Lady Whistledown
JF-Expert Member
- Aug 2, 2021
- 1,024
- 1,614
Jeshi la Polisi mkoani Mbeya linamshikilia mwanamke mmoja, Riziki Henry (22), mkazi wa Nditu wilaya ya Rungwe mkoani hapa kwa tuhuma za kumuua mume wake, Ayub Aron (33) baada ya kumpiga na kitu kizito kichwani.
Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya, Urlich Matei amesema leo Jumatatu Aprili 4, 2022 kuwa tukio hilo limetokea juzi majira ya alfajiri baada ya marehemu kupigwa na kitu kizito kichwani baada ya kutokea ugomvi.
Matei amesema kuwa baada marehemu kujeruhiwa na kukimbiza katika hosptali ya Wilaya ya Makandana, wilaya ya Rungwe alifariki dunia wakati akipatiwa matibabu kutokana na kumwagika damu nyingi.
Amesema kuwa chanzo cha mauaji hayo ni baada ya kutokea ugomvi kutokana na marehemu kumtuhumu mkewe kuchelewa kurejea nyumbani na alipohojiwa ndipo ulipozuka ugomvi.
Amesema kuwa mtuhumiwa anashikiliwa na polisi huku mwili wa marehemu ukiwa umehifadhiwa hosptali ya wilaya kwa ajili ya uchunguzi zaidi.
Kufuatia tukio hilo Kamanda Matei ameonya jamii kuachana na tabia ya kujichukulia sheria mkononi hususan kwa wanandoa ili kuepukana na migogoro isiyokuwa na tija inayosababisha vifo
Chanzo: Mwananchi
Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya, Urlich Matei amesema leo Jumatatu Aprili 4, 2022 kuwa tukio hilo limetokea juzi majira ya alfajiri baada ya marehemu kupigwa na kitu kizito kichwani baada ya kutokea ugomvi.
Matei amesema kuwa baada marehemu kujeruhiwa na kukimbiza katika hosptali ya Wilaya ya Makandana, wilaya ya Rungwe alifariki dunia wakati akipatiwa matibabu kutokana na kumwagika damu nyingi.
Amesema kuwa chanzo cha mauaji hayo ni baada ya kutokea ugomvi kutokana na marehemu kumtuhumu mkewe kuchelewa kurejea nyumbani na alipohojiwa ndipo ulipozuka ugomvi.
Amesema kuwa mtuhumiwa anashikiliwa na polisi huku mwili wa marehemu ukiwa umehifadhiwa hosptali ya wilaya kwa ajili ya uchunguzi zaidi.
Kufuatia tukio hilo Kamanda Matei ameonya jamii kuachana na tabia ya kujichukulia sheria mkononi hususan kwa wanandoa ili kuepukana na migogoro isiyokuwa na tija inayosababisha vifo
Chanzo: Mwananchi