Mbeya: Ashikiliwa na polisi kwa mauaji ya Mumewe

nasikia wanawake wa huko wana tabia kama wanaume wa kikurya when it comes to jabbing, ni kweli?
 
Jeshi la Polisi mkoani Mbeya linamshikilia mwanamke mmoja, Riziki Henry (22), mkazi wa Nditu wilaya ya Rungwe mkoani hapa kwa tuhuma za kumuua mume wake, Ayub Aron (33) baada ya kumpiga na kitu kizito kichwani.

Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya, Urlich Matei amesema leo Jumatatu Aprili 4, 2022 kuwa tukio hilo limetokea juzi majira ya alfajiri baada ya marehemu kupigwa na kitu kizito kichwani baada ya kutokea ugomvi.

Matei amesema kuwa baada marehemu kujeruhiwa na kukimbiza katika hosptali ya Wilaya ya Makandana, wilaya ya Rungwe alifariki dunia wakati akipatiwa matibabu kutokana na kumwagika damu nyingi.

Amesema kuwa chanzo cha mauaji hayo ni baada ya kutokea ugomvi kutokana na marehemu kumtuhumu mkewe kuchelewa kurejea nyumbani na alipohojiwa ndipo ulipozuka ugomvi.

Amesema kuwa mtuhumiwa anashikiliwa na polisi huku mwili wa marehemu ukiwa umehifadhiwa hosptali ya wilaya kwa ajili ya uchunguzi zaidi.

Kufuatia tukio hilo Kamanda Matei ameonya jamii kuachana na tabia ya kujichukulia sheria mkononi hususan kwa wanandoa ili kuepukana na migogoro isiyokuwa na tija inayosababisha vifo


Chanzo: Mwananchi
Miaka 22? Huyu so Binti mdogo kabisa? Ya kuua Mumeo yanatokea wapi? Bila shaka waliisha zoeshana kutwangana ndani ya nyumba! Leo Binti kamuwahi TU Mwenzie!
 
kumalizia maisha yako yote jela kwa Jambo unaloweza kuliepuka ni Ujinga.
Mali zinatafutwa.
Mimi wanawake wangu uwa nawaambia ukiona umenichoka wewe niambie tu tuachane.
Kuliko kufanyiana vituko.
Na kosa ambalo uwa sisamehi ni usaliti.simpigi ila kuachana tu.
zile harakati za kuachana tu,nazo ni mtihani mkuu,hususani muwe na hazina yakutosha,ni balaa. mnaanza kuviziana nani anatangulia kukata kauli ya kumwacha mwenzie. Soln ni kuvumiliana pale inapostahili .ikishindikana ,ondoka kaa mbali nae!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mambo ya kupigana na vitu vizito na vyenye ncha kali ni uhayawani.
 
Mkishindwana muachane kwa wema
we unadhani ni rahisi nyumba ambayo umejenga kwa kujitolea maisha yako yote kuibomoa na kuanza upya ?

hivi unajua wanaume tunasota sana kwa ajili ya familia zetu halafu mtu analeta mambo ya ajabu ajabu .

kama umeoa/umeolewa omba Mungu majaribu hayo yasikukute
 
Naona wanawake mwaka huu mmedhamiria kweli kweli! Ni kutupiga tu wanaume na vitu vizito kichwani! Alianza kupigwa Nduguway, wakaja Mataga na Sukumagang!

Na sasa wanawake wengine wameamua kurithi! Ukizubaa tu, unakuta 'kitu kizito' kimesha dondoshwa kichwani. Sijui tukimbilie wapi! Yaani mnaupiga mwingi kweli kweli.
 
Naona wanawake mwaka huu mmedhamiria kweli kweli! Ni kutupiga tu wanaume na vitu vizito kichwani! Alianza kupigwa Nduguway, wakaja Mataga na Sukumagang!

Na sasa wanawake wengine wameamua kurithi! Ukizubaa tu, unakuta 'kitu kizito' kimesha dondoshwa kichwani. Sijui tukimbilie wapi! Yaani mnaupiga mwingi kweli kweli.
Ole wao wanywao mvinyo mpaka usiku mwigi, vitu vizito vimechukua nafasi ya Covid!
 
Kama sio rahisi ndo utaenda jela kuwa mke wa nyapara
Uamuzi ni wako.
we unadhani ni rahisi nyumba ambayo umejenga kwa kujitolea maisha yako yote kuibomoa na kuanza upya ?

hivi unajua wanaume tunasota sana kwa ajili ya familia zetu halafu mtu analeta mambo ya ajabu ajabu .

kama umeoa/umeolewa omba Mungu majaribu hayo yasikukute
 
Back
Top Bottom