Bro alikua anapiga hizo mbanga kuweka makaratasi kwenye gazette lililokunjwa kisha inatokea misimbazi kadhaa kisha anairudisha ilipotoka michezo ya kucheza na kitambaa kisha linatokea ua (njiwa) lilikua sio jambo la hatari kwake na aliwahi kutuonyesha michezo ya kuleta ndizi, embe mpaka majani ya chai tena majani ya chai nakumbuka aliruhusu tupikie chai tunywe na tukafanya hivyo kutoka kusikojulikana ni ilikua jambo la kawaida kabisa, sasa alipomaliza shughuli zake town akarudi bush kule hawakumuelewa unajua siku zote nabii hakubaliwi nyumbani kwao na professional yake alikua ni Mwalimu wa Primary tu hadi anafariki ndio kazi alikua anaifanya kufundisha watoto kwa hio unafika muda humo humo class anapiga show ya bure anaingia bila chai kisha chaki inaletwa kutoka kusikojulikana, point ya kwanza walisema ni Mchawi point ya pili walisema vile vitu anavyoleta anaiba kwenye maduka yao yaan chuma ulete, kingine bro alikua hapendi kumfundisha mtu hizo mambo kabisa yaan hata ungemwambiaje akufundishe alikataa sababu yeye pekee ndio alikua anaijua hatari yake na hakuwahi kusema ni hatari kiasi gani kufanya vile