Maxence Melo atinga ofisi za IMF Washington DC

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
137,673
Reaction score
272,509



Taarifa zinaonyesha kwamba amekutana na Mkurugenzi wa IMF Kristalina Giorgieva , ambapo mazungumzo yao yalijikita katika kuwasaidia vijana wa Kitanzania ili kuangalia uwezekano wa kuboresha mazingira ya kufanya biashara .

Kwa niaba ya Wafanyabiashara vijana wa kimataifa naipongeza sana hatua hii ya Melo kutumia fursa hii adimu kutuombea msaada sisi vijana wa Kitanzania .

Mungu ibariki JF
 
Aiseee; amefikaje huko? Ni JF au kuna chombo kingine?

Heko na Hongera nyingi. Natumaini ombi litafanikiwa.

Lakini ngoja nikutupie dongo laini.
Hiyo picha ya kwanza umejinyenyekesha sana mkuu! Au ni kabla ya kuwasilisha mahitaji kwa mkubwa?
 
Sasa badala ya kukutana na JPM anakwenda kumwambia Director wa IMF?Max ulitakiwa ukamwambie Magufuli bwana,au unamwogopa ? Huyu Kristina hatosaidia lolote. Mwenye rungu la kuboresha mazingira ya wafanya biashara hapa Tanzania ni JPM.
 
Sasa badala ya kukutana na JPM anakwenda kumwambia Director wa IMF?Max ulitakiwa ukamwambie Magufuli bwana,au unamwogopa ? Huyu Kristina hatosaidia lolote. Mwenye rungu la kuboresha mazingira ya wafanya biashara hapa Tanzania ni JPM.
JPM haingiliki best
Congrats Maxence Melo utafika mbali Mkuu kaza mwendo
 
Aiseee; amefikaje huko? Ni JF au kuna chombo kingine

Heko na Hongera nyingi. Natumaini ombi litafanikiwa.

Lakini ngoja nikutupie dongo laini.
Hiyo picha ya kwanza umejinyenyekesha sana mkuu! Au ni kabla ya kuwasilisha mahitaji kwa mkubwa?


Hapana..nadhan ni pose la heshima tu..ulitaka aweke midole km wasanii wa hiphop na limkono limoja kati ya zip ya salawili?
 
Sasa badala ya kukutana na JPM anakwenda kumwambia Director wa IMF?Max ulitakiwa ukamwambie Magufuli bwana,au unamwogopa ? Huyu Kristina hatosaidia lolote. Mwenye rungu la kuboresha mazingira ya wafanya biashara hapa Tanzania ni JPM.
Labda yeye kaenda kuweka mambo sawa au kuongeza nguvu jikoni kwani hata JPM uwafuata hao IMF.
 
Hongera sana Max,tunajua wewe ni mpambanaji kwa niaba ya wengine
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…