Maudhi ya operesheni kimbunga!!

Maudhi ya operesheni kimbunga!!

Jipe moyo. Adha ya namna hii itampata kila mtu mahala popote. Ila zoezi lina nia njema, kwani uhamiaji haramu ni threat to the national security. Ugumu wake unatokana na kukosa national ID.



Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Tuache ubaguzi,wengine tusijione watz zaidi kuliko wengine,kama ni mtanzania mwenzetu na anaonewa lazima tumtetee kwa nguvu zote.Tumewafukuza watutsi sasa tunaanza kubaguana wenyewe,mwishowe tutasema hata Wakwere walitokea burundi enzi za biashara ya utumwa na baada ya uhuru kufuata ndugu zao Bagamoyo

yangu macho kako.kesho utasikia hawa wangoni na wanyasa warudi kwao..inaniuma mtu kazaliwa tanzania miaka 45 iliyopita, wazazi wake walilitokea burundi,wakafia pale uyowa ulyanhulu tbr..vijana wakasambaa wengine wapo serikalini yule kaka yao na wadogo zake wa kijiji wao ni haramu,ila hawa wa serekalini ni halali.serikali ije na mipango imara bhana.sio ubabe ubabe
 
vizuri. Lakin mbona raia wa uganda.kenya na rwanda watimuliwe kama mbuzi na raia wa malawi waambiwe wakajiandikishe wapate vibali? Nijibu mkuu

raia wa malawi wengi wao wanatumiwa kama cheap labour na matajiri,,,,niwataalamu sana katika mambo ya bustani,,usafi wamazingira,viwandani,na ulinzi,,,matajiri wengi wanawatumia katika maitaji yao kwa ajili yakupunguza cost,,,hao ndio watakuwa wanawakingia kifua hawa jamaa wamalawi wasiondoke tz wabaki kuwatumikia hawa matajiri,,,,wamalawi wengi wanaishi kawe,,,,mfano kuna hoteli moja ipo karume ilala,,,wamejaa sana pale,,,mpaka leo wapo wanakula bata..
 
Jipe moyo. Adha ya namna hii itampata kila mtu mahala popote. Ila zoezi lina nia njema, kwani uhamiaji haramu ni threat to the national security. Ugumu wake unatokana na kukosa national ID.



Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums

kuna mwaka fulani hivi tulivuka mpaka kwenda kula Debe(mziki) mishale ya saa kumi na moja tunarudi stendi tukakamatwa na askari wa kenya..kitu cha kwanza kuulizwa (unatoka wapi na unakwenda wapi wapi)? Wapi Kipande yako,kaa chini.kitambulisho cha taifa muhimu sana.sema tu tumechelewa
 
kwanza naomba ku-declare interest yangu hapa!

"i am not only a tanzanian or just a luo, but a citizen of the world...."

tarehe 16/09/2013 niliitwa uhamiaji makao makuu kwa kisingizio kuwa mimi si raia halali wa nchi ya tanzania...

Walifuatilia jina langu; wakaangalia na sura yangu eti waka-rule out kuwa mimi si raia wa tanzania! Wengi wamepata kashi kashi

hizi hapa mjini na maeneo mengine kama arusha, kigoma, kagera, musoma, mwanza, n.k

wakaniuliza maswali mengi likiwemo hili la kustaajabisha kidogo... Kuwa "babu mzaa baba yangu au bibi mzaa mama yangu aliingia

lini nchini tanzania...???" maswali ya kipuuzi nami niliwajibu kipuuzi "sijuhi kwa sababu sikuwepo kuthibitisha kama ni kweli walitoka

sehemu nyingine kuingia nchini tanzania ama la"

lakini nami nikawauliza sheria inasemaje kuhusu uraia? - maelezo niliyopewa hayakuridhisha na ni kiri tu kuwa wale jamaa

wanaoweka pale ni weupe sana kichwani!

Nikauliza tena swali: Nani ni mtanzania? Je kama tukianza kuwafuatilia watu kwa asili ya majina yao na maeneo tunayohisi historia

ndiko ilikoanzia kuna watu watakuwa watanzania kweli?

Jamani maudhi ya operesheni hii ni mengi sana usiombe yakufikie! Ni waase tu wale wenye majina yenye asili ya nchi kama kenya,

sudani kusini, congo drc, uganda, rwanda, burundi, n.k kamwe usitembee bila vitambulisho vyako - birth certificate, voter id, n.k.

Zoezi hili linaweza kuwa na nia njema kabisa lakini waliopewa kulisimamia na mbinu wazazotumia zitatuachia nyufa nyingi sana na

uhasama mkubwa sana na majirani zetu! Lakini pia unabaki unajiuliza maswali mengi bila majibu.

Ina maana hapa nchini usalama wa taifa hawajui majukumu yao?

Mbona zoezi hili ni kwa baadhi ya watu tu tena waafrika wenzetu?

Mbona zoezi linazingatia majina ya watu na muonekano wa sura zao tu?

Je, ni halali kwa waendesha operesheni kukamata/kugawana mali za watuhumiwa?

Je, taratibu za kidiplomasia zinaelekeza hivi au hizi ni hasira dhidi ya kenya, rwanda na uganda?

upo sahihi mkuu,,,hawa jamaa wanaofanya zoezi la utambuzi na kuchukua maelezo walitakiwa wakalishwe darasani kabla ya hili zoezi halijaanza,,,,

maana hii operation kimbunga inaweza ikawakumba hata wasio na husika na kuwasababishia usumbufu usiokuwa na sababu,,,,
 
[h=3]MATATIZO YA OPERATION KIMBUNGA

WATANZANIA 70 WARUDISHWA NCHINI KUTOKEA RWANDA
[/h]
Serikali ya nchi ya Rwanda imewarejesha watanzania 70 jamii ya wafugaji wa kabila la wahima na wazinza waliokamatwa kimakosa katika operesheni kimbunga inayoendelea nchini na kuwataka wananchi wake kuwa watulivu wakati kamati ya bunge la jumuiya ya Afrika Mashariki ikishughulikia mgogoro uliopo kati ya rwanda na nchi ya Tanzania
 
Binafsi naona zoezi linasuasua,piteni hadi uku kitaani nyumba hadi nyumba wakenya wamejaa
 
Tatizo watu wame vamia operesheni kichwa kichwa bila kujiandaa,
Ni sawa na daktari kwenda kumfanyia operesheni mgonjwa bila kuandaa visu, taa wala dawa ya usingizi,
Matokeo yake anamweka mgonjwa kwa operating table na kumsafisha halafu anaanza kuhaha
Kwengine ukionyesha kitambulisho cha uraia au passport au hata driving licence tu mchezo kwisha..kama wewe ni permanent resident, raia au haramu itajulikana , lakini hapa sisi loop holes kila pahala, na pesa za vitambulisho vya uraia zimegugunwa na panya
Labda sasa tuweke historians na anthropologists etc pale immigration watusaidie
 
jambo ninaloshangaa raia wa uganda,rwanda na kenya wakishikwa wanarudishwa kwao fasta,lakin raia wa malawi walioambiwa wakajiandikishe wapewe vibali vya kuishi.kwa nini raia wengine wasisingeambiwa hivo.

mimi naona kuna aina fulani ya kulipizana kisasi na jirani zetu wa afrika mashariki,pia walioshikwa wengi ni black wakat kuna wahindi,waarabu kibao,hawana vibali harafu kamanda anajidai kusema tumeshika na wahindi 2,ili ionekane kuna raia wengine pia.

na ata majirani zetu washausoma mchezo ndio maana wameanzisha umoja wao,na watatekeleza kwa vitendo waliyokubaliana ili watuache kwenye mataa.
sisi tutakalia na uchadema,uccm,unga etc

Wafuate mfanye maendeleo nao! SISI BONGO HATUACHWI KWENYE MATAA, TUNA UELEKEO WETU!
 
kwan wazaramo hawawez kuwa wahamiaj haram?.........sion sababu ya kuwafukuza walimu kutoka nje ya nchi maana wanawaelimisha vijana wetu tena wapo na vibali..
 
Hapo kuna issue gani wakati serikali inatimiza wajibu wake? au nawe mhamiaji haramu? kama mtu alichukuliwa kwa mahojiano akaonyesha vilelezo kisha akaachiwa kuna ubaya gani? kwanza huyo jamaa si ndiyo yule aliyeleta thread ya kuichafua Tanzania katika sakata la Immigration JNIA Airport?
Zoezi hili ni zuri lakini jinsi linavyofanyika sivyo kabisa.Watu wanachukuliwa kwa kuhisiwa wahamiaji haramu(sijui haramu kwa nani), wakibainika kuwa siyo wahamiaji haramu wanageuziwa kibao kuwa wanahisiwa kufanya biashara haramu.. Wananchi wananyanyaswa, wanadhalilishwa katika nchi yao na hii inatokea Dar es salaam sijui mikoani itakuwaje.
Inaonekana kama nia ya zoezi ni ukamataji zaidi kuliko kuonyesha vielelezo. Tunapoelekea sipo kabisa..
Usione rahisi kusema mtu anachukuliwa kwa mahojiano lakini maana yake ni nyingine kabisa.Watu wanalala lupango hadi siku mbili ili tu kuonyesha vielelezo wakati wana vielelezo vyote na ni raia halali..
 
Kama kawaida Tunafukuza WAO natujue na WETU watafukuzwa !! WaTanzania wengi wapo nchi za nje na nchi jirani wakiendesha maisha yao ya kila siku kama kawaida. Sasa zoezi hili la kutimua uhamiaji haramu linapowakumba Wakenya au waGanda, nk; Basi na wa Tz. wetu hawatasalimika nasi tutafukuzwa hii ndo sheria ya kisiasa zisizo na nidhamu. Tujipangee na kutayarisha kambi za kupokea wananchi wetu kutoka nje !! Hayo nisemayo yasiwashtue lakini Ukweli tuige nchi zilizoendelea km: USA, CANDA,AUSTRALIA,EUROPE na nyingi hizi nchi hadi hii leo hupokea wageni wengi kila leo (walokuwa wahamiaji haramu au halali) na wote hao wanatosha kutokana na kuwajibika kikazi na kutoa huduma za aina tofauti....! Nchi hizo zinajengeka na kujengwa na watu wa VICHWA mbali mbali na ufumbuzi wenye maarifa katika zsekta nyingi. imedhirika kuwa maendeleo na uchumi Unakuja kwa njia ya mashindano na kuchuana kikazi kati ya wakazi....!
Sisi kama tumeshindwa kujua basi tungoje hadi tutakapoamka au kuzinduka.!!!!
God bless CLEAN HEARTs and OPEN minds.
 
Hapo kuna issue gani wakati serikali inatimiza wajibu wake? au nawe mhamiaji haramu? kama mtu alichukuliwa kwa mahojiano akaonyesha vilelezo kisha akaachiwa kuna ubaya gani? kwanza huyo jamaa si ndiyo yule aliyeleta thread ya kuichafua Tanzania katika sakata la Immigration JNIA Airport?

Kwa hiyo kama ni yeye alileta ile thread, hiyo inahusika vipi na suala lake analoliongelea??
Na who do you think you are kuhoji yeye kuleta hiyo thread?? Au ndio afande kilaza wa airport?
Eti kuidhalilisha Tanzania, nyie wenyewe mamburula huko uhamiaji kazi kula rushwa tu hata hamjui mnachofanya, eti unamtishia.......... !!
 
Kama kawaida Tunafukuza WAO natujue na WETU watafukuzwa !! WaTanzania wengi wapo nchi za nje na nchi jirani wakiendesha maisha yao ya kila siku kama kawaida. Sasa zoezi hili la kutimua uhamiaji haramu linapowakumba Wakenya au waGanda, nk; Basi na wa Tz. wetu hawatasalimika nasi tutafukuzwa hii ndo sheria ya kisiasa zisizo na nidhamu. Tujipangee na kutayarisha kambi za kupokea wananchi wetu kutoka nje !! Hayo nisemayo yasiwashtue lakini Ukweli tuige nchi zilizoendelea km: USA, CANDA,AUSTRALIA,EUROPE na nyingi hizi nchi hadi hii leo hupokea wageni wengi kila leo (walokuwa wahamiaji haramu au halali) na wote hao wanatosha kutokana na kuwajibika kikazi na kutoa huduma za aina tofauti....! Nchi hizo zinajengeka na kujengwa na watu wa VICHWA mbali mbali na ufumbuzi wenye maarifa katika zsekta nyingi. imedhirika kuwa maendeleo na uchumi Unakuja kwa njia ya mashindano na kuchuana kikazi kati ya wakazi....!
Sisi kama tumeshindwa kujua basi tungoje hadi tutakapoamka au kuzinduka.!!!!
God bless CLEAN HEARTs and OPEN minds.

'Wasiwasi wangu ni uwezo na utayari wa kuwapokea. Tuliwafukuza wahamiaji haramu' ktk hali ya ugafura sana:-tulisikia Rwnd wakilalamika kuwa hawakupewa taarifa...lakini wakaonesha mapokezi makubwa na ya kujari.. wakatoa na usafiri wakupeleka watu wao; walipoombwa magari 50 wakatoa mabasi 100..

Wakifukuzwa wakwetu, tutaweza?...rushwa, umaskini, upendeleo wakupeana tenda....refer matukio ya mabomu ya mbagara na mafuriko jangwani....nasubili comment za ' wazalendo' hapa.
 
'Wasiwasi wangu ni uwezo na utayari wa kuwapokea. Tuliwafukuza wahamiaji haramu' ktk hali ya ugafura sana:-tulisikia Rwnd wakilalamika kuwa hawakupewa taarifa...lakini wakaonesha mapokezi makubwa na ya kujari.. wakatoa na usafiri wakupeleka watu wao; walipoombwa magari 50 wakatoa mabasi 100..

Wakifukuzwa wakwetu, tutaweza?...rushwa, umaskini, upendeleo wakupeana tenda....refer matukio ya mabomu ya mbagara na mafuriko jangwani....nasubili comment za ' wazalendo' hapa.
Mkuu Muta', kila heshima juu yako, Ahsante mh. Mwenzangu unaupeo na busara aminika, Hawa wajamaa zetu Sijui niwaite jina gani la myama ( WANYAMA WETU ) hawanaga mpango na hawana UTU na wamefilisika damu na kutokuwa na MOYO wa kibinaadamu !! Na bado sijui niwaeke daraja gani humu duniani!! Hadi sasa ninaomba kwa mungu asituletee jangaa hilo na atuepushe na BALAA la aina yeyote katika nchi hii TANZANIA huwaga nina salii sana kuliombea Taifa letu liwe lenye amani na usalama.... hayo Kwa maana nyingi tunawjua VIONGOZI, WANASIASA na WAHUSIKA na WATETEZI, nk Wa nchi hii walivyo Bila kuambiwa, wawezaona Makovu yetu na Majeraha tulonayo !!
Wakuu naomba tutafakari na Tujipange tujitolee na tuwe tayari katika taathira za aina yeyote .... Malipo tutalipwa na MWenyezzi Mungu.AMIN

Shukraani wapenda UTAIFA na wenye UZALENDO.
 
kwan wazaramo hawawez kuwa wahamiaj haram?.........sion sababu ya kuwafukuza walimu kutoka nje ya nchi maana wanawaelimisha vijana wetu tena wapo na vibali..
Tanzania tunawahitaji sana walimu toka nje lakini wanatakiwa wawepo nchini kisheria, na hawawezi kufukuzwa iwapo wana vibali halali. Ila inawezekana au
-vibali vyao ni vya bandia au
- vilitolewa kwa ajili ya kazi nyingine na siyo kufundisha, kwa mfano waliomba kama anahudumu masuala ya kidini kwenye taasisi ya dini kumbe ni mwalimu kwenye shule binafsi.
wanaofuata sheria na utaritibu hawapaswi kubughudhiwa.
 
Zoezi hili ni zuri lakini jinsi linavyofanyika sivyo kabisa.Watu wanachukuliwa kwa kuhisiwa wahamiaji haramu(sijui haramu kwa nani), wakibainika kuwa siyo wahamiaji haramu wanageuziwa kibao kuwa wanahisiwa kufanya biashara haramu.. Wananchi wananyanyaswa, wanadhalilishwa katika nchi yao na hii inatokea Dar es salaam sijui mikoani itakuwaje.
Inaonekana kama nia ya zoezi ni ukamataji zaidi kuliko kuonyesha vielelezo. Tunapoelekea sipo kabisa..
Usione rahisi kusema mtu anachukuliwa kwa mahojiano lakini maana yake ni nyingine kabisa.Watu wanalala lupango hadi siku mbili ili tu kuonyesha vielelezo wakati wana vielelezo vyote na ni raia halali..
Zoezi ni zuri kama unavyosema lakini palipo na wengi hapakosi dosari na hasa ukizingatia linafanywa na vyombo mchanganyiko lakini mwisho wa yote faida yake ni kubwa kuliko hasara yake.

 
Tatizo watu wame vamia operesheni kichwa kichwa bila kujiandaa,
Ni sawa na daktari kwenda kumfanyia operesheni mgonjwa bila kuandaa visu, taa wala dawa ya usingizi,
Matokeo yake anamweka mgonjwa kwa operating table na kumsafisha halafu anaanza kuhaha
Kwengine ukionyesha kitambulisho cha uraia au passport au hata driving licence tu mchezo kwisha..kama wewe ni permanent resident, raia au haramu itajulikana , lakini hapa sisi loop holes kila pahala, na pesa za vitambulisho vya uraia zimegugunwa na panya
Labda sasa tuweke historians na anthropologists etc pale immigration watusaidie
With high RESPECT mkuu, umeongea kwa hekima na busara " yaonekana Serikali haykulisoma na kulitafakari jambo hili "
kukurupuka kwao kutazaa tija na matokeo yasiyo tatulika... Yaani human DISASTER ! Si ajabu hasara zake ni kubwa kuliko walivyotegemea. Watanzania tupo pamoja na Mungu atusaidie.
 
Hakuna operesheni itakayosifiwa ukiona inasifiwa hamna kitu
 
Back
Top Bottom