumpur, New York, Chicago,Los Angeles,Tokyo , Kyoto , selous, London, Paris , Berlin, Abu Dhabi n.k. Ukienda hukwo ulirudi Tanzania utasema Tanzania hamna jiji Bali kuna vijiji. Tanzania hakuna jiji lenye skyscraper nzuri , flyovershttps://m.youtube.com/watch?v=ajC4Ap0vzyI
[emoji327] MahaNakhon: Building Thailand's Tallest Tower | The B1M ...
 
Nadhani kuna sehemu sisi kama watanzania tunakwama sana.

Nani alisema uwepo wa wapishi wazuri wa chakula ni miongoni mwa vigezo vya sehem kupandishwa hadhi kuwa jiji?
Mbeya hakuna nyumba nzuri, uzuri wa nyumba ni nini? utakuta unajisifia tu lakini unakotoka nyumba nzuri zilizopo sio zenu ni za mashirika ya serikali au hotel za kitalii na wewe kwenu na wazazi wako mnakaa nyumba za tembe.

Kila sehem ina umaarufu wake na Jiji la Mbeya maarufu si kwa Majengo au upishi wa chakula.
Muhimu ukifika sehem shughulikia lililokupeleka kuliko kuanza kuchunguza mambo ambayo hayana msaada kwako,, au wewe ni afisa mipango miji?

Tumechoka na thread zenu za kuisema Mbeya , sisi wenyewe wana Mbeya tumeridhika na jiji letu maana Kisoka tupo vizur , kielim tupo vizur, nguo na viatu vinapatikana kwa wing na ubora mzur. Chakula na matunda ndio usiseme.

Mwisho. Ukiona Mbeya kuwa jiji wewe inakuuma sana nenda Mahakamani fungua kesi ya madai ya kutaka Mbeya iondolewe hadhi hiyo ili wewe uridhike.
 
Mmezidi kutusema, tutoleeni hiyo hadhi ya jiji basi mridhike. Nadhani kukosekana migahawa mizuri ni fursa ambayo mnatakiwa kuitumia na sio kuja kulalamika hapa.

Kuna miji mingine imejaa maghorofa ya serikali na mifuko ya jamii lakini unaona wakijilalamisha hapa kuwa mbeya ni kijiji kama vile hayo maghorofa huko kwao ni ya kwao. Nawashukuru NSSF kwa kutujengea kile kighorofa. LAPF nao wakitujengea jengo kama lile la Dodoma na NSSF kama lile la Moshi basi tutashukuru sana.

Nadhani ukitoa Mwanza, Mbeya ndio mji unaofuata kwa kuendelea kwa juhudi binafsi. Ni mji wa wakulima, hauna vivutio vya maana kufanya watu wajenge Hotel za nyota tano au kupokea wageni wengi walete pesa za kigeni. Ukilijua hili basi utaelewa kwanini mji wetu umekaa kishamba

Kama mtoa mada ulitegemea kukutana na migawahawa ya McDonalds au KFC kule Mbeya basi pole sana. Kule kwetu wengi ni wakulima kwahiyo kununua Chakula kwa hela nyingi haiwezekani. Hata Mall hakuna, ni mwendo wa kununua bidhaa sokoni tena kwa vipimo ambavyo kwenu hamna Mfano mchele kwa ndonya (kibaba).
 
Kwa kuongeza Mbeya ni mji ambao wakazi wake wengi wana uhakika wa milo mitatu tofauti na karibia miji yote Tanzania.

Kuna watu wanaishi Mbeya wanamaisha mazuri kushinda aliyeko Dar au hata pale Washington.

Thread yako haina mashiko unakejeli tu ,ungekuwa muungwana ungetoa mawazo nini kifanyike pia ili kuwe na hadhi nzuri zaidi ila umeishia kukeji tu,

Kila mji una mazuri yake na mapungufu yake , Kufika kwenye miji ya watu huna hata wiki unaanza kukejeli bila ushauri pia sio vizuri ,


By the way Dar ni kijiji kikubwa cha wala lala hoi. (Wengi wao)

Watu wa Mbeya wanaishi maisha mazuri sana kushinda wa Dar es salam .kwanini

Mazingira mazuri sana ya Mbeya
Hewa safi
Wengi wana uhakika wa milo mitatu
Wengi wana uhakika wa mahali pa kulala
Usafiri wao wa uma (daladala ) ni mzuri sana kushinda miji yote Tanzania.
Uhakika wa huduma ya maji
Kuna makazi mazuri sana Ituha ,iwambi ,forest ,isyesye na igawilo ya juu yenye hadhi ya Copenhagen


Usafiri wa barabara ,ngege na treni upo wa kuufikia mji.


Mbeya pale bana pako vizuri kiasi chake acha nongwa Mkuu

Pia uswahili nayo mbeya inayo mitaa kama isanga ,mabatini, ccm,Makondeko ,isengo ,majengo kule.



Mbeya ilipewa hadhi sababu ya idadi ya watu, pia mbeya hamna majengo marefu sababu ni eneo la bonde la ufa ,ni mji pia ulio telekezwa na serekali ya Mh Jiwe.

NB. Mimi sio mzaliwa wa Mbeya wala sijakulia Mbeya .Harakati za maisha zimenifanya tu nikujue.
 
Shida moja ya watu mnashindwa kutambua kuwa, ukizoea aina flani ya mapishi halafu ukaenda sehemu ingine lazima utapata tabu tu mwanzoni. Kila sehemu ina mapishi yao yaliyozoeleka, hata ukitoka dar ukienda New York mwanzo unaweza pata shida kwenye vyakura. Mi pia toka enzi hizo nimeingia dar mpaka leo napata shida sana, unakuta umeingia sehemu unauziwa supu kwa maandazi! Wakati mbeya nilizoea supu kwa ndizi ya kuchemsha!

Trust me ukikaa hapo mbeya zaidi ya week moja unaweza usitamani kurudi kwenu. Mifano ipo kuna watu walipangiwa kazi huko mwanzo walilalamaaa, lakini saizi hawataki hata kusikia ukiwambia wanahama lini.
 
Shida moja ya watu mnashindwa kutambua kuwa, ukizoea aina flani ya mapishi halafu ukaenda sehemu ingine lazima utapata tabu tu mwanzoni. Kila sehemu ina mapishi yao yaliyozoeleka, hata ukitoka dar ukienda New York mwanzo unaweza pata shida kwenye vyakura. Mi pia toka enzi hizo nimeingia dar mpaka leo napata shida sana, unakuta umeingia sehemu unauziwa supu kwa maandazi! Wakati mbeya nilizoea supu kwa ndizi ya kuchemsha!
Trust me ukikaa hapo mbeya zaidi ya week moja unaweza usitamani kurudi kwenu. Mifano ipo kuna watu walipangiwa kazi huko mwanzo walilalamaaa, lakini saizi hawataki hata kusikia ukiwambia wanahama lini.


Umeandika kitu kimoja kikubwa sana .Ukishaka mahala kidogo unazoea kila kitu.
 
Kwa kuongeza Mbeya ni mji ambao wakazi wake wengi wana uhakika wa milo mitatu tofauti na karibia miji yote Tanzania.

Kuna watu wanaishi Mbeya wanamaisha mazuri kushinda aliyeko Dar au hata pale Washington.

Thread yako haina mashiko unakejeli tu ,ungekuwa muungwana ungetoa mawazo nini kifanyike pia ili kuwe na hadhi nzuri zaidi ila umeishia kukeji tu,

Kila mji una mazuri yake na mapungufu yake , Kufika kwenye miji ya watu huna hata wiki unaanza kukejeli bila ushauri pia sio vizuri ,


By the way Dar ni kijiji kikubwa cha wala lala hoi. (Wengi wao)

Watu wa Mbeya wanaishi maisha mazuri sana kushinda wa Dar es salam .kwanini

Mazingira mazuri sana ya Mbeya
Hewa safi
Wengi wana uhakika wa milo mitatu
Wengi wana uhakika wa mahali pa kulala
Usafiri wao wa uma (daladala ) ni mzuri sana kushinda miji yote Tanzania.
Uhakika wa huduma ya maji
Kuna makazi mazuri sana Ituha ,iwambi ,forest ,isyesye na igawilo ya juu yenye hadhi ya Copenhagen


Usafiri wa barabara ,ngege na treni upo wa kuufikia mji.


Mbeya pale bana pako vizuri kiasi chake acha nongwa Mkuu

Pia uswahili nayo mbeya inayo mitaa kama isanga ,mabatini, ccm,Makondeko ,isengo ,majengo kule.



Mbeya ilipewa hadhi sababu ya idadi ya watu, pia mbeya hamna majengo marefu sababu ni eneo la bonde la ufa ,ni mji pia ulio telekezwa na serekali ya Mh Jiwe.

NB. Mimi sio mzaliwa wa Mbeya wala sijakulia Mbeya .Harakati za maisha zimenifanya tu nikujue.
You guys have to do something kwa ajili ya Mbeya. Yaani huu mji ukisikia habari zake ukiwa sehemu nyingine unaweza kusema Ulaya. Lakini ukifika na kujionea ndiyo utashangaa
 
Mmezidi kutusema, tutoleeni hiyo hadhi ya jiji basi mridhike. Nadhani kukosekana migahawa mizuri ni fursa ambayo mnatakiwa kuitumia na sio kuja kulalamika hapa.

Kuna miji mingine imejaa maghorofa ya serikali na mifuko ya jamii lakini unaona wakijilalamisha hapa kuwa mbeya ni kijiji kama vile hayo maghorofa huko kwao ni ya kwao. Nawashukuru NSSF kwa kutujengea kile kighorofa. LAPF nao wakitujengea jengo kama lile la Dodoma na NSSF kama lile la Moshi basi tutashukuru sana.

Nadhani ukitoa Mwanza, Mbeya ndio mji unaofuata kwa kuendelea kwa juhudi binafsi. Ni mji wa wakulima, hauna vivutio vya maana kufanya watu wajenge Hotel za nyota tano au kupokea wageni wengi walete pesa za kigeni. Ukilijua hili basi utaelewa kwanini mji wetu umekaa kishamba

Kama mtoa mada ulitegemea kukutana na migawahawa ya McDonalds au KFC kule Mbeya basi pole sana. Kule kwetu wengi ni wakulima kwahiyo kununua Chakula kwa hela nyingi haiwezekani. Hata Mall hakuna, ni mwendo wa kununua bidhaa sokoni tena kwa vipimo ambavyo kwenu hamna Mfano mchele kwa ndonya (kibaba).
Mbeya mliwahi sana kuitwa jiji.
 
Nimefika Mbeya nimechoka mwenyewe. Nyumba nyingi siyo nzuri. Chakula kwenye migahawa usiseme. Yaani hamna kitu kwa kweli. Kazi ya ziada inahitajika. Bado saaaana
Wewe kwenu wapi ? . Japo kama kweli unaitwa Lowasa bila shaka kwenu Monduli. Nadhani ingeanza kutujuza habari za kwenu kwanza kuliko kuanza kujifanya mchambuzi wa miji ya watu
 
Nimefika Mbeya nimechoka mwenyewe. Nyumba nyingi siyo nzuri. Chakula kwenye migahawa usiseme. Yaani hamna kitu kwa kweli. Kazi ya ziada inahitajika. Bado saaaana
Wewe utakuwa umeishia Chunya, vijiji vile vya Mtanila, maeneo ya Lupa tinga tinga.
 
Back
Top Bottom