TUKUTUKU
JF-Expert Member
- Sep 14, 2010
- 11,765
- 4,033
Mgombea ubunge wa jimbo la kawe kwa tiketi ya chama cha NCCR MAGEUZI,bwana james mbatia,ametishia kwenda mahakamani ili kukabiliana na kile alichokiita kudhalilishwa na mgombea ubunge wa jimbo hilo kwa tiketi ya CHADEMA,Halima mdee.Mbatia analalamika kuitwa mamluki wa CCM,na aliyepandikizwa kugawa kura za upinzani katika jimbo la kawe.Mbatia pia anamlalamikia mkurugenzi mtendaji wa chama cha waandishi wa habari wanawake (TAMWA),Ananilea Nkya akidai alitoa maneno ya uzushi,uongo na udhalilishaji dhidi yake kwamba amekuwa akiwadhalilisha wanawake.(Tanzania Daima,26 October 2010,u.k 3)
My take
Naona sasa Mbatia maji shingoni,amebaki kulalamika tu, bila sababu za msingi,kwa kuwa ukichunguza vizuri utagundua maneno anayodai aliambiwa ni maneno ya kawaida ya siasa na hasa kambi ya upinzania,imekuwa ni jambo la kawaida kutuhumiana kwamba chama furani,au kiongozi furani ni mamluki wa CCM.
My take
Naona sasa Mbatia maji shingoni,amebaki kulalamika tu, bila sababu za msingi,kwa kuwa ukichunguza vizuri utagundua maneno anayodai aliambiwa ni maneno ya kawaida ya siasa na hasa kambi ya upinzania,imekuwa ni jambo la kawaida kutuhumiana kwamba chama furani,au kiongozi furani ni mamluki wa CCM.