Maumivu na raha ya kukataliwa

Maumivu na raha ya kukataliwa

Nakumbuka kama bado siku mbili kufanya necta nikamtongoza dada fulani aiseee akanichomolea halafu alikuwa ndio mwanamke wa kwanza kumtongoza kwa kweli nilikaa mwaka mzima bila kutongoza
kila nikifikiria inaniuma alikuwa mzuri kweli.

Kuna huyu mwengine tulikuwa tupo mahali tunasoma ni mzuri kweli baba yake alikuwa professor udsm kipindi hiko simu zinzingia room ya computer nikafika hadi alipokaa nikachukua simu yake nikaipiga namba yangu kisha nikarudi pa kukaa Nakumbuka usiku wake alinitumia good night aiseee sikulala siku hiyo nilikuwa namuogopa mpaka basi baada ya masomo nilimkuta anadrive mkoko mimi nimeshika bomba kwenye daladala akanipa hi nilitamani nijifiche kwa kweli

Kuna huyu alikuwa jirani yetu kipindi hicho hapa Dar kuna vipori tulikuwa tunafuga mbuzi kulikuwa kuna msichana fulani hivi anasoma olympio kipindi hicho ni ya kishua basi kila nikionana naye namhadithia kwamba kwetu kuna mbuzi mpaka akapata akili sasa hivi ana mtoto huyu ndio namjutia kwa kweli najiona mjinga kila nikikutana naye

Hao ndio niliwakosa kwa kweli

Hahaha hivi vistori vyako...wew siku mbili kabla ya necta ulikua unatongoza ya nin?
 
Dah!mapenzi mh!!!yalisababisha nikarudia mtihani wa kidato cha nne, mdada nilimpenda nilijivunia urembo wake akaniteka nikawa mateka wa mapenzi, kutokana na uwezo wangu class nikawa namfundisha baadhi ya masomo, ikiwa imebaki mwezi mmoja tufanye paper ya kumaliza nikamfumania akiwa na jamaa mwingine, dah nilichanganyikiwa nikafanya paper vibaya.sijui na haitatokea kupenda vile.
 
Mialienipiga kibuti ni senior member humuhumu jamvini 😛eep::horn:
 
Nikipenda mwanamke akinitosa ndo natamani zaidi kuwa nae na kumpenda hadi kutoa hata chochote cha thamani ila akinikubali tu simpendi tena namuona hana thamani. Law of diminishing marginal utility in b place
 
Nikipenda mwanamke akinitosa ndo natamani zaidi kuwa nae na kumpenda hadi kutoa hata chochote cha thamani ila akinikubali tu simpendi tena namuona hana thamani. Law of diminishing marginal utility in b place
Angalia wasije wakakuita mfupi wa kimo maana wanasema wanaume wafupi ni noma kwa kukomalia watu
 
Mimi kuna mmoja namsotea mpaka amenichizisha sasa, yaani ni shiiiiiiida!.
 
Mapenzi huwa mnatoa nusu nusu kumbe ndio maana watu hawadumu kwenye mapenzi au ndoa, kumbe siri ni hii!!!!!
 
Kwa nini leo hii ulikua usimlipizie, ungemuelezea mpaka saivi bado nakupenda ili kulipa kisasi
 
Umri unahusu nini hapa..? Elewa tu mie ni mkubwa kwako.. Nimetoa opinion yangu kuhusu hii dhana..
Ungekuwa ni mkubwa ungejua msingi wa swali langu ....

Usijisumbue kujibu tena umri wako kwakuwa tayari nimeshaujua!
 
Back
Top Bottom