Mawazo yangu juu ya wanaume

Mawazo yangu juu ya wanaume

Binafsi yangu

Hapo haujamzungumzia mwanaume ila umemzungumzia binaadamu kiujumla yaani mwanamke na mwanaume

Binaadamu haswa wanatakiwa wawe hivyo kwa maelezo yako sio mwanaume pekee wala mwanamke pekee
 
Uanaume si koti unalolivaa ukubwani; ni mbegu iliyooteshwa ndani ya vinasaba (DNA) .
Sifa kuu za kiume—Uongozi, Uthubutu, na Ulinzi—ni silika za kibaolojia ambazo mwanaume huzaliwa nazo. Hata katika utoto, mtoto wa kiume hujipambanua kama kiongozi wa kundi bila kuhitaji muongozo; huu ni ushahidi kuwa uwezo wa kutawala ni zawadi ya Muumba, si zao la semina za nabii au vikao vya wanaume.

Kuitana kwenye vikao ili "kufundishwa uanaume" ni kudhalilisha hadhi na uwezo wa asili wa mwanaume. Mwanaume wa kweli huongozwa na dhamira na sauti yake ya ndani (Inner Compass). Kutegemea maoni ya watu wengine au "Manabii" wa mitandao ili kufanya maamuzi ya ndani ya nyumba yako, ni kukataa mamlaka uliyopewa kiumbaji.
Mwanaume hafundishwi kuwa mwanaume; yeye hujitambua na kusimama kwenye nafasi yake.

Ally si Juma
Kila mwanaume ana namna yake ya kipekee ya kutekeleza majukumu yake kama Mtoaji (Provider), Kiongozi (Leader), na Mlinzi (Protector). Mifumo ya kigeni inayolazimisha wanaume kuishi kwa namna fulani ili "waridhike" ni batili.

Mapenzi hayapaswi kuwa biashara ya kubadilishana na zawadi kama simu za gharama (iPhone).
Mwanaume haongozwi na tamaa ya mwili (utamu), kwani anajua thamani yake ni kubwa kuliko anasa za muda mfupi. Kwake, mke ni mwenzi wa maisha (Life Partner) anayeongozwa kwa hekima binafsi ya mume, si kwa miongozo ya vikao vya wanaume

Tufundishane: Biashara, uwekezaji, kilimo, uzalendo, na teknolojia (Hizi ni stadi za maisha).

Tusiingiliane: Kwenye misingi ya uanaume. Ujasiri, msimamo, na namna ya kuishi na mke ni mambo ya asili ambayo mwanaume anapaswa kuyaishi kwa kadiri ya akili na utashi wake aliopewa na Mungu.

Kwa kifupi: Mwanaume ni kiumbe kilichoundwa na uwezo wa asili wa kutawala, kulinda, na kutoa mwelekeo. Akirudi kwenye asili yake (The Instinct), hahitaji darasa la kumfundisha jinsi ya kuwa yeye.
Gender based nonsense.
 
Unahisi father figure influence ndio inasababisha mtoto wa kiume asipoteze male identity?

inaweza ikawepo na mtoto akapoteza pia.
Uanaume hautengenezwi wala hautafutwi.
male boundaries na masculinity mtu anaweza zaliwa nazo tu kwa 100% bila kujifunza, au ni zile instincts tu za kiume?
 
Ni vyote tyuuh, unless useme father figure influence inataka kustay kwenye nini.

Ila uanaume hautengenezwi wala hautafutwi.
Male boundaries, Biological masculinity traits,Social masculinity / male identity , sio kwamba kuna namna tunachanganya mafaili🤔
 
si kwa miongozo ya vikao vya wanaume
Inasikitisha sana, Millenials (age 30+) ndio walijazana pale

Wakapewa na dress code kabisa black suit, shati jeupe, tai nyekundu na kiingilio 50k

Nabii anawafundisha "nilimnunulia mke wangu iPhone 17 siku hiyo hiyo akanipa unyumba."

Kweli mwanaume wa miaka 30+ unalipia 50k kufundishwa kuomba uchi wa mke wako! WTF!!

Gen Z wataendelea kuwadharau sana mabroo wao
 
Male boundaries, Biological masculinity traits,Social masculinity / male identity , sio kwamba kuna namna tunachanganya mafaili🤔
Labda nikupe uhuru wee, unataka tujadili nini, ili tusipteze focus.

Maana mie binafsi naona hivyo vyote unavyotaja, havihitaji father figure influence ili viwepo.
Ni vinajitosheleza vyenyewee.
 
Labda nikupe uhuru wee, unataka tujadili nini, ili tusipteze focus.

Maana mie binafsi naona hivyo vyote unavyotaja, havihitaji father figure influence ili viwepo.
Ni vinajitosheleza vyenyewee.
Kusema kuzaliwa navyo kwa 100% sio kweli mengine anahitaji father figure influence au jamii ya watu wakiume walio mzunguka ila kupata social masculinity na male boundaries 🤔
 
Back
Top Bottom