Mawakili wa Jamuhuri wasipokuwa makini watairahisishia kazi ICC, maana wanataka kuingiza mahakamani mambo ya Oktoba 29

Mawakili wa Jamuhuri wasipokuwa makini watairahisishia kazi ICC, maana wanataka kuingiza mahakamani mambo ya Oktoba 29

Leo lissu sincerely kageuka kuwa
Haya ni maoni yangu.

Kwa yaliyotokea leo mahakamani ni kana kwamba mawakili wa serikali wanahisi ushahidi unaotolewa na mashahidi wa upande wao hauwezi kumtia hatiani Lissu, hivyo wameamua kutaka kuingiza ushahidi unaohusu Octoba 29, kwa nia ya kuongeza substance ya kumkuta Lissu na hatia.

Mi ninachoona hapa ni kama vile samaki anaweza kukaangwa kwenye mafuta yake mwenyewe. Maana hata kama mimi sio mwanasheria, lakini najua hii move itakuwa imempa pumzi kubwa sana Lissu ya kufichua mambo ambayo serikali kwa hii miezi minne wamekuwa wakipambana kuyaficha.

Lakini kingine ambacho serikali wanapaswa kutambua ni kwamba: ICC wanaonekana kucheza blind game, kwa kuonekana kwamba hawajayaona yaliyotokea Tanzania, na ni kama hii blind game inaenda ikifanikiwa kwasababu sasa ni kama serikali wanataka kukiweka kila kitu hadharani kupitia kesi ya Lissu.

Na kwa kweli mimi sio mwanasheria nguli, ila the moment mahakama itakubali huu ushahidi mpya wa Octoba 29 uingie mahakamani, sio tu ufawafanya watanzania mamilioni waanze kuifuatilia hii kesi, bali pia jumuiya ya kimataifa (ukijumuisha ICC) watakuwa wamepata mwanya wa kufanya validation ya ushahidi wowote ule ambao ulitumwa kwao.

Kwahiyo hii move ya kina Katuga, is not well thought. Madhara yake yatakuwa na mwangwi ambao hawatautarajia. Si kwasababu pia itamruhusu Lissu kuja na mashahidi wake wa kilichotokea Octoba 29 au?

Kwa hii move, mawakili wa serikali mtakuwa mmefanya sabotage kwa serikali ya CCM, lazima ita-back-fire kwa namna ambayo hamtaipenda.

Wenu,
MC

Leo Lissu sincerely kawashauri hawa jamaa jambo la maana, kama ambavyo siku zote hawataki kusikia hii move ni mbaya kweli.
 
Lakini kwa majibu ya Lissu leo mahakamani, ni kama vile sheria inaruhusu mashahidi wapya, kwahiyo hilo likitokea na Lissu akaleta mashahidi wake wa Octoba 29, itakuwa ni ushindi mkubwa sana. Hiyo ndo itakuwa precedence ya ICC kufanya yao.
Ni kama jamhuri walikuwa hawajui kuwa wataenda kurefusha ushahidi kwa pande zote mbili,hata majaji hawakujua madhara yake mpaka pale Lissu alipo watahadharisha nini kitafuata na yupo tayari.
Kiukweli hakukuwa na uwanja wa kuahirisha kesi maana kifungu kinajieleza wazi kuwa ni shahidi mpya kuongezwa...
Majaji wamehamaki
 
Lakini kwa majibu ya Lissu leo mahakamani, ni kama vile sheria inaruhusu mashahidi wapya, kwahiyo hilo likitokea na Lissu akaleta mashahidi wake wa Octoba 29, itakuwa ni ushindi mkubwa sana. Hiyo ndo itakuwa precedence ya ICC kufanya yao.
Tundu Lissu: Mheshimiwa jaji naomba kumuuliza shahidi kuhusu mauaji ya 29/10/2025.

Nani ana mamlaka ya kisheria kutoa amri kuuwa kwa risasi, hapa Tanzania.

Swali la pili. Mahakama ipo tayari Kupokea ushahidi wa sauti na picha ili kuthibitisha kuwa vyombo vya dola viliuwa.

Swali la tatu: Mahakama ipo tayari kumleta hapa amiri jeshi kutoa ushahidi kwa hotuba yake ?

Ni hayo tu Mheshimiwa sana.

Nimewaza tu kwa maandishi yangu itakavyokuwa wakiruhusu ushahidi wa genocide.
 
Hapa watampa mwanya wa Lissu kuongeza mashahidi wake wa kutosha hasa wafiwa na walemavu walio mtaani,
Mafwele na wenzake wataletwa mahakamani, maana saiv wanafichwa na kulinda
Waliyotoa order ya shut to kill wataanikwa
Mungu ni mwema mambo yatakuwa wazi, CCM wameamua kutumia mawakili wapumbavu kujivua nguo
Watakuwa wamejiingiza kwenye shimo ambalo watashindwa kuona pakutokea.
 
Leo lissu sincerely kageuka kuwa


Leo Lissu sincerely kawashauri hawa jamaa jambo la maana, kama ambavyo siku zote hawataki kusikia hii move ni mbaya kweli.
Na ushauri wa Lissu umekuwa kama mtego, wao wakichukulia kwamba Lissu anaogopa kuyazungumzia ya Octoba 29, halafu wakaamua kuyaingiza, ndo itampa mwanya Lissu wa kuwababua na moto usoni. Hii session ya leo imekuwa na umuhimu mkubwa sana kwenye hii kesi
 
Ni kama jamhuri walikuwa hawajui kuwa wataenda kurefusha ushahidi kwa pande zote mbili,hata majaji hawakujua madhara yake mpaka pale Lissu alipo watahadharisha nini kitafuata na yupo tayari.
Kiukweli hakukuwa na uwanja wa kuahirisha kesi maana kifungu kinajieleza wazi kuwa ni shahidi mpya kuongezwa...
Majaji wamehamaki
Wao Jamuhuri walijua kwamba wakiyaleta ya Octoba 29 basi itakuwa rahisi kwao kuunganisha narrative ya ushahidi unaotolewa. Ila naona kama hypotheses zao zimekosa uhalisia kwasababu ya Octoba 29 ni mapana sana, wanataka kuingia kwenye mto ambao hawajui kina chake.
 
Nilikuwa najua kuna wanasheria wa serikali wajinga, ila nilikiwa sijajua wapo wajinga kiasi hiki.

Hao wanasheria na polisi.

Kesi hii imewaanika ujinga wao.
1771849842801.png
 
Wanajua wanamkomoa asee saiv ndio naamin ccm ni chama cha manyumbu kabisa unashindwa kufikis la mbele na matokeo yake asa hapo madalakan wanafanya nini mbona hawana hadh ya kuwa viongozi
Hapo wanahisi wakiyaleta ya Octoba 29 kwamba itawarahisishia kazi ila ndo wanaenda kujibabua
 
Tundu Lissu: Mheshimiwa jaji naomba kumuuliza shahidi kuhusu mauaji ya 29/10/2025.

Nani ana mamlaka ya kisheria kutoa amri kuuwa kwa risasi, hapa Tanzania.

Swali la pili. Mahakama ipo tayari Kupokea ushahidi wa sauti na picha ili kuthibitisha kuwa vyombo vya dola viliuwa.

Swali la tatu: Mahakama ipo tayari kumleta hapa amiri jeshi kutoa ushahidi kwa hotuba yake ?

Ni hayo tu Mheshimiwa sana.

Nimewaza tu kwa maandishi yangu itakavyokuwa wakiruhusu ushahidi wa genocide.
Hahaha, naona ume-forward looking namna mtanange utakavyokuwa
 
Na ushauri wa Lissu umekuwa kama mtego, wao wakichukulia kwamba Lissu anaogopa kuyazungumzia ya Octoba 29, halafu wakaamua kuyaingiza, ndo itampa mwanya Lissu wa kuwababua na moto usoni. Hii session ya leo imekuwa na umuhimu mkubwa sana kwenye hii kesi

Utaamua hatima ya kesi, maana kwa upande wao bila hii move washaona mashahidi wataisha na hakuna kipya!

Wanatakiwa kuchutama ki utu uzima wamuachie jamaa wa watu
 
kinachozungumzwa kwenye kesi ya lissu ni ishu ya uchaguzi na sidhani matukio ya 29 Octoba hatakuwemo kwenye records
Kinachoongelewa kwa kina na mashahidi ni(kufanya fujo) kukinukisha, mashahidi wote walihamasika kukinukisha,wachache wameongelea kuvuruga uchaguzi.
Matokeo ya kukinukisha ni hayo ya 29 October ambayo ndiyo anaungiwa na ushahidi wa ACP Mahinda alioufanyia upelelezi baada ya uchaguzi
 
Kinachoongelewa kwa kina na mashahidi ni(kufanya fujo) kukinukisha, mashahidi wote walihamasika kukinukisha,wachache wameongelea kuvuruga uchaguzi.
Matokeo ya kukinukisha ni hayo ya 29 October ambayo ndiyo anaungiwa na ushahidi wa ACP Mahinda alioufanyia upelelezi baada ya uchaguzi
Lissu nae ataleta mashahidi wake akina na Sativa wale waliotekwa na Mafwele, hopefully na Mafwele ataletwa mahakamani
Lissu utamkutaje na hatia wakati wa uchaguzi alikuwa jera Toka mwezi April.
Yaani hili ndo jambo nalitamani waleingize masuala ya mo29 tuwavue nguo
 
Watu wengi wanadhani Tundu Lissu anapinga hii kitu (matukio ya mauaji ya 29/10 - 4/11/2025 kuingia mahakamani. LA HASHA...!

Anachopinga Tundu Lissu ni njia ya kuliingiza hili kinyume cha sheria. Kawaambia kama wanataka liingie, walilete kupitia proper channels za kisheria na kisha wapambane...

Honestly, hata sisi tunataka matukio ya MO29/10 na kuendelea yaingie na kujadiliwa mahakamani na kumbukumbu zake zitunzwe...!

Kwa lugha rahisi ni kuwa, hii inapaswa kuwa kesi mpya ya makosa mapya na hivyo inapaswa kuandaliwa ushahidi mpya na vivyo hivyo mshitakiwa kuandaa mashahidi na ushahidi wake mpya ktk kujitetea kwake...
 
Hata ukifuatilia ushahidi ulio tolewa wote umelenga kilicho tokea 29 October,kila shahidi ana kuja na ushahidi ule ule wa kuona video ya kukinukisha na kuhamasika. Wote waliiona video tarehe 4 kwenye simu zao.
Na wote walihamasika na kutenda kile walichohamasishwa.

Kwa nini sasa wahalifu wakawa mashahidi badala ya kuwa ni washitakiwa!

Mimi na wewe tuendelee kujiuliza aina hii ya kesi ya Lissu!
 
Back
Top Bottom