real G
JF-Expert Member
- Feb 7, 2013
- 5,227
- 5,287
Mkurugenzi wa Jamii Forums, Maxence Melo na Mkurugenzi wa taasisi ya utafiti ya Twaweza, Aidan Eyakuze walifanya mahojiano asubuhi ya leo Azam Tv, mjadala ulikuwa unahusu Kanuni za Maudhui ya Mtandaoni za Sheria ya EPOCA (Electronic and Postal Communication Act).
Maxence ameeleza kuwa Sheria ya EPOCA ilikuwepo tangu 2010 ila kanuni hizi zimekuja sasa tena kupitia Wizara ya Habari na maoni ya wadau yametakiwa ndani ya siku 7 tu.
Maxence anaendelea kusema Kanuni zenyewe zimeandikwa kwa Kiingereza na zinawalenga watanzania. Yawezekana nia ni njema lakini uharaka unatia shaka.
Maxence: Kwa Kanuni za Maudhui Mtandaoni za Sheria ya EPOCA (2010), Mamlaka zimetoa siku 7 wadau wawe wametoa maoni. Muda hautoshi!
Aidan Eyakuze: Kanuni zitapelekea watu kufanya censorship kwa kiwango kikubwa. Vijana watashindwa kufanya kazi kwa ubunifu kwa uoga
Maxence: Sheria, Kanuni au Sera zinazokuwa zinaua ubunifu(innovation) kwa namna yoyote hazifai katika ulimwengu wa sasa
Maxence: Mamlaka zifafanue “Maadili ya Mtanzania” ni yepi kabla ya kutunga sheria za kudhibiti wanaoenda kinyume na ‘maadili’ hayo
Maxence: Viongozi wetu wanapenda kusema “Hatuwezi kuwa na uhuru usio na mipaka” ila mipaka hiyo mara nyingi inawalenga wananchi tu
Aidan Eyakuze: Dola pia inatakiwa kuwekewa mipaka kisheria. Sio suala la kuweka mipaka kwa wananchi wakati Katiba imetoa uhuru huo
Maxence: Waandishi wana maadili ya uandishi; mtandaoni wananchi ndio waandishi. Tunakosea kuwachukulia raia kama waandishi wa habari
Aidan: Internet cafe zitatakiwa kuweka kamera kufuatilia kinachofanywa na wateja wao, hii ni kuingilia uhuru wa wananchi kupita kiasi
Maxence: Kuweka kamera si jambo jipya, hata hotelini zinakuwepo ila si vyumbani. Surveillance inayopendekezwa na kanuni haikubaliki
Maxence: Kanuni zinapendekeza maudhui kuchujwa kabla hayajaenda kwa umma; uchujaji huu nauona kama [HASHTAG]#censorship[/HASHTAG] isiyofaa karne hii
Aidan: Kwa mwenye ukurasa Facebook au Blog kupitia maoni yote itakuwa kazi kubwa. Mwandishi aliyekuwa anaibuka atakata tamaa ku-blog
Maxence Melo: Kanuni hizi pia zinataka wenye mitandao kukusanya taarifa za wateja wao. Si wote wana uwezo kiteknolojia kufanya hivyo
Maxence Melo: Kanuni zinataka ukiambiwa uondoe taarifa kwenye mtandao ufanye hivyo ndani ya saa 12. Ni muda mfupi na ni mtego unasao
Maxence Melo: Kimataifa, kuna utaratibu wa kuondoa taarifa mtandaoni. Mhimili wa Mahakama ndo ungethibitisha taarifa gani iondolewe. Ametolea mfano wa Chile walivyoamua kuhakikisha Mahakama ndiyo inasimamia haki katika hili. Amesema kwa namna ilivyokaa, watu binafsi na taasisi binafsi watautumia mwanya huu kuipoteza maana nzima ya Take Down Notice.
Maxence: Kuna vijana wana mawazo mazuri na wanatamani kuwa zaidi ya JamiiForums, Facebook, Instagram, WhatsApp, Twitter n.k; mazingira yanayoandaliwa yanaua ubunifu.
Maxence: Tulitakiwa kuhakikisha vitu vya kitanzania tunavitengenezea mazingira ya kukua na kuonekana kimataifa. Tuhamasishe ubunifu
Maxence Melo: Mataifa kadhaa niliyotembelea nimebaini huwa yanakazana kuhamasisha maudhui na ubunifu wa ndani. Huo ndio uzalendo. Tusione haya kuwataja wanaofanya vyema nchini. Kataja baadhi ya blogs.
Maxence Melo: Sijajua maana ya neno “Uzalendo” kwa wenye mamlaka ni ipi; nadhani ni vyema tukaelezwa kwao mtu mzalendo ni yupi.
Maxence: Kama wao ndio wazalendo, kwanini kanuni zinazotengenezwa kuhudumia waswahili ziandaliwe kwa Kiingereza na zipitishwe haraka?
Maxence: Tunahitaji Kanuni/Sheria ila tunatakiwa kuwa na ushiriki wa wadau ili Mamlaka zipate maoni tofauti. Tusijenge Taifa la Waoga
Maxence: Kanuni zinataka Blogs na Mitandao isajiliwe na TCRA. Ieleweke, mtu anaweza kukataliwa usajili pia! Hili pia linashangaza
Maxence: Wanaweza fanikiwa kudhibiti wabunifu wa ndani; wabunifu wa nje kama Facebook, Twitter hawawezi kudhibitiwa kirahisi hivyo
Maxence: Mwanasiasa awe Upinzani au Chama Tawala, asingependa akosolewe na mwananchi kirahisi. Kanuni zinatakiwa kuwalinda wananchi
Maxence: Katiba imetaja umuhimu wa faragha ya raia; Kanuni zinataka watumiaji wa mtandao taarifa zao nyeti zikusanywe na watoa huduma
Maxence Melo: Tukiwaogofya wabunifu hapa Tanzania, watakimbilia nchi nyingine na tunaweza kujikuta tunawapokea kama wawekezaji
Aidan: Mwaka 2015 wakati wanajaribu kupitisha Sheria 4 tuliambiwa tusiwe na wasiwasi; kwa sasa wameshawakamata wengi kwa sheria hizo.
Maxence Melo: Bahati mbaya, mtoa taarifa (whistleblower) ambaye Mamlaka zinamtambua ni yule aliyeenda kwao(mamlaka) na si vinginevyo!
Maxence ameeleza kuwa Sheria ya EPOCA ilikuwepo tangu 2010 ila kanuni hizi zimekuja sasa tena kupitia Wizara ya Habari na maoni ya wadau yametakiwa ndani ya siku 7 tu.
Maxence anaendelea kusema Kanuni zenyewe zimeandikwa kwa Kiingereza na zinawalenga watanzania. Yawezekana nia ni njema lakini uharaka unatia shaka.
Maxence: Kwa Kanuni za Maudhui Mtandaoni za Sheria ya EPOCA (2010), Mamlaka zimetoa siku 7 wadau wawe wametoa maoni. Muda hautoshi!
Aidan Eyakuze: Kanuni zitapelekea watu kufanya censorship kwa kiwango kikubwa. Vijana watashindwa kufanya kazi kwa ubunifu kwa uoga
Maxence: Sheria, Kanuni au Sera zinazokuwa zinaua ubunifu(innovation) kwa namna yoyote hazifai katika ulimwengu wa sasa
Maxence: Mamlaka zifafanue “Maadili ya Mtanzania” ni yepi kabla ya kutunga sheria za kudhibiti wanaoenda kinyume na ‘maadili’ hayo
Maxence: Viongozi wetu wanapenda kusema “Hatuwezi kuwa na uhuru usio na mipaka” ila mipaka hiyo mara nyingi inawalenga wananchi tu
Aidan Eyakuze: Dola pia inatakiwa kuwekewa mipaka kisheria. Sio suala la kuweka mipaka kwa wananchi wakati Katiba imetoa uhuru huo
Maxence: Waandishi wana maadili ya uandishi; mtandaoni wananchi ndio waandishi. Tunakosea kuwachukulia raia kama waandishi wa habari
Aidan: Internet cafe zitatakiwa kuweka kamera kufuatilia kinachofanywa na wateja wao, hii ni kuingilia uhuru wa wananchi kupita kiasi
Maxence: Kuweka kamera si jambo jipya, hata hotelini zinakuwepo ila si vyumbani. Surveillance inayopendekezwa na kanuni haikubaliki
Maxence: Kanuni zinapendekeza maudhui kuchujwa kabla hayajaenda kwa umma; uchujaji huu nauona kama [HASHTAG]#censorship[/HASHTAG] isiyofaa karne hii
Aidan: Kwa mwenye ukurasa Facebook au Blog kupitia maoni yote itakuwa kazi kubwa. Mwandishi aliyekuwa anaibuka atakata tamaa ku-blog
Maxence Melo: Kanuni hizi pia zinataka wenye mitandao kukusanya taarifa za wateja wao. Si wote wana uwezo kiteknolojia kufanya hivyo
Maxence Melo: Kanuni zinataka ukiambiwa uondoe taarifa kwenye mtandao ufanye hivyo ndani ya saa 12. Ni muda mfupi na ni mtego unasao
Maxence Melo: Kimataifa, kuna utaratibu wa kuondoa taarifa mtandaoni. Mhimili wa Mahakama ndo ungethibitisha taarifa gani iondolewe. Ametolea mfano wa Chile walivyoamua kuhakikisha Mahakama ndiyo inasimamia haki katika hili. Amesema kwa namna ilivyokaa, watu binafsi na taasisi binafsi watautumia mwanya huu kuipoteza maana nzima ya Take Down Notice.
Maxence: Kuna vijana wana mawazo mazuri na wanatamani kuwa zaidi ya JamiiForums, Facebook, Instagram, WhatsApp, Twitter n.k; mazingira yanayoandaliwa yanaua ubunifu.
Maxence: Tulitakiwa kuhakikisha vitu vya kitanzania tunavitengenezea mazingira ya kukua na kuonekana kimataifa. Tuhamasishe ubunifu
Maxence Melo: Mataifa kadhaa niliyotembelea nimebaini huwa yanakazana kuhamasisha maudhui na ubunifu wa ndani. Huo ndio uzalendo. Tusione haya kuwataja wanaofanya vyema nchini. Kataja baadhi ya blogs.
Maxence Melo: Sijajua maana ya neno “Uzalendo” kwa wenye mamlaka ni ipi; nadhani ni vyema tukaelezwa kwao mtu mzalendo ni yupi.
Maxence: Kama wao ndio wazalendo, kwanini kanuni zinazotengenezwa kuhudumia waswahili ziandaliwe kwa Kiingereza na zipitishwe haraka?
Maxence: Tunahitaji Kanuni/Sheria ila tunatakiwa kuwa na ushiriki wa wadau ili Mamlaka zipate maoni tofauti. Tusijenge Taifa la Waoga
Maxence: Kanuni zinataka Blogs na Mitandao isajiliwe na TCRA. Ieleweke, mtu anaweza kukataliwa usajili pia! Hili pia linashangaza
Maxence: Wanaweza fanikiwa kudhibiti wabunifu wa ndani; wabunifu wa nje kama Facebook, Twitter hawawezi kudhibitiwa kirahisi hivyo
Maxence: Mwanasiasa awe Upinzani au Chama Tawala, asingependa akosolewe na mwananchi kirahisi. Kanuni zinatakiwa kuwalinda wananchi
Maxence: Katiba imetaja umuhimu wa faragha ya raia; Kanuni zinataka watumiaji wa mtandao taarifa zao nyeti zikusanywe na watoa huduma
Maxence Melo: Tukiwaogofya wabunifu hapa Tanzania, watakimbilia nchi nyingine na tunaweza kujikuta tunawapokea kama wawekezaji
Aidan: Mwaka 2015 wakati wanajaribu kupitisha Sheria 4 tuliambiwa tusiwe na wasiwasi; kwa sasa wameshawakamata wengi kwa sheria hizo.
Maxence Melo: Bahati mbaya, mtoa taarifa (whistleblower) ambaye Mamlaka zinamtambua ni yule aliyeenda kwao(mamlaka) na si vinginevyo!