Mazishi kwa kuchoma moto mwili wa marehemu( cremation)

Mazishi kwa kuchoma moto mwili wa marehemu( cremation)

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
359,869
Reaction score
828,403
Wiki iliyopita niliongoza ibada fupi na zoezi la kuchoma mwili wa raia mmoja wa nje pale Makumbusho
Zoezi lile lilinikumbusha mbali sana enzi za ujana wangu huko ughaibuni nilipokuwa nalifanya kwa raha zangu
Japo kwasasa inachukuliwa kama njia ya kuokoa nafasi lakini haya ni mazishi ya kimapokeo na kiimani kwenye hizi dini zinazoabudu miungu
Dhana kubwa hapa ni kuifanya roho iuachilie mwili na kuwa huru kwenda kuingia kwenye hatua nyingine ya maisha ( reincarnation, rebirth ama into realms)
Mazishi mengine ya kimapokeo ni kuuhifadhi vizuri mwili kwenye vifaa ambavyo vitafanya mwili usihabike kwa imani kwamba kuna siku uhai wake utarejea
Na mengine ni kuukausha mwili au kuuweka kwenye kichanja ili uwe chakula cha ndege na wanyama wengine
Sasa hili la kuchoma pia lina namna na taratibu zake kulingana na imani husika

Wakati Wahindu wakiamini katika kutanguliza miguu kwenye tanuru la moto wachina wao wanaamini kwenye kutangliza kichwa

Dhana ya kutanguliza miguu.. Ulikuja duniani ukitanguliza kichwa sasa utarudi kwa kutanguliza miguu kwakuwa unaweza kutembea sasa!
Dhana ya kutanguliza
kichwa kwenye tanuru
Ulitanguliza kichwa ulipokuja duniani, utatanguliza kichwa utakapoondoka

Laiti kama yale matanuru yangekuwa ya vioo. Hakika tungejionea maajabu namna mwili unavyopokea moto kwa mara ya kwanza katika ufu wake na vile unavyoteketea mpaka unakuwa jivu
Ukitanguliza miguu nyama zote za miguuni hupanda mpaka kiunoni na kuendelea kuungua hadi kichwani.. Lakini ukitqnguliza kichwa nyama zote kichwani hujivuta pia mpaka kiunoni na kuendelea kuteketea kuelekea miguuni

Umegundua nini hapo!! Kiuno ndio centa bolt ya mwili.. Ndio maana kuna mpemba baada ya kuzinduka hospitali akauliza ameumia wapi na wapi
Madktari wakamwambia amekatwa miguu yote.. Akauliza na kiuno je? Akaambiwa hicho kimesalimika😆 Huwezi kuamini alifurahi mno!
 
Hizo tamaduni hazipo kwenye Jamii yetu ya Kitanzania, huku kwetu tuna imani kwamba marehemu hana kosa

Na kitendo cha kuchoma moto maiti kinatafsiriwa kama ni ukatili dhidi ya maiti

Ndiyo maana kwa miaka yote hii, Mchaga, Mkinga, Mjaluo n.k wote wanachimbiwa kabuli kwaajili ya kuhifadhi miili yao iwapo watakuwa wamekufa

Tunauishi msemo wa "adhabu ya kaburi, aijuaye maiti"

Sasa kuanza kuchomana maiti moto, si italeta tafsiri tofauti 🙌
 
Back
Top Bottom