Mazingaombwe: Imeishia wapi ile michezo? Wewe unakumbuka nini enzi zako?

"Kash kash letee ....na tena letaeeee..."
Kumbe walikuwa wanamaanisha tumpe CASH, siye tunaitikia tuu!
 
...zamani mazingaombwe ulikuwa mchezo tu. Siku hizi wachezaji walewale wanawaibia watu kwa kutumia mchezo uleule kwa kujifanya waganga eti. Amakweli WAJINGA NDIO WALIWAO!!

Heeeh,Kumbe!!!!!
 
Habari za mchana wanajamvi?
Bila shaka shughuli zimekwenda vizuri katika muda huo wote tangu tumeanza pale asubuhi na mapema!

Jamani kuna wakati Miaka ya 1980 hadi mwisho wa miaka ya 1990 kulikuwa na watu waliotambulika kuwa wana mazingaombwe walikuwa wakija mashuleni wakati ule tupo shule za msingi.

Hawa jamaa alikuwa wakionesha mambo (michezo) mbalimbali ya kimazingaombwe; mfano kijiti kugeuzwa Penseli, kishikizo kugeuka Pelemende na kadhalika, swali linakuja hivi ni kwa namna gani yale mambo yalikuwa yakitokea je kuna uhusiano na ushirikina?

Wakati mwingine walikuwa wanajiita Pawa (Power) kwa maana ya mtu mwenye nguvu za ajabu waliweza kuzuia magari na pikipiki (sikuwahi kusikia kuhusu Treni)!


Na mbona imetoweka kabisa au ni kwa sababu ya kukuwa kwa sanyansi na Teknolojia ikihusisha kuwapo kwa michezo mingi ya kiteknolojia zaidi au kuna sababu nyingine ya kutowesha hiyo michezo?

Mkuu umekumbuka nini hadi ulaleta 'uzi' huu hapa?
Those old good days, akina profesa ....., wakija na masanduku yao makubwa ya mazingaombwe na vibuyu. Ole wako ukiingia ukumbini na limao/ndimu au umegeuza viatu - kushoto kwenda kulia! Ofuye!
 
Mkuu umekumbuka nini hadi ulaleta 'uzi' huu hapa?
Those old good days, akina profesa ....., wakija na masanduku yao makubwa ya mazingaombwe na vibuyu. Ole wako ukiingia ukumbini na limao/ndimu au umegeuza viatu - kushoto kwenda kulia! Ofuye!

He he he umenikumbusha mbali hayo mambo ya ndimu na kugeuza viatu
 
hahahaha,
Kua babu mmoja alikuwa anakuja shuleni kwetu
anajiita "POWER MABULA" duhh nilikuwa namuogopa
kipindi hicho darasa la pili. Naota mavitu ya ajabu kweli usiku..
 
hahahaha,
Kua babu mmoja alikuwa anakuja shuleni kwetu
anajiita "POWER MABULA" duhh nilikuwa namuogopa
kipindi hicho darasa la pili. Naota mavitu ya ajabu kweli usiku..

Ulishawahi kukutana na Profesa Eyesso!
Ukiingia kwenye mazingaombwe yake kwa njia za panya, lazima uwe kipofu!
 
hahahaha,
Kua babu mmoja alikuwa anakuja shuleni kwetu
anajiita "POWER MABULA" duhh nilikuwa namuogopa
kipindi hicho darasa la pili. Naota mavitu ya ajabu kweli usiku..

Sikilikiza mkwara: 'mimi ni power Mabula, kijana mdogo, lakini mambo yangu ni makubwa! Nitafanya wote hapa kuwa vipofu'. Kama umeingia ukumbini bila kutoa kiingilio, the soft center yako utadhani imechukuliwa ghafla kwenda Geza Ulole, Murutungulu au Chako ni chako.
 
duh,namkumbuka power mabula enzi hizo pale makurumla shule ya msingi(mwembechai)siku hizi kuna shule mbili sijui,yani mpaka ladha imepotea,..ndugumbi,nyerere primary school..crap..mnatuharibia historia
.

Karibu na kijiwe cha majungu enzi zile pale M/chai! Habari zote Nzito za DSM utazikuta pale. Jirani akiwepo Sheikh Yahya (RIP).
 
Halafu wengi walikuwa wanajinasibu kuwa ni watu kutoka Kongo, au Zaire enzi hizo. Utasikia...moto na motooo....mnaitikia...abongi saaaa! Ilikuwa burudani sana.
 
Ha ha ha haaah!! Kuna mmoja nimemuona juzi kituo cha daladala akifanya haya mambo ya mazingaombwe!
 
namkumbuka sana kababa yee. Jamaa alikuwa na unywele mmoja mrefu sana uliosokotwa. Anautumia kubebea vitu vizito hadi unashangaa.
 
Ulishawahi kukutana na Profesa Eyesso!
Ukiingia kwenye mazingaombwe yake kwa njia za panya, lazima uwe kipofu!

Kule mikoa ya Kusini ya Lindi na Mtwara kulikuwa na Mhindi anaitwa Jeki Magongo. Yeye alikuwa anamwaga pesa kama njugu!
 
jamaa walikuwa wakitutisha na nyoka wa plastiki.utoto kazi sana. nasikia power mabula kaokoka ni mchungaji sasa hivi. ila kitu kimoja nilichiobserve waliokuwa wafanaya hii michezo wakiacha akili zao zinakuwa si katika hali nzuri, wanakuwa kama wamewehu hivi
 
akinan profesa singila,wa zamani mwenzangu umenikumbusha mbali sana,walikuwa wanachimba mkwara usigeuze nguo au viatu jamaa atashindwa kufanya magic..
 
Back
Top Bottom