Pole kwa unayopitia dada Tina,
Hii kauli imenishangaza sana''Nilikuwa nina uhakika kwamba anachepuka lakini nikajipa moyo anatumia condom''
Kuchepuka ni tabia ya kutokujali, kwa tabia hii usitegemee mtu huyu kujali kutumia condom maana kama mchepuko ni wa muda mrefu huwa ndio condom zinasahaulika kabisa.
Najua shida yako ni maambukizo ya magonjwa ya zinaa hasa HIV-AIDS ,fanya maamuzi na chukua muda wako na uende kupima, miaka 38 bado sana usikubali babu wa miaka 52 akushike mkono kukuwaisha ahera.