Mawazo yenu pls

Chinga boy

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
412
101
Heshima kwenu wanajamvi,nipo ktk harakati za kujiari na kuachana na ajira na lengo langu ni kununua coaster kwa ajili ya daladala na kwa kuwa sina capital ya kutosha lengo langu niombe mkopo benk kutumia nyumba yangu.so wadau mnanishauri vipi kwa hili.natangulisha shukrani zangu
 
Nakushauri fanya utafiti wa kutosha kuhusu hio biashara ya Daladala kabla hujapoteza nyumba,
 
Aisee kama utaiendesha na kuitunza we mwenyewe chukua lakini kama utanunua ya kumpa dereva acha kabisa utapoteza nyumba yako bro..
 
Hongera ndugu kwa kuwa na mtaji wa kutosha.
Ni hivi; Jaribu kuwekeza kwenye vitu visivyohamishika (Immobile properties)

Kawaida ukitaka kununua gari, kama una mtaji wa magar mawili unashauriwa kununua gari 1; ukiwa na wa magar manne unatakiwa kununua magari mawili n.k. kwani hii ni biashara isiyo nauhakika muda wote, ko inahtaji mtaji mkubwa.
Fikiria umenunua gari baada ya wik 1 likapata ajal na likaharibika itakuwaje?
kwa kuanzia biashara ya magari sio nzuri jaribu bussiness nyingine.
 
Kwanza nakupa hongera kwa kuamua kujiajiri mwenyewe mkuu please nakuomba hilo la kuomba mkopo uliangalie kwa jicho lako mara mbili maana najua mkopo una manufaa zaidi na ni njia mojawapo ya kumsaidia mfanyabiashara kwa kumuongezea mtaji kabla hujafanya maamuzi yako ya kuitoa nyumba yako kwa kupata mkopo ingatia haya.

1. umeamua kuomba mkopo ka ajili ya kununua coaster je unakipato kingine cha kuendesha familia kuhusu matumizi madogo madogo ya kila siku hapo nyumbani?

Hili kosa hufanyika na watu wengi sana maana ukiamua kuomba mkopo wa hela jaribu kuitumia kwa makusudio ya huo mkopo maana vijana wengi huwa wakiomba mkopo mara utasikia katoa hela kidogo hapo kalipia sijui ada, kanunua mchele, na vitu vidogo vidogo asikuambie mtu ukitumia hata sh 2000 hapo umepunguza makusudio ya mkopo huo so ni vizuri ujitathimini kwanza uhakikishe kuhusu matumizi madogo madogo unayo angalau ya kukutosheleza ndani ya miezi nane au zaidi bila kugusa hata senti moja ya hiyo biashara yako. maana utakapoanza biashara yako ujue kuna return ambayo utakuwa unarudisha kil mwezi na inategemea utaomba kwa muda gani, hili ni muhimu sana

2. Pili uko tayari kuwa bandigu? hili lina maana sana unaweza kufikiri nakufundisha tabia mbaya ila ukweli kabisa tupo katika jamii ya kitanzania na tumelelewa hivyo nasema hivyo kwa sababu tunapoona mtu amenunua coaster au anakitu flani cha gharama tayari masikio yetu na fikra zetu tunafikiri ameshatajirika na wala hatujuia katoa wapi hiyo hela so unachotakiwa ndugu yangu funika masikio na macho ya watu maana watu watakuja kulilia matatizo ya shida zao usifikiri watakuja kukuomba mahela mengi hapana watakuja hata sh 1000, mara 5000 mwisho michango mara jirani anaumwa sisemi usiwe eti mkimya kabisa naomba uangalie pale kwenye ulazimu tu na uwe serious maana siku ukianguka hakuna atakayekusaidia zaidi ya kukucheka wakishangilia nyumba yako inapigwa mnada.

3. tatu je hiyo biashara ya daladala nani anakuwa dreva ni wewe au unaajiri mtu? mapendekezo nafikiri hujafikia hatua ya majukumu mengine mengi maana umesema ndio unataka kuanza hiyo biashara ninapendekeza wewe mwenye uwe driver maana wakati wa mwanzo ni muhimu sana ili kupata uzoefu angalau mwaka mzima ili ukija kumuajiri mtu hawezi kukudanganya maana utakuwa umepata uzoefu wa kutosha.

4. mwisho kabisa je mkopo huo na hiyo biashara inalingala na kiasi ambacho utakuwa unarudisha kwa mwezi hili ni muhimu sana ili usije ukawa unapigiwa na credit officer unazikimbia simu jaribu kufanya uchunguzi wako kwanza
nakutakia biashara njema na mafanikio katika hilo.

Asante
 
Kama unatamani kulala kwenye gari basi fanya unachotaka kufanya
 
Hiyo Coaster unayotaka kununua ni mpya au used??.. Nina experience ya hiyo biashara. Nilinunua daladala used, kidogo nipate presha.. Jamani ni Biashara ngumu sana..Ilibidi niliuze baada ya miezi sita tena kwa bei ya hasara.. Ushauri wangu ni kwamba uwe makini na hiyo biashara na inahitaji supervision kubwa sana..Kila la heri.
 
ndugu yangu hiyo biashara inategemea sana na upepo. Mimi ndugu yangu aliwahi poteza nyumba hivi hivi kisa alichukua mkopo akanunua gari ya abiria kwa ajili ya kufanyia biashara yaliyo mkuta hatakuja kusahau.
Sikutishi lakini biashara ya magari inahitaji uzoefu na uangalizi wa hali ya juu yani unaweza pata hasara kwa mara moja ukapoteza kila kitu.
 
mkuu usiache kazi yako,biashara ya daladala ni wachache sana wanaimudu,wengi ni presha tu...tusije kukupoteza bure hapa jamvini...
 
Back
Top Bottom