Mbatia aombe kazi ya uchungaji kkkt. anajua kuimbisha nyimbo za kanisani hadi anaimbisha kwenye mikuno ya siasa nyimbo za kanisani. uongozi wa siasa umemshinda hadi chama chake nccr kimekufa. amebaki kazi kujipendekeza chadema na kwa sasa yeye ni nyumbu mfuata malisho. jpm ndio champion.. hayo mapapa anayodai mbona mengi yashatumbuliwa. mbatia anafikiri watu hawayajui mafisadi papa. inaelekea jinsi jpm anavyotumbua majipu ndio mbatia et al wanashikwa na kiwewe.RAIS John Magufuli anakabiliwa na tuhuma za ubadhirifu, jambo hilo linamwondoa kwenye orodha ya watu wasafi kama anavyotaka ifahamike hivyo,anaandika Pendo Omary.
James Mbatia, Mwenyekiti wa Chama cha NCCR- Mageuzi amemtaka Rais Magufuli kujisafisha kutokana na kashfa ya kuhusika katika kuuza nyumba za serikali kabala ya kusafisha watuhumiwa wengine wa ufisadi.
“Rais Magufuli anapaswa kujisafisha mwenyewe kwanza kutokana na kashfa inayomuhusu ya uuzwaji wa nyumba za serikali,” amesema Mbatia.
Akizungumza leo jijini Dar es Salaam katika mkutano na waandishi wa habari, Mbatia amesema “tumeona ni kwa namna gani Rais Magufuli anahangaika kupambana na ufisadi au uhujumu uchumi kwa kutumia nguvu kubwa kwa vidagaa na kuacha mapapa kama wale wa Tegeta ESCROW, Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere ‘Terminal III’, makontena bandarini, IPTL, Richmond na Mradi wa Umeme wa Kinyerezi.
“Hivyo rais anapaswa kujisafisha kwanza kwa kuwa na yeye anatajwa kuhusika katika kashfa ya uuzwaji wa nyumba za serikali,” amesema Mbatia.
Mbatia amesema, katika kufanikisha hayo Rais Magufuli anapaswa kuacha kuongoza nchi kwa matamko badala yake aongoze kwa kufuata Katiba, Sheria na Kanuni za Nchi.
“Demokrasia imeendelea kukiukwa huku uhuru wa kujieleza ukiendelea kudidimizwa. Kutokana na hali hiyo, nchi sasa iko kwenye hali mbaya katika; bunge kuingiliwa, hali ya maisha ya Watanzania kiusalama iko njia panda hususani Zanzibar.
Pia, kuna ukiukwa kwa haki za wananchi kutafuta na kusambaza taarifa na matumizi ya nguvu za dola kupitia Jeshi la Polisi kwa kuzuia mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa vya upinzani.
Aidha, amesema Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho (NEC) imebaini athari za kiuchumi zitokanazo na uamuzi wa viongozi kufuatia matamko mbalimbali ya serikali.
Miongoni mwa athari hizo ni kupungua kwa mzigo bandarini ikiwa ni sambamba na watumiaji wa bandari wakihamia nchi jirani.
Chanzo: Mwanahalisi
Kiwewe kipi ? Zipo wapi zile bilion 252 zilizopotea wizara ya ujenzi Kwa kuwalipa makandarasi Hewa? Kivuko cha Azam kipya kilinunuliwa bilion 5 tu, lakini kivuko chakavu cha Dar Bagamoyo kikanunuliwa Kwa bilion 8, huku nyumba za serikali baba yako alijiuzia kibao mpaka akagawa zingine bure , unatakiwa Mbatia akae kimya Kwa hili ?Mbatia aombe kazi ya uchungaji kkkt. anajua kuimbisha nyimbo za kanisani hadi anaimbisha kwenye mikuno ya siasa nyimbo za kanisani. uongozi wa siasa umemshinda hadi chama chake nccr kimekufa. amebaki kazi kujipendekeza chadema na kwa sasa yeye ni nyumbu mfuata malisho. jpm ndio champion.. hayo mapapa anayodai mbona mengi yashatumbuliwa. mbatia anafikiri watu hawayajui mafisadi papa. inaelekea jinsi jpm anavyotumbua majipu ndio mbatia et al wanashikwa na kiwewe.
Yapasuliwe!Majipu mengine hayatumbuliki.
Ngosha hayo hayawezi na kuna mengine mengi kama hayo! Hayawezi. Mfano; epa, meremeta.Hiv Escrow imeishia wap ,Richmond je ?
Kwanini yeye msafi?!RAIS John Magufuli anakabiliwa na tuhuma za ubadhirifu, jambo hilo linamwondoa kwenye orodha ya watu wasafi kama anavyotaka ifahamike hivyo,anaandika Pendo Omary.
James Mbatia, Mwenyekiti wa Chama cha NCCR- Mageuzi amemtaka Rais Magufuli kujisafisha kutokana na kashfa ya kuhusika katika kuuza nyumba za serikali kabala ya kusafisha watuhumiwa wengine wa ufisadi.
“Rais Magufuli anapaswa kujisafisha mwenyewe kwanza kutokana na kashfa inayomuhusu ya uuzwaji wa nyumba za serikali,” amesema Mbatia.
Akizungumza leo jijini Dar es Salaam katika mkutano na waandishi wa habari, Mbatia amesema “tumeona ni kwa namna gani Rais Magufuli anahangaika kupambana na ufisadi au uhujumu uchumi kwa kutumia nguvu kubwa kwa vidagaa na kuacha mapapa kama wale wa Tegeta ESCROW, Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere ‘Terminal III’, makontena bandarini, IPTL, Richmond na Mradi wa Umeme wa Kinyerezi.
“Hivyo rais anapaswa kujisafisha kwanza kwa kuwa na yeye anatajwa kuhusika katika kashfa ya uuzwaji wa nyumba za serikali,” amesema Mbatia.
Mbatia amesema, katika kufanikisha hayo Rais Magufuli anapaswa kuacha kuongoza nchi kwa matamko badala yake aongoze kwa kufuata Katiba, Sheria na Kanuni za Nchi.
“Demokrasia imeendelea kukiukwa huku uhuru wa kujieleza ukiendelea kudidimizwa. Kutokana na hali hiyo, nchi sasa iko kwenye hali mbaya katika; bunge kuingiliwa, hali ya maisha ya Watanzania kiusalama iko njia panda hususani Zanzibar.
Pia, kuna ukiukwa kwa haki za wananchi kutafuta na kusambaza taarifa na matumizi ya nguvu za dola kupitia Jeshi la Polisi kwa kuzuia mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa vya upinzani.
Aidha, amesema Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho (NEC) imebaini athari za kiuchumi zitokanazo na uamuzi wa viongozi kufuatia matamko mbalimbali ya serikali.
Miongoni mwa athari hizo ni kupungua kwa mzigo bandarini ikiwa ni sambamba na watumiaji wa bandari wakihamia nchi jirani.
Chanzo: Mwanahalisi
Acha kusapoti maovu kwa hoja dhaifu eti SUMAYE!! SUMAYE ni nani hapa Tz? Tz kwanza SUMAYE au MAGUFULI baadae awe SUMAYE au LOWASSA au JK au CHENGE YOYOTE alie tupiga hela awajibike.uuzwaji hovyo Wa Nyumba za serikali!!!! hoja ya kijinga kabisaaaa!!!ebu mh mbatia muulize mh sumaye akupe Maelezo vizuri!!yawezekana wakati mchakato unaendelea wewe ulikuwa darasani ukibukuwa!!!kama ziliuzwa kiholela basi wakulaumu ni mh sumaye kwa kushindwa kusimamia vizuri mawaziri na Mali za serikali/umma!!vinginevo Mzee ikujiabisha unapoleta hoja kama hii wakati wakukupa jibu umekaa naye mezani na anagombea uenyekiti huko chadema
Anatafuta kiongozi msafi? kweli hoja naona zimefika mwisho......Mheshimiwa Mbatia unaheshimiwa sana tafadhali usijishushe hadhi yako kwa matamko ambayo hayatarajiwi toka kwako.
JPM hakuwahi kuwa na uwezo wa kuuza nyumba au mali yoyote ile ya serikali. Kwenye kuuzwa nyumba za serikali rightly or wrongly ilikuwa uamuzi wa baraza zima la mawaziri chini ya rais. Na hili lilifikiwa baada ya mjadala mrefu kuhusu nyumba hizo. Hivyo basi kumlaumu JPM eti kwa vile ametekeleza wajibu wake kisheria ni kutomtendea haki kabisa.
Kama unatafuta wa kumlaumu mbona Mzee Ben humchokozi? Tatizo la Escrow lilikuwa la kisheria mno na kwa mtu kama wewe unalifahamu vizuri sana.
Hisia zangu, rightly or wrongly ni kuwa huyu JPM anawanyima raha jinsi anavyokubalika na umma na kwa kiasi fulani mnahisi mkiendelea kunyamaza kimya basi mtakuwa hamna ajenda na hili ndiyo maana mara mnafunga midomo yenu, mara naibu spika hamumtaki[taratibu za kumng'oa mnazijua lakini hamfuati hizo].
Ushauri wangu ni kwamba kwa sasa tulieni. JPM yuko honeymoon. wananchi wengi wanamkubali na wanaamini kuwa muelekeo wa serikali yake ni mzuri kwao na honeymoon ikiisha mtapata tu mada za kuzungumzia.
Na pia meno hayadhuru ulimi!Kamwe kidole hakiwezi kulidhuru jicho