theprogrammer C++
Senior Member
- May 17, 2013
- 139
- 334
Hii ni stori nimeiskia ikizungumzwa kinyemela kwenye vijiwe vyetu vya kahawa Kariakoo. Sijui kama ni kweli au ni soga tu za wazee. ila nimeona niilete hapa tujadili.
Habari nzuri na uwajibikaji, uchapakazi mzuri wa DCEA unaonekana mtaani na faida zake. Tani za dawa zinakamatwa, mamia ya watuhumiwa wanafikishwa mahakamani, kesi nzito zinaendelea na conviction rate ya taasisi yetu ni nzuri sana.
Kuna wanaodai kila operesheni kubwa inayofanikiwa inaongeza imani ya wananchi kwa viongozi wa vyombo vya usalama kuliko hata baadhi ya wanasiasa wanaotafuta kura..... Kuna wanaonong'ona kwamba kama hali hii itaendelea mpaka 2030, huenda akatokea mtu ambaye hatahitaji kuzunguka na ilani ndefu ya CCM. Watu watakuwa wanamtambua kwa rekodi ya operesheni, kukamata wahalifu na kusimamia sheria.
Sisemi ndiyo itatokea. Sina uthibitisho. Ila siasa za Tanzania zina tabia ya kutushangaza.
Nauliza tu, je, inawezekana uchaguzi wa 2030 ukaandikwa mapema kupitia mafanikio ya vita dhidi ya dawa za kulevya???
Habari nzuri na uwajibikaji, uchapakazi mzuri wa DCEA unaonekana mtaani na faida zake. Tani za dawa zinakamatwa, mamia ya watuhumiwa wanafikishwa mahakamani, kesi nzito zinaendelea na conviction rate ya taasisi yetu ni nzuri sana.
Kuna wanaodai kila operesheni kubwa inayofanikiwa inaongeza imani ya wananchi kwa viongozi wa vyombo vya usalama kuliko hata baadhi ya wanasiasa wanaotafuta kura..... Kuna wanaonong'ona kwamba kama hali hii itaendelea mpaka 2030, huenda akatokea mtu ambaye hatahitaji kuzunguka na ilani ndefu ya CCM. Watu watakuwa wanamtambua kwa rekodi ya operesheni, kukamata wahalifu na kusimamia sheria.
Sisemi ndiyo itatokea. Sina uthibitisho. Ila siasa za Tanzania zina tabia ya kutushangaza.
Nauliza tu, je, inawezekana uchaguzi wa 2030 ukaandikwa mapema kupitia mafanikio ya vita dhidi ya dawa za kulevya???