Mawaziri waghushi vyeti

Nimeambiwa hatimaye Kamala kafanikiwa kupata Ph.D inayotambulika kutoka Hull university.

Sina uhakika sana ila inaelekea baada ya scandal kuanza akajiandikisha kimya kimya na ameonekana akitembelea hicho hicho mara nyingi.

Wenye taarifa zaidi mnaweza kutujulisha. Kule bungeni bado hajaweka hiyo taarifa. Labda anasubiri watu wamshambulie ndio atoe ushahidi wake, au anasubiri 2010 wapinzani wake wakija na tuhuma ndio ataoe ushahidi wake.

Itaidi Kamala atuombe radhi kwanza kwa kutuletea Ph.D feki (aliyosomea kwa miezi mitatu) ambayo ilikuwa msingi wa uteuzi wake mbalimbali. Huo ni udanganyifu ambao unaadhibika chini ya sheria za nchi.
 
Fataki hapo umenena! Kamala lazima aombe msamaha PhD yake fake ndo ime-influance teuzi zake zote kuanzia Ubunge mpaka unaibu waziri! aaargh! inaudhi sana...nway cku yao inakaribia...watalia na kusaga meno!!
 
Ministers in fake degrees saga

DAILY NEWS Reporter, 22nd February 2009 @ 10:49

Eight Senior Cabinet Members and Members of Parliament are among recipients of questionable academic qualifications, particularly Doctorate Degrees (PhDs), from overseas Learning Institutions that are not internationally recognized. Some of the academic credentials are understood to have been obtained through correspondence between 1997 and 2005.

Well informed sources in the academia have told the ‘Daily News' that the institutions which issued the doubtful qualifications include Washington International University based in Hawaii, Commonwealth Open University based in Caicos Virgin Island, Free States University, Ambala University in India and Almeda University, USA. The report comes amid revelations that some academicians, including at least one from Kenya, secured teaching jobs at higher learning institutions in the country using forged PhDs.

The Tanzania Commission of Universities (TCU) recently cautioned Tanzanians to be on maximum alert against the influx of bogus degrees. According to TCU Executive Secretary, Professor Mayunga Nkunya, many Tanzanians are easily trapped by agents of degree mills that are selling them at a negotiable prices starting from 2,000 US dollars (2.6m/-).

"There are so many fake Universities that are increasingly advertising online courses that don't require one to attend classes but their physical addresses can not be traced anywhere. We advise those aspiring to pursue higher studies overseas to contact us first for guidance," said Professor Nkunya.

The applicants should also contact embassies of the countries they intend to study in for guidance. One of the ministers is said have acquired a Masters in Business Administration (MBA) and a PhD. concurrently between 2001 and 2003. Another one undertook a Post Graduate Diploma course in 2000-2001 and a PhD course from 2001 to 2003.

According to our sources, there are more than 600 bogus Universities around the world enrolling students using fake addresses and mostly transact online. Dr Mussa Assad from the University of Dar es Salaam, who has been researching on fake Universities around the World, says getting a PhD involves hard work and that bona fide holders of such qualification is distinguished by their knowledge . "To earn a Ph.D., one must accomplish two things.

First is to master a specific subject completely. Second, one must extend the body of knowledge about that subject," he explained. Prof Nkunya said that the ministers and MPs or their employers can bring the credentials to the Commission for verification. "We have no legal powers to make any follow up on the credentials for the time being, until the present Universities Act is amended, hopefully," he said.
 
Ministers in fake degrees saga

One of the ministers is said have acquired a Masters in Business Administration (MBA) and a PhD. concurrently between 2001 and 2003. Another one undertook a Post Graduate Diploma course in 2000-2001 and a PhD course from 2001 to 2003.


Haya ni mazingaombwe, haiwezekani ukasoma PhD kwa style hiyo...!! Hawa wameupotosha umma juu ya elimu zao hawafai kuwa viongozi.
 
Kazi ipo. Na hivi sasa LOWASSA aliyekuwa akiwakingia kifua kwa MASLAHI YA CHAMA hayuko madarakani. Sioni uwezekano wa PINDA kulinda huu uozo.

Wakimaliza hapa waingie katika ngazi za ukurugenzi na menejimenti za taasisi za umma. Huko kumejaa vyeti bandia. Wapo waliotumia matokeo ya wengine kujiunga na vyuo kadha. Wapo walionunua vyeti baraza la mitihani na wapo walionunua vya mitaani.....na ni wengi mno...

omarilyas
 
Haya ndiyo mapungufu ya mfumo wetu wa elimu na utawala. Kuwa na cheti cha shahada katika fani fulani haina maana ni kuwa mtendaji mzuri katika fani husika. Maana mtu anaweza kupata cheti kwa njia nyingi sizizo za kihalali. Lakini pia cheti hakitoi fursa ya kujua mwenendo na tabia ya muhusika, ambayo ni muhimu sana katika umahiri na uamininfu wautendaji wa kazi.

Nadhani wakati umefika wa kubadili kabisa ya fikira zetu kuhusiana na elimu. Elimu isiwe wingi wa shahada, bali uwezo wa muhusika katika kutenda kazi.
 
Tufike wakati tujiulize GPA ya Mkulu ikoje?. Kwa nini hakufanya Masters. Majibu ya maswali hayo yatathibitisha kwamba shule nene sio issue, issue ni kuwa mpiga domo mzuri wa kuinadi ilani ya uchaguzi kwa wananchi na CCM itaendelea kutawala

GPA haiko mbali. Nenda Dept pale mimani archive utaipata. MAKARAI MPAKA UTACHOKA NAONA JAMAA WALIKUWA WANANYAKA KILA MWAKA!!
 
Sidhani kama watu kama hao wanastahili heshima ya kufichiwa siri.Kama wao hawakuwaheshimu watanzania na kuwapa utaalamu feki na sub-standard, kwa nini wao waheshimiwe?Huku si kuenzi maovu.Ninachelea kusema kwamba utamaduni huu wa kuchukuliana na waovu ndio uliotufikisha hapa tulipo.Lazima kila mtu ajue kwamba akifanya uovu ataumbuliwa,hii ni hatua muhimu katika kuwafanya watu waogope kutenda uovu.Vinginevyo hatufiki popote.

Mawaziri waghushi vyeti

• Wahaha kulinda siri isivuje

na Mwandishi Wetu
Tanzania Daima~Sauti ya Watu

KASHFA ya kughushi vyeti vya taaluma mbalimbali imeendelea kulitafuna taifa, baada ya kubainika uwepo wa mawaziri wanne wanaodaiwa kughushi vyeti vya elimu ya juu.

Kugundulika kwa mawaziri hao kunatokana na kuwapo kwa taarifa kuwa baadhi ya wasomi nchini wamepata taaluma hizo kupitia kwenye vyuo visivyotambulika kimataifa, hivyo elimu yao kutokuwa halali.

Aidha, kuna kundi linalodaiwa kughushi vyeti vya vyuo mbalimbali vya nje ambavyo havina umaarufu au sifa zinazotambulika kimataifa.

Miongoni mwa wasomi ambao wamo katika kundi la mawaziri ni wahadhiri wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, ambao wamepata shahada za falsafa (PhD) lakini zimebainika kupatikana kupitia katika tovuti mbalimbali za vyuo hivyo visivyo na sifa.

Kutokana na wahadhiri wao kutopata elimu hiyo kwenye vyuo vinavyotambulika, uongozi wa chuo hicho pamoja na Kamisheni ya Vyuo Vikuu vya Elimu ya Juu (TCU) imewataka wale wote waliopata elimu katika vyuo hivyo kusomea upya shahada zao katika vyuo vinavyotambulika kimataifa.

Habari ambazo zimeifikia Tanzania Daima Jumapili, zinadai kuwa mawaziri hao wanne (majina tumeyahifadhi), ambao ni madaktari wa fani mbalimbali hadi sasa hawajaweza kusomea upya shahada zao kama walivyoshauriwa na vyombo vya kitaaluma.

Hadi sasa mawaziri hao wamekuwa wakihaha kuhakikisha kuwa utata wa elimu yao hauwekwi hadharani ili kulinda heshima yao waliyojijengea ndani na nje ya nchi.

“Kuna mawaziri wanne ambao taaluma zao zina utata, hasa kutokana na wengine kughushi na wengine kusoma katika vyuo visivyotambulika kimataifa, uchunguzi wa walikozipata taaluma zao unaendelea,” kilidokeza chanzo chetu cha habari.


Mmoja wa mawaziri hao siku za hivi karibuni amekuwa akionekana zaidi katika vyombo vya habari, kwa msimamo wake wa kuitetea nchi ili isiingie katika mikataba na makubaliano na nchi nyingine bila kufanya tathmini ya kina.

Waziri mwingine anayedaiwa kuwemo kwenye mkumbo huo aliwahi kuingia katika malumbano na vyombo vya habari kutokana na kumuandika kuwa anatetea ufisadi, pamoja na kuwemo kwenye kundi la wanamtandao.

Kutokana na sakata hilo, mawaziri hao huenda wakalazimishwa kuachia nyadhifa walizonazo ndani na nje ya chama au kufukuzwa, iwapo suala lao litavaliwa njuga na viongozi wao au wananchi.

Kashfa hiyo ya mawaziri kughushi vyeti imekuja huku Baraza la Mitihani la Taifa NECTA likiandamwa kwa shutuma za uvujaji wa mitihani pamoja na uuzaji wa vyeti vya elimu ya sekondari.

Matukio ya kughushi vyeti yamekuwa yakiongezeka kila kukicha hapa nchini, jambo linalohatarisha mustakabali wa taifa katika nyanja ya elimu, hasa katika zama hizi za utandawazi, ambapo nchi kadhaa zimekuwa zikielekeza nguvu zaidi katika sekta ya elimu ili ziweze kuwa na wataalamu watakaozisaidia kuandaa mipango ya maendeleo.

Mmoja wa wabunge aliyewahi kukumbwa na kashfa ya kughushi vyeti vya elimu ya juu ni Ali Ramadhani Kihiyo, wa Jimbo la Temeke (CCM), ambaye alifunguliwa kesi na Chama cha NCCR-Mageuzi iliyosimamiwa na mwanasheria wake maarufu wakati huo, Masumbuko Lamwai.

Mbunge huyo alilazimika kuachia wadhifa huo baada ya kubainika kuwa hakuwa na elimu hiyo kama vyeti vyake vilivyokuwa vikionyesha na hatimaye kuachia ngazi na kuitishwa uchaguzi mwingine.


Mbali ya Kihiyo, Mbunge wa Buchosa, Samwel Chitalilo (CCM), amekumbwa na tuhuma za kughushi vyeti, lakini hadi sasa anaendelea na ubunge, licha ya kuwapo kwa kelele za baadhi ya watu wakimtaka aachie ngazi kutokana na kashfa hiyo.
 
Ninavyofahamu Dr. Mathayo hana Degree kutoka huko PWU bali Orange Free State RSA. Sasa kama kweli ni feki basi atakuwa amefoji cheti maana OFS ni one of the best universities in RSA hivyo hakuna cha kununua cheti pale.

Huyo bwana matayo hivyo vyeti wala hakuvisubmitt botswana, ni vigumu sana kwa botswana kusubmitt vyeti fake, kuna wakenya wengi sana wameshakamatwa na vyeti fake, mimi nina wasiwasi sana na huyo bwana kwa maana hata majina anayotumia si aliyokuwa anatumia botswana botswana alikuwa akijulikana kama DAVID MATHAYO MSUYA, LAKINI NASHANGAA HAPA TANZANIA JINA LA MSUYA ALIPO
NA KWA KIFUPI HAKUWA ANAFUNDISHA UNIVERSITY, ALIKUWA KWENYE COLLAGE KAMA ZA VETA AMBAZO KWA BOTSWANA ZINAITWA BRIGADE
 
Hakika kwa hali kama hii J.K ANATAKIWA kuact upon.Kinyume na hilo watu hawatakaa wakamuelewa.Tutaongea na kuongea na kuongea mpaka sauti zetu zisikike.Tumesoma kwa shida sana vibachelor vyetu.Na wadogo zetu wanasoma kw shida kubwa mno sasa hivi,Wakati huo huo kuna watu waliotemper na shulw wameshhika mpini.Inawezekaana mazingira magumu ya elimu tanzania yanatengenezwa na watu kama hawa.

SAUTI YA WENGI NI SAUTI YA MUNGU!
 
One of the ministers is said have acquired a Masters in Business Administration (MBA) and a PhD. concurrently between 2001 and 2003. Another one undertook a Post Graduate Diploma course in 2000-2001 and a PhD course from 2001 to 2003.[/B][/color]

Hawa jamaa VIPANGA mno, yani unafanya Masters na PhD pamoja. Sasa sijui maeneo yao ya tafiti kwa Masters na PhD ni tofauti. Nilishangaa kusikia Nchimbi akitangazwa ni Dr. Nikajiuliza kasomea wapi wakati alikuwa Mzumbe, kumbe wanatupiga changa la macho.
 
Fukuza hawa watu na sisi tutaona kweli tuna Rais.
. Mkuu alishasema hakuna shule ya Uwaziri na kuwa mbunge yeyote aweza kuwa waziri au n/waziri. Kwa maana hiyo hakuwachagua hayo kwa kuzingatia professional wala academic title zao. Hivyo suala la kumwambia awafukuze itakuwa ni kelele za chura.............. .Nionavyo mimi ni suala la tasisi husika kuchukua mkondo wake kwa kuwapokonya hizo Dr zao.
 
Request for CVs
Competent and qualified Tananians are invited to submit their CVs for consideration in the appointment to serve as the Ministers, Deputy Ministers and Permanent Secretaries of the United Republic of Tanzania: The applicant should fullfill the following general criteria for him/her be considered for short listing prior to the interview scheduled to be held on November, 2010:

1. Graduate from recognised deomestic or International universities with minimum of upper second class with cut off points 3.7 for Undergraduate, for a masters degree holder, he/she must have a minimum score of B+ in his/her Thesis. PhD qualification from recognised University will be an added advantage. For the PhD holders, copy of the degree must be certified by the Univeristy he/she graduated.

2.Five years experience in the field of study

3. Thorough knoweldege of the country political and socio-economic behaviours

4. He/she must declare any business interest he/she may have and must be ready for intelligency watch for scrutiny

5. He must declare a dully signed legal papers for all his/her spouse, family members liquidy and fixed assets and must be ready for intelligency watch for scrutiny

6. He must submit a concise of up to 5 pages explain to why she/he thinks that he is the best in serving Tanzanians

7.Wadau nakaribisha general qualifications hapa

Note that :
(i) these positions are open to all Tanzanians who believe that have the passion to work for Tanzanians. If you feel that you have that passion and you meet the above qualifications, please submit your CV with 3 referees one from the Academic Institution in which you obtained your current degree.

(ii) If the applicant is successfully selected, the placing of the Ministries will base on the compartibility of degree with respect to the Ministry to be served.

Covering letter specifying among others the Ministry you prefer to serve must reach the PCCB by 28th April 2009 so as to give enough time for intelligency watch processes prior to the interview date to be scheduled later.
 
Last edited:
=Maane;381638]Request for CVs
Competent and qualified Tanzanians are invited to submit their CVs for consideration in the appointment to serve as the Ministers, Deputy Ministers and Permanent Secretaries of the United Republic of Tanzania:

Where Should I submit my CV?
 
Judging from previous and numeral forums discusions I have come to realize ai't shit gonna happen!

Tutaongea weee but where????
 
Judging from previous and numeral forums discusions I have come to realize ai't shit gonna happen!

Tutaongea weee but where????
 


According to
Tanzania Commission of Universities Executive Secretary, Professor Mayunga Nkunya, many Tanzanians are easily trapped by agents of degree mills that are selling them at a negotiable prices starting from 2,000 US dollars (2.6m/-).

"There are so many fake Universities that are increasingly advertising online courses that don't require one to attend classes but their physical addresses can not be traced anywhere. We advise those aspiring to pursue higher studies overseas to contact us first for guidance," said Professor Nkunya.

The applicants should also contact embassies of the countries they intend to study in for guidance.
Kama huyu Professor Nkunya ndio mhusika wa kutatua hili tatizo basi tumekwisha! Mzee haelewi tatizo.

Anasema Watanzania wanakuwa "trapped" na wauza shahada. Yani anamaanisha hawa walimu wa Mzumbe na mawaziri wenye u-professor Maji Marefu walikuwa hawajui kwamba nia yako ni kupata hivyo vyeti feki! Nkunya anaogopa kusema ukweli, au ni kilaza mwingine huyu?

Halafu, kukuonyesha zaidi kwamba Professor Nkyunya hajui kinachoendelea au si msema kweli, anatamka "wale wanaotaka kusoma nje ya nchi wawasiliane na sisi kwanza kwa ushauri..."

Mtu ambae anataka kupata shahada ya uongo uongo mtandaoni utategemeaje aje kwako kwa ushauri, au sijui ajipekele ubalozini, kwani ye mjinga akanyakwe? Yani Prof. Nkunya haelewi kwamba haya matatizo ni usanii wa kunuia, intentional chicaneries. Huyu Professor Nkunya ndio yuko in charge wa hili tatizo?

Alitakiwa aseme wazi wazi kwamba ukijipenyeza kwenye kazi ya mtu kwa vyeti feki feki hiyo inaweza kuwa ni fraud! Hakuna kubembelezana eti wamekuwa "trapped"! Bongo tumebarikiwa viongozi jamani jamani!
 
Last edited:
Back
Top Bottom