Mchambuzi
JF-Expert Member
- Aug 24, 2007
- 4,850
- 9,405
Ni jambo lisilohitaji mjadala kwamba serikali ya awamu ya nne, hasa katika kipindi cha minne imefeli katika maeneo yote yanayohusiana usimamizi wa rasilimali za nchi kwa manufaa ya walio wengi na utawala bora kwa jumla. Tumefikia hali ambapo Serikali ya CCM haistahili tena kuendelea kushikilia dhamana na kutawala nchi. Kwa mfano, kwa muda sasa, tumekuwa na baraza la mawaziri lililokosa ‘Stability', na kupelekea utawala mzima wa nchi kuanzia ngazi ya serikali kuu hadi serikali za mitaa kuzidi kukosa mwelekeo. Tunazidi kushuhudia jinsi gani mamlaka ya nchi inavyoanza kuhama taratibu kutoka kwa viongozi wa kisiasa tuliowapa dhamana (mawaziri na wabunge) na kwenda kwa viongozi wasiotokana na ridhaa yetu ya moja kwa moja (bureaucrats – makatibu wakuu n.k). Matokeo yake ni viongozi tuliowachagua kusimamia rasilimali za nchi yetu kushindwa kufanya maamuzi wanayostahili - kisera.
Nia ya makala hii ni kujaribu kuja na mada ya kutusaidia kuachana japo kwa mara moja, na mtazamo/uchambuzi tuliouzoea wa kutoangalia mambo nje ya boksi juu ya suala la instability ya serikali ya awamu ya nne, na badala yake kuangalia suala hili kwa mapana na marefu zaidi. Ni imani yangu kwamba zoezi linaweza kutusaidia kubadilisha mawazo zaidi na kuzidi kutuandaa na mchakato wa kupata Katiba Mpya. Kama anavyohimiza Mh. Zitto, iwapo tunahitaji neno moja tu ndani ya katiba yetu mpya, basi neno hili si lingine bali "UWAJIBIKAJI."
Katika mchakato wa kuandika katiba mpya, ni muhimu tukatambua ‘trade-offs' muhimu zinazohusiana na aina mbali mbali ya mabunge ya kidemokrasia. Trade-offs nitakayo zungumzia ni ile baina ya muundo wa ‘MAJORITY DEMOCRACY' na muundo wa ‘PROPORTION (uwiano) & CONSENSUS'. Tukianzia na ‘majority democracy', hii ni system ambayo imekuwa inatumika Tanzania chini ya katiba iliyopo na chini ya serikali ya Chama Cha Mapinduzi. Kwa jinsi hali ilivyo sasa, kuna ishara zote kwamba hata ikitokea kwa mfano CHADEMA wakafanikiwa kutwaa madaraka ya nchi hii mwaka 2015, hivyo kuwa katika nafasi ya kuunda serikali, CHADEMA itaendelea na mfumo uliopo wa ‘majority democracy.' Ni kawaida kwa watu kuwa na imani kwamba muundo wa ‘majority democracy', huzaa serikali/baraza la mawaziri lenye ‘stability', hivyo kupelekea uwepo wa mazingira ya maamuzi ya haraka ya serikali – kisera, pamoja na hali ya uwajibikaji wa hali ya juu kwa upande wa chama kinachofanikiwa kuunda serikali. Sidhani kama CHADEMA wangependelea mfumo mbadala na huu iwapo wakishinda.
Nimetoa mfano wa CHADEMA mwaka 2015 kwa makusudi kabisa kwani sidhani kama nitakuwa nimekosea kutamka kwamba malengo ya CHADEMA, kama chama chochote kingine cha siasa ni kushinda uchaguzi ili kuunda serikali na kukamata Dola. Sidhani kama ni makosa kusema pia kwamba iwapo CHADEMA itashinda uchaguzi mkuu wa 2015 hivyo kupata nafasi ya kuunda serikali, nia yao itakuwa kuunda serikali/baraza la mawaziri lenye ‘STABILITY' na ‘ACCOUNTABILITY' kuliko ilivyo sasa chini ya CCM. Kama nipo sahihi, basi ina maana kwamba, iwapo CHADEMA watafanikiwa kushinda kiti cha urais na majority of seats za majimboni 2015, CHADEMA itapendelea kutawala Tanzania chini ya mfumo ule ule wa sasa chini ya CCM – yani ‘Majority Democracy' kwani wakati wote, CHADEMA wamekuwa wakionyesha umma kwamba wana uwezo wa kusahihisha mapungufu chini ya CCM. Nadhani nipo sahihi kutamka haya kwani hata kauli za wabunge wengi wa Chadema mfano – Zitto, Mbowe, Lissu na wengineo, huwa zinaelezea masikitiko makubwa juu ya jinsi gani wanavyokosa nguvu ya kuiwajibisha serikali kutokana na uchache wao bungeni. Vile vile katika kampeni za chaguzi ndogo, CHADEMA huwa wanasisitiza kwa wapiga kura umuhimu wa kuongezewa idadi ya wabunge ili wawe katika nafasi nzuri zaidi ya kuiwajibisha serikali ya CCM.
Baada ya kujadili muundo wa ‘majority democracy', sasa tugeukie muundo wa ‘proportion and consensus' ili tuweze kubaini trade offs iliyopo na ‘majority democratic system'. Huu uwiano na Consensus ni baina ya vyama vya siasa. Kama ilivyo kwa mfumo wa ‘majoritary democracy, mfumo wa ‘proportion and consensus' pia una faida na hasara zake. Kwa mfano mara nyingi mfumo huu huzaa baraza la mawaziri lisiloishi kwa muda mrefu na huzaa mazingira magumu ya maamuzi ya haraka ya serikali – kisera; lakini pia una faida zake, hasa kuzaa mazingira ambayo mchakato wa maamuzi kisera huwa ni ‘more inclusive' & ‘more fair', unaowakilisha a ‘larger' majority ya wananchi kwani wawakilishi wa vyama vyote vikubwa hushiriki kwenye maamuzi katika mazingira ya usawa na makubaliano.
Baada ya kujadili miundo hii miwili, sasa tujiulize, JE: Katika Katiba Mpya, tulenge kipi hasa:
· Kuendeleza mfumo wa sasa wa ‘Majority Democracy' kwa nia ya kuimarisha stability ya serikali/baraza la mawaziri, kuimarisha mazingira yanayozaa maamuzi ya haraka ya serikali - kisera, na kuimarisha uwajibikaji wa kwa upande wa serikali?
OR
· Kujaribu mfumo mpya wa proportion na consensus kwa nia ya kuongeza ‘inclusiveness & fairness'?
Ni muhimu hapa tukatambua kwamba ni vigumu kuwa na miundo yote miwili kwa wakati mmoja.
Muundo wa Majority Democracy & Misuko suko chini ya Utawala wa Kikwete.
Hoja ya hivi majuzi ya Mh. Zitto imeamsha hisia za wengi wetu ambao siku hadi siku, tumekuwa tunazidi kukata tamaa kutokana na utendaji mbovu wa baadhi mawaziri wa Kikwete. Hoja ya Zitto imekuja wakati muafaka. Lakini kuna tatizo moja kubwa: ni vigumu kubaini iwapo mawaziri wanaotajwa kuwa wabovu watajiuzulu, basi tutakuwa tumetatua tatizo la ‘instability' ya serikali/baraza na mawaziri. Kwa mfano, Je, Tatizo ni nini hasa:
· Instability ya baraza la mawaziri/serikali kutokana na dhana ya collective responsibility?
· Matatizo yaliyopo kwenye baadhi ya wizara?
· Mapungufu ya mfumo wa ‘Majority Democracy'?
Kwa sasa, ni dhahiri kwamba iwapo Waziri Mkuu au Mawaziri husika watajiuluzu, bado ni CCM ndiyo itakayobunda tena serikali; Pia, mawaziri wengi watarudi, na kitacho badilika pengine ni nani atapewa dhamana katika wizara ipi. Bila mkakati mzuri, hali hii inaweza pelekea mabadiliko ya mawaziri kutokea mara kwa mara katika kipindi cha miaka mitatu iliyobakia. Na hii inanipeleka kujadili suala lingine muhimu la ‘cabinet turn over'/'turnover of personel' i.e. mabadiliko ya mara kwa mara ya baraza la mawaziri, pamoja na sababu zake na athari zake katika utendaji wa serikali.
Katika kipindi cha miaka saba ya utawala wa Rais Kikwete (2005 – 2012), Rais ameunda baraza la mawaziri sio chini ya mara nne. Hii ndio ‘turn over' ya personell niliyoitaja awali. Kwa jinsi hali ilivyo sasa, kuna kila dalili kwamba ‘turnover ya personel' chini ya Kikwete itakuwa ni kubwa kuliko awamu nyingine zote tangia uhuru. Swali la kujiuliza hapa ni je, kwanini imekuwa hivi? Je ni kutokana na instability ya serikali/baraza la mawaziri au matatizo ya wizara moja moja? Ni vigumu kupata jibu la moja kwa moja, hivyo ningependa kujenga hoja kwamba pengine hii ‘high turnover of personnel in the cabinet' inatokana na Rais Kikwete kukabiliwa na ugumu wa ‘talent allocation' tangia aingie madarakani. Nitahidi kufafanua.
Tuseme nipo sahihi – then, chini ya Ari Mpya, Nguvu Mpya na Kasi Mpya, Kikwete alianza awamu ya nne katika mazingira magumu/uncertainity kuhusu nani/kina nani ndio wenye uwezo wa kumsaidia kufanikisha kauli mbiu ya Ari Mpya, Nguvu Mpya na Kasi Mpya. Ningependa kutumia mfano wa wizara mbili ili kuimarisha hoja kwamba pengine Kikwete alianza na nia ya dhati ya kuweka maslahi ya taifa chini ya kauli mbiu ya ari, nguvu na kasi mpya. Tuchukue Wizara ya ‘Justice & Constitutional Affairs' kama mfano. Chini ya Ari Mpya, Nguvu Mpya na Kasi Mpya, hii ilikuwa ni moja ya wizara muhimu sana za kumsaidia Kikwete kufanikisha malengo ya maisha bora kwa kila mtanzania. Mbali ya kuitumia kuanzisha mchakato wa katiba mpya, Kikwete pia angeweza kuitumia kupanua wigo wa ‘Justice' ili kujumuisha ya the the three types of justice that operate as a triplets in any genuine democracy ambazo ni: POLITICAL JUSTICE, SOCIAL JUSTICE AND ECONOMIC JUSTICE. Kukosekana kwa moja ya haki hizi tatu ‘hudumaza' dhana nzima ya haki katika taifa.
Ndani ya malengo ya Maisha Bora Kwa Kila Mtanzania, kwa vile Minister for Justice ana uwezo/nafasi kubwa to influence ‘reforms' muhimu zenye uwezo wa kuongeza haki za watanzania kiuchumi, kisiasa na kijamii, Rais angeweza kumweka waziri wa sheria au mwanasheria kuu wa serikali ambae angekuwa na imani kwamba ataweza kusimamia such reforms kwa ustadi mkubwa ili kuzidi kujenga imani ya CCM na Serikali yake kwa watanzania. Hivyo, Rais angehitaji kujenga ‘trust' na mtu mmoja na kumteua kushika dhamana hiyo muhimu. Lakini mbali ya ‘trust' ya Rais kwa mtu wa namna hiyo, pia lipo suala la uwezo (ability) ya mtu huyo – kwa mfano mawaziri wanatakiwa kuwa na utaalamu na uzoefu wa kuwawezesha kuongoza/kusimami sera kwa ufanisi wa hali ya juu, hivyo kupelekea CCM na serikali yake kufanikiwa kutekeleza kwa mfano, ilani yake ya uchaguzi kwa ufanisi zaidi.
Waziri mwingine muhimu chini ya dhana ya Maisha Bora Kwa Kila Mtanzania ni Waziri wa Fedha. Rais alihitaji kuteua mtu mwenye ujuzi, uzoefu na uwezo wa kujtengeneza mazingira ya uchumi yatakayoendanana falsafa ya maisha bora kwa kila Mtanzania. Kwa mfano, kusimamia kwa ustadi mkubwa suala la mfumuko wa bei, kodi, thamai ya shilingi, kupunguza kasi ya deni la taifa na upatikanaji wa mikopo nafuu kwa wananchi. Waziri wa fedha wa kiwango hiki angeweza shirikiana na waziri wa Justice kwa kuhakikisha kwamba combination ya sera zao zingezaa economic growth (waziri wa fedha) na Social Justice (Waziri wa Justice) hivyo kufanikisha lengo la Rais la kuhakikika kuna Maisha Bora Kwa Kila Mtanzania. Mbali na haya, chini ya dhana ya Ari Mpya, Nguvu Mpya na Kasi Mpya, Rais angeweza kabisa kuja na kikosi tofauti cha mawaziri chenye uwezo mkubwa wa kisiasa/wa kujenga hoja mbalimbali, uwezo wa ku ‘negotiate' na upinzani wa ndani na nje ya CCM, ujasiri wa kukabiliana na waandishi wa habari kwa nguvu za hoja na sio hoja za nguvu, uwezo wa kusimamia sera na maamuzi ya serikali bungeni, uwezo wa kuwa ‘manage' watumishi wa umma ili wasipoteze ‘motivation', na mengineyo mengi ambayo yangepelekea CCM na serikali yake kuzidi kuwa na mafanikio katika siasa za ushindani.
Ningependa kumalizia na mambo yafuatayo: Tukiachilia mbali ukosefu wa maadili miongoni mwa baadhi ya mawaziri, hivyo kupelekea Serikali kuwa na utendaji mbovu, Je, ubovu wa serikali ya Kikwete unatokana na mambo mengine yapi?
1. Je, mwanzo wa utawala wake na hadi sasa, Kikwete anakabiliwa na wakati mgumu/uncertainity kuhusu kina nani wana uwezo wa kuwa MAWAZIRI BORA tofauti na sasa ambapo tuna BORA MAWAZIRI? Kwani the higher the uncertainty on part of the President juu ya hilo, the more likely atateua mawaziri wabovu.
2. Je, tatizo ni kwamba mchakato wa sasa wa kupata wabunge hauzai watu wenye elimu, uzoefu na utaalam wa kuwawezesha kuwa mawaziri bora? Kwani uncertainty on part of Rais kuhusu wabunge gani wanafaa kuwa mawaziri inapungua iwapo kuna a large pool ya wabunge wenye uwezo wa kuwa mawaziri bora ambao ni zao la mchakato wa uchaguzi mkuu uliojaa ushindani mkubwa lakini katika mazingira ya haki na demokrasia ya kweli.
3. Je, wabunge wenye uwezo huwa wapo wakati wote lakini kuna utamaduni wa kutowapa nafasi?
4. Je, tatizo ni umri wetu wa mdogo ndani ya Demokrasia? Kwani uncertainity on part of Rais kuhusu kina nani wana uwezo wa kuwa mawaziri bora huwa ni kubwa zaidi katika nchi zilizopo katika hatua za awali ya demokrasia. Kwa mfano, nchi yenye uzoefu mdogo na mfumo unaofuata utawala wa Baraza la mawaziri hupelekea ukosefu wa idadi ya kutosha ya wataalam, lakini pia ukosefu wa taarifa kuhusu watu gani wana sifa za kuwa mawaziri bora, hivyo kumpa Rais wakati mgumu kupata mawaziri bora kutoka miongoni mwa wabunge. Na kwa Tanzania, je, kipindi gani ndicho sahihi kuanza kuhesabu umri wetu ndani ya demokrasia miaka: 1961 (uhuru)? 1967 (ujamaa)? 1985 (soko huria)? 1992/3 (mfumo wa vyama vingi)??????
Mwisho kabisa, nimalizie kwa kusema kwamba, binafsi nina amini kwamba iwapo mchakato wa kuwapata viongozi/wenyeviti wa kamati mbalimbali za bunge ungekuwa unazingatia haki, uwazi, elimu, uzoefu na utalaam wa wagombea katika fani zao mbalimbali, hali hii ingempunguzia Rais ugumu wa kupata wabunge wenye uwezo wa kuongoza wizara mbalimbali kwa ufanisi kwa sababu Rais angekuwa na nafasi nzuri ya kuteua wabunge ambao ni wenyeviti wa kamati mbali mbali za bunge ambao wamekuwa wanaonyesha uwezo mkubwa wa kuongoza kamati zao. Kwa mfano tukiweka ushabiki wa vyama pembeni na kuangalia maslahi ya nchi, ni wazi kwamba wabunge kama Zitto, Cheyo, Kigoda, Lissu wameonyesha ‘performance' ya hali ya juu katika kamati zao, na kutoa ishara kwamba kwamba wanaweza kabisa kuwa Mawaziri Bora na sio Bora Mawaziri kwa mfano wakipata nafasi za kuongoza wizara zinazoendana na shughuli za kamati zao za bunge.
Naomba kuwasilisha.
Nia ya makala hii ni kujaribu kuja na mada ya kutusaidia kuachana japo kwa mara moja, na mtazamo/uchambuzi tuliouzoea wa kutoangalia mambo nje ya boksi juu ya suala la instability ya serikali ya awamu ya nne, na badala yake kuangalia suala hili kwa mapana na marefu zaidi. Ni imani yangu kwamba zoezi linaweza kutusaidia kubadilisha mawazo zaidi na kuzidi kutuandaa na mchakato wa kupata Katiba Mpya. Kama anavyohimiza Mh. Zitto, iwapo tunahitaji neno moja tu ndani ya katiba yetu mpya, basi neno hili si lingine bali "UWAJIBIKAJI."
Katika mchakato wa kuandika katiba mpya, ni muhimu tukatambua ‘trade-offs' muhimu zinazohusiana na aina mbali mbali ya mabunge ya kidemokrasia. Trade-offs nitakayo zungumzia ni ile baina ya muundo wa ‘MAJORITY DEMOCRACY' na muundo wa ‘PROPORTION (uwiano) & CONSENSUS'. Tukianzia na ‘majority democracy', hii ni system ambayo imekuwa inatumika Tanzania chini ya katiba iliyopo na chini ya serikali ya Chama Cha Mapinduzi. Kwa jinsi hali ilivyo sasa, kuna ishara zote kwamba hata ikitokea kwa mfano CHADEMA wakafanikiwa kutwaa madaraka ya nchi hii mwaka 2015, hivyo kuwa katika nafasi ya kuunda serikali, CHADEMA itaendelea na mfumo uliopo wa ‘majority democracy.' Ni kawaida kwa watu kuwa na imani kwamba muundo wa ‘majority democracy', huzaa serikali/baraza la mawaziri lenye ‘stability', hivyo kupelekea uwepo wa mazingira ya maamuzi ya haraka ya serikali – kisera, pamoja na hali ya uwajibikaji wa hali ya juu kwa upande wa chama kinachofanikiwa kuunda serikali. Sidhani kama CHADEMA wangependelea mfumo mbadala na huu iwapo wakishinda.
Nimetoa mfano wa CHADEMA mwaka 2015 kwa makusudi kabisa kwani sidhani kama nitakuwa nimekosea kutamka kwamba malengo ya CHADEMA, kama chama chochote kingine cha siasa ni kushinda uchaguzi ili kuunda serikali na kukamata Dola. Sidhani kama ni makosa kusema pia kwamba iwapo CHADEMA itashinda uchaguzi mkuu wa 2015 hivyo kupata nafasi ya kuunda serikali, nia yao itakuwa kuunda serikali/baraza la mawaziri lenye ‘STABILITY' na ‘ACCOUNTABILITY' kuliko ilivyo sasa chini ya CCM. Kama nipo sahihi, basi ina maana kwamba, iwapo CHADEMA watafanikiwa kushinda kiti cha urais na majority of seats za majimboni 2015, CHADEMA itapendelea kutawala Tanzania chini ya mfumo ule ule wa sasa chini ya CCM – yani ‘Majority Democracy' kwani wakati wote, CHADEMA wamekuwa wakionyesha umma kwamba wana uwezo wa kusahihisha mapungufu chini ya CCM. Nadhani nipo sahihi kutamka haya kwani hata kauli za wabunge wengi wa Chadema mfano – Zitto, Mbowe, Lissu na wengineo, huwa zinaelezea masikitiko makubwa juu ya jinsi gani wanavyokosa nguvu ya kuiwajibisha serikali kutokana na uchache wao bungeni. Vile vile katika kampeni za chaguzi ndogo, CHADEMA huwa wanasisitiza kwa wapiga kura umuhimu wa kuongezewa idadi ya wabunge ili wawe katika nafasi nzuri zaidi ya kuiwajibisha serikali ya CCM.
Baada ya kujadili muundo wa ‘majority democracy', sasa tugeukie muundo wa ‘proportion and consensus' ili tuweze kubaini trade offs iliyopo na ‘majority democratic system'. Huu uwiano na Consensus ni baina ya vyama vya siasa. Kama ilivyo kwa mfumo wa ‘majoritary democracy, mfumo wa ‘proportion and consensus' pia una faida na hasara zake. Kwa mfano mara nyingi mfumo huu huzaa baraza la mawaziri lisiloishi kwa muda mrefu na huzaa mazingira magumu ya maamuzi ya haraka ya serikali – kisera; lakini pia una faida zake, hasa kuzaa mazingira ambayo mchakato wa maamuzi kisera huwa ni ‘more inclusive' & ‘more fair', unaowakilisha a ‘larger' majority ya wananchi kwani wawakilishi wa vyama vyote vikubwa hushiriki kwenye maamuzi katika mazingira ya usawa na makubaliano.
Baada ya kujadili miundo hii miwili, sasa tujiulize, JE: Katika Katiba Mpya, tulenge kipi hasa:
· Kuendeleza mfumo wa sasa wa ‘Majority Democracy' kwa nia ya kuimarisha stability ya serikali/baraza la mawaziri, kuimarisha mazingira yanayozaa maamuzi ya haraka ya serikali - kisera, na kuimarisha uwajibikaji wa kwa upande wa serikali?
OR
· Kujaribu mfumo mpya wa proportion na consensus kwa nia ya kuongeza ‘inclusiveness & fairness'?
Ni muhimu hapa tukatambua kwamba ni vigumu kuwa na miundo yote miwili kwa wakati mmoja.
Muundo wa Majority Democracy & Misuko suko chini ya Utawala wa Kikwete.
Hoja ya hivi majuzi ya Mh. Zitto imeamsha hisia za wengi wetu ambao siku hadi siku, tumekuwa tunazidi kukata tamaa kutokana na utendaji mbovu wa baadhi mawaziri wa Kikwete. Hoja ya Zitto imekuja wakati muafaka. Lakini kuna tatizo moja kubwa: ni vigumu kubaini iwapo mawaziri wanaotajwa kuwa wabovu watajiuzulu, basi tutakuwa tumetatua tatizo la ‘instability' ya serikali/baraza na mawaziri. Kwa mfano, Je, Tatizo ni nini hasa:
· Instability ya baraza la mawaziri/serikali kutokana na dhana ya collective responsibility?
· Matatizo yaliyopo kwenye baadhi ya wizara?
· Mapungufu ya mfumo wa ‘Majority Democracy'?
Kwa sasa, ni dhahiri kwamba iwapo Waziri Mkuu au Mawaziri husika watajiuluzu, bado ni CCM ndiyo itakayobunda tena serikali; Pia, mawaziri wengi watarudi, na kitacho badilika pengine ni nani atapewa dhamana katika wizara ipi. Bila mkakati mzuri, hali hii inaweza pelekea mabadiliko ya mawaziri kutokea mara kwa mara katika kipindi cha miaka mitatu iliyobakia. Na hii inanipeleka kujadili suala lingine muhimu la ‘cabinet turn over'/'turnover of personel' i.e. mabadiliko ya mara kwa mara ya baraza la mawaziri, pamoja na sababu zake na athari zake katika utendaji wa serikali.
Katika kipindi cha miaka saba ya utawala wa Rais Kikwete (2005 – 2012), Rais ameunda baraza la mawaziri sio chini ya mara nne. Hii ndio ‘turn over' ya personell niliyoitaja awali. Kwa jinsi hali ilivyo sasa, kuna kila dalili kwamba ‘turnover ya personel' chini ya Kikwete itakuwa ni kubwa kuliko awamu nyingine zote tangia uhuru. Swali la kujiuliza hapa ni je, kwanini imekuwa hivi? Je ni kutokana na instability ya serikali/baraza la mawaziri au matatizo ya wizara moja moja? Ni vigumu kupata jibu la moja kwa moja, hivyo ningependa kujenga hoja kwamba pengine hii ‘high turnover of personnel in the cabinet' inatokana na Rais Kikwete kukabiliwa na ugumu wa ‘talent allocation' tangia aingie madarakani. Nitahidi kufafanua.
Tuseme nipo sahihi – then, chini ya Ari Mpya, Nguvu Mpya na Kasi Mpya, Kikwete alianza awamu ya nne katika mazingira magumu/uncertainity kuhusu nani/kina nani ndio wenye uwezo wa kumsaidia kufanikisha kauli mbiu ya Ari Mpya, Nguvu Mpya na Kasi Mpya. Ningependa kutumia mfano wa wizara mbili ili kuimarisha hoja kwamba pengine Kikwete alianza na nia ya dhati ya kuweka maslahi ya taifa chini ya kauli mbiu ya ari, nguvu na kasi mpya. Tuchukue Wizara ya ‘Justice & Constitutional Affairs' kama mfano. Chini ya Ari Mpya, Nguvu Mpya na Kasi Mpya, hii ilikuwa ni moja ya wizara muhimu sana za kumsaidia Kikwete kufanikisha malengo ya maisha bora kwa kila mtanzania. Mbali ya kuitumia kuanzisha mchakato wa katiba mpya, Kikwete pia angeweza kuitumia kupanua wigo wa ‘Justice' ili kujumuisha ya the the three types of justice that operate as a triplets in any genuine democracy ambazo ni: POLITICAL JUSTICE, SOCIAL JUSTICE AND ECONOMIC JUSTICE. Kukosekana kwa moja ya haki hizi tatu ‘hudumaza' dhana nzima ya haki katika taifa.
Ndani ya malengo ya Maisha Bora Kwa Kila Mtanzania, kwa vile Minister for Justice ana uwezo/nafasi kubwa to influence ‘reforms' muhimu zenye uwezo wa kuongeza haki za watanzania kiuchumi, kisiasa na kijamii, Rais angeweza kumweka waziri wa sheria au mwanasheria kuu wa serikali ambae angekuwa na imani kwamba ataweza kusimamia such reforms kwa ustadi mkubwa ili kuzidi kujenga imani ya CCM na Serikali yake kwa watanzania. Hivyo, Rais angehitaji kujenga ‘trust' na mtu mmoja na kumteua kushika dhamana hiyo muhimu. Lakini mbali ya ‘trust' ya Rais kwa mtu wa namna hiyo, pia lipo suala la uwezo (ability) ya mtu huyo – kwa mfano mawaziri wanatakiwa kuwa na utaalamu na uzoefu wa kuwawezesha kuongoza/kusimami sera kwa ufanisi wa hali ya juu, hivyo kupelekea CCM na serikali yake kufanikiwa kutekeleza kwa mfano, ilani yake ya uchaguzi kwa ufanisi zaidi.
Waziri mwingine muhimu chini ya dhana ya Maisha Bora Kwa Kila Mtanzania ni Waziri wa Fedha. Rais alihitaji kuteua mtu mwenye ujuzi, uzoefu na uwezo wa kujtengeneza mazingira ya uchumi yatakayoendanana falsafa ya maisha bora kwa kila Mtanzania. Kwa mfano, kusimamia kwa ustadi mkubwa suala la mfumuko wa bei, kodi, thamai ya shilingi, kupunguza kasi ya deni la taifa na upatikanaji wa mikopo nafuu kwa wananchi. Waziri wa fedha wa kiwango hiki angeweza shirikiana na waziri wa Justice kwa kuhakikisha kwamba combination ya sera zao zingezaa economic growth (waziri wa fedha) na Social Justice (Waziri wa Justice) hivyo kufanikisha lengo la Rais la kuhakikika kuna Maisha Bora Kwa Kila Mtanzania. Mbali na haya, chini ya dhana ya Ari Mpya, Nguvu Mpya na Kasi Mpya, Rais angeweza kabisa kuja na kikosi tofauti cha mawaziri chenye uwezo mkubwa wa kisiasa/wa kujenga hoja mbalimbali, uwezo wa ku ‘negotiate' na upinzani wa ndani na nje ya CCM, ujasiri wa kukabiliana na waandishi wa habari kwa nguvu za hoja na sio hoja za nguvu, uwezo wa kusimamia sera na maamuzi ya serikali bungeni, uwezo wa kuwa ‘manage' watumishi wa umma ili wasipoteze ‘motivation', na mengineyo mengi ambayo yangepelekea CCM na serikali yake kuzidi kuwa na mafanikio katika siasa za ushindani.
Ningependa kumalizia na mambo yafuatayo: Tukiachilia mbali ukosefu wa maadili miongoni mwa baadhi ya mawaziri, hivyo kupelekea Serikali kuwa na utendaji mbovu, Je, ubovu wa serikali ya Kikwete unatokana na mambo mengine yapi?
1. Je, mwanzo wa utawala wake na hadi sasa, Kikwete anakabiliwa na wakati mgumu/uncertainity kuhusu kina nani wana uwezo wa kuwa MAWAZIRI BORA tofauti na sasa ambapo tuna BORA MAWAZIRI? Kwani the higher the uncertainty on part of the President juu ya hilo, the more likely atateua mawaziri wabovu.
2. Je, tatizo ni kwamba mchakato wa sasa wa kupata wabunge hauzai watu wenye elimu, uzoefu na utaalam wa kuwawezesha kuwa mawaziri bora? Kwani uncertainty on part of Rais kuhusu wabunge gani wanafaa kuwa mawaziri inapungua iwapo kuna a large pool ya wabunge wenye uwezo wa kuwa mawaziri bora ambao ni zao la mchakato wa uchaguzi mkuu uliojaa ushindani mkubwa lakini katika mazingira ya haki na demokrasia ya kweli.
3. Je, wabunge wenye uwezo huwa wapo wakati wote lakini kuna utamaduni wa kutowapa nafasi?
4. Je, tatizo ni umri wetu wa mdogo ndani ya Demokrasia? Kwani uncertainity on part of Rais kuhusu kina nani wana uwezo wa kuwa mawaziri bora huwa ni kubwa zaidi katika nchi zilizopo katika hatua za awali ya demokrasia. Kwa mfano, nchi yenye uzoefu mdogo na mfumo unaofuata utawala wa Baraza la mawaziri hupelekea ukosefu wa idadi ya kutosha ya wataalam, lakini pia ukosefu wa taarifa kuhusu watu gani wana sifa za kuwa mawaziri bora, hivyo kumpa Rais wakati mgumu kupata mawaziri bora kutoka miongoni mwa wabunge. Na kwa Tanzania, je, kipindi gani ndicho sahihi kuanza kuhesabu umri wetu ndani ya demokrasia miaka: 1961 (uhuru)? 1967 (ujamaa)? 1985 (soko huria)? 1992/3 (mfumo wa vyama vingi)??????
Mwisho kabisa, nimalizie kwa kusema kwamba, binafsi nina amini kwamba iwapo mchakato wa kuwapata viongozi/wenyeviti wa kamati mbalimbali za bunge ungekuwa unazingatia haki, uwazi, elimu, uzoefu na utalaam wa wagombea katika fani zao mbalimbali, hali hii ingempunguzia Rais ugumu wa kupata wabunge wenye uwezo wa kuongoza wizara mbalimbali kwa ufanisi kwa sababu Rais angekuwa na nafasi nzuri ya kuteua wabunge ambao ni wenyeviti wa kamati mbali mbali za bunge ambao wamekuwa wanaonyesha uwezo mkubwa wa kuongoza kamati zao. Kwa mfano tukiweka ushabiki wa vyama pembeni na kuangalia maslahi ya nchi, ni wazi kwamba wabunge kama Zitto, Cheyo, Kigoda, Lissu wameonyesha ‘performance' ya hali ya juu katika kamati zao, na kutoa ishara kwamba kwamba wanaweza kabisa kuwa Mawaziri Bora na sio Bora Mawaziri kwa mfano wakipata nafasi za kuongoza wizara zinazoendana na shughuli za kamati zao za bunge.
Naomba kuwasilisha.