Mbatia 'aipa' CCM ushindi kuongoza Halmashauri ya Uvinza

Mbatia 'aipa' CCM ushindi kuongoza Halmashauri ya Uvinza

Mchele mchele wa Rais.....kazi kweli kweli

"Duniani hakuna kitu cha bure" Kimweri alisema.
Kila mtu anayo naman ya kulipa "cha bure"
Ila sijaelewa WABUNGE wanawake wanaoteuliwa wanalipaje???
TAFAKARI.
 
Dawa ya moto ni moto..... Ukiua kwa panga utauawa kwa panga
 
Kitendo cha Mkiti wa NCCR James Mbatia kukataa makubaliano yaliyokuwa yamefikiwa kati ya NCCR na CHADEMA kuongoza halmashauri ya Uvinza yamesababisha CCM kutumia mwanya huo na kutwaa nafasi ya Makamu Mkiti wa Halmashauri hiyo.

Kwa upande wa nafasi ya Mkiti uchaguzi umeahirishwa hadi utakapotangazwa tena baada ya vyama vyote vitatu kushindwa kupata theluthi mbili ya kura.

Katika nafasi ya Mkiti vyama vyote vitatu viliweka wagombea ambapo CCM ilipata kura 8 CHADEMA kura 7 na NCCR kura 6.

Nafasi ya Makamu Mkiti mgombea wa CCM hakuwa na mpinzani na alipita bila kupingwa.

Katika makubaliano ya awali ngazi ya wilaya na mkoa vyama vya NCCR na Chadema vilikubaliana kuachiana nafasi ambapo ilukubaliwa CHADEMA igombee nafasi ya Mkiti na NCCR Makamu Mkiti.

Katika hali ya kushangaza siku ya kurudisha fomu vyama vyote viwili vilirudisha fomu nafasi ya Mkiti na NCCR ikakataa kugombea nafasi ya Makamu Mkiti hivyo mgombea wa CCM akapita bila kupingwa.

Inadaiwa Mkiti wa NCCR James Mbatia ndiye aliingilia kati kuvunja makubaliano ya vyama hivyo na hatimaye ushindi ukawa upande wa CCM

Mbatia na kauli yake 'Mama yetu tanzania' ni janga jingine.
 
Mbatia kafanya jambo jema tu. Kama ambavyo Chadema walivyogoma kwenye kuunda kambi ya upinzani ndivyo ambavyo NCCR walivyogoma.
 
mkuu, chadema ni waroho sana. Wao wanajua kuwa kigoma ni ngome ya nccr, badala ya wao chadema kuwaachia nccr nafasi hiyo ya umeya, wao ndo wanaitaka. Vinginevyo wangekubaliana mapema. Nccr wagombee umeya na chadema wawaunge mkono na chadema wangegombea unaibu meya na nccr wawaunge mkono. Nadhani hapo wakepata wote. Vinginevyo kwa uroho huu watakosa wote

cdm si waroho kama usemavyo, walikubaliana kuwa chama kitakachosimamisha mwenyekit kitaongoza kamat 1 na makam 2, nccr wakakubal makam bt at the end wakaleta jina kwa nafas ya mwenyekit, na cdm nao, so maajabu yasingeweza kutokea kwa nccr na cdm kushinda, mi ni cdm bt naona ni bora wakawaachia ccm au nccr kuongoza kwan mbatia ameweka wazi kutokukubal ushirikiano na sidhan kama kuna cdm atakayepiga kura kwa ccm au nccr,na wakiendelea kupiga kila mmoja kwa chama chake no one can lead, nccr na ccm waungane tu cdm tusubiri 2015.busara itumike kwan mbatia ameonesha kuunga mkono ccm.
 
Gamba side be

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Molemo, chadema ni waroho wa madaraka, wabinafsi, na mnataka kuwaona wenzenu ni wajinga kumbe nyie machadema ndio majinga ya mwisho kabisa, kambi ya rasmi ya chadema bungeni ndio funzo kuu kwenu manyang'au nyie

Hivi kati ya mjinga wa kwanza na mjinga wa mwisho, yupi ana afadhari??
 
Hata hivyo Chadema tulikosea kufikiria Mbatia(mbunge Wa JK) Na chama anachokiongoza waweza kuwa wadau Wa kutetea wananchi
 
Hivi wana jf na Chadema mlitegemea nini hapo,Mbatia kuipa CDM uongozi? hili suala lilikuwa wazi iwe hivyo chini ya M/kiti Mbatia,NCCR ingekuwa inaongozwa na mtu tofauti anayejua na kuheshimu upinzani hapo ingepasa tulalamike lkn kwa Mbatia,tuseme tu ila tusiumize vichwa CDM wajipange uchaguzi ujao wafanye kweli wakae chonjo na huyo mlipa fadhila.
Mbatia huyu recently alisema hakubaliani na uanzishwaji wa Red Brigade. Sasa mtu wa namna hii alitegemewa aunge mkono mahali penye Chadema? Kwanza angewashukuru NCCR Kigoma otherwise chama chake kingekuwa na mbunge mmoja ambaye ni yeye anayeshindana na wabunge wa viti maalum.


Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Saafi sana NCCR mmeonyesha ukomavu wa kisiasa
 
Mbatia analipa fadhila kwa Mwenyekiti wa CCM-Taifa kwani suala la kuteuliwa kuwa Mbunge si dogo kwake.Hapo ndipo ninapokubaliana na Kafulila kwamba Mwanaume aliyeshindwa na Mwanamke katika nafasi ya Ubunge hawezi kukiongoza chama ipasavyo!

Kauli yako ni ya kipuuzi...mwanamke hawezi kuongoza? wewe huna mama? Mama yako hawezi kuongoza? Disgrace you are
 
kabiiisa kabiiiisaaa mkuuu..me nasema bora fenesi likikomaa likiiva linatoa harufu kuliko parachichi mpaka lina oza...njaa zitamua tuu..
 
Kitendo cha Mkiti wa NCCR James Mbatia kukataa makubaliano yaliyokuwa yamefikiwa kati ya NCCR na CHADEMA kuongoza halmashauri ya Uvinza yamesababisha CCM kutumia mwanya huo na kutwaa nafasi ya Makamu Mkiti wa Halmashauri hiyo.

Kwa upande wa nafasi ya Mkiti uchaguzi umeahirishwa hadi utakapotangazwa tena baada ya vyama vyote vitatu kushindwa kupata theluthi mbili ya kura.

Katika nafasi ya Mkiti vyama vyote vitatu viliweka wagombea ambapo CCM ilipata kura 8 CHADEMA kura 7 na NCCR kura 6.

Nafasi ya Makamu Mkiti mgombea wa CCM hakuwa na mpinzani na alipita bila kupingwa.

Katika makubaliano ya awali ngazi ya wilaya na mkoa vyama vya NCCR na Chadema vilikubaliana kuachiana nafasi ambapo ilukubaliwa CHADEMA igombee nafasi ya Mkiti na NCCR Makamu Mkiti.

Katika hali ya kushangaza siku ya kurudisha fomu vyama vyote viwili vilirudisha fomu nafasi ya Mkiti na NCCR ikakataa kugombea nafasi ya Makamu Mkiti hivyo mgombea wa CCM akapita bila kupingwa.

Inadaiwa Mkiti wa NCCR James Mbatia ndiye aliingilia kati kuvunja makubaliano ya vyama hivyo na hatimaye ushindi ukawa upande wa CCM


Mbatia na ccm ni kitu kimoja,sikutarajia kama angefanya kinyume na hili alilolitenda.Hizo ndizo Changamoto za kisiasa.
 
Chadema isirudi tena kushirikana na vyama vilivyofunga ndoa na ccm maana hao sio wapinzani tena.
 
Mbatia na ccm ni kitu kimoja,sikutarajia kama angefanya kinyume na hili alilolitenda.Hizo ndizo Changamoto za kisiasa.

Lakini mwisho wasiku hii issue haimuathiri Mbatia wala NCCR ila itakula kwa wana Kigoma, kama zitto, kafulila na wengineo wameshinda kukubaliana na kuweka Kigoma kwanza basi shahuri yao.
 
Nani umemuona analia? sisi hatutaki Vyama ambavyo vimeolewa na CCM

NCCR hawezi kuolewa na CCM kwani ni mdogo sana kwake. Huyo ni mtoto tena wa kambo. Mke wa CCM anafahamika unless useme CCM wamejiingiza kwenye uchangu...

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
"Duniani hakuna kitu cha bure" Kimweri alisema.
Kila mtu anayo naman ya kulipa "cha bure"
Ila sijaelewa WABUNGE wanawake wanaoteuliwa wanalipaje???
TAFAKARI.

Wabunge wanawake hawana cha kulipa kwa kuwa hiyo ni affirmative action ya kuwafanya wanawake watambulike. Labda tujiulize mbunge mwanamume wa kuteuliwa kama James Mbatia analipaje.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom