Mauaji ya mtoto wangu

Mauaji ya mtoto wangu

Pole sana, nikivivaa viatu vyako hata siwezi, mtoto wangu anaushika moyo wangu kumuua ni sawa na kuniua Mimi, walai nasema haijalishi huko maabusu nitakulipa tu na naweza kwenda mbali zaidi.
Issue yako wapo wasomaji humu ambao wanasimamia mamlaka husika, ungetaja tu majina, pengine ungepata msaada zaidi hata wakurudishiwa hela yako.
Asante sana mkuu, mimi ninahisi endapo wasingekuwa wamemshikilia ingekuwa story nyingine tena, ila ninaamini hata nisipofanya kitu mimi hatobaki salama.
 
Nadhani ni tamaa ya pesa iliwaingia.
Wapo tayari kukaa kwenye jua kali na kichanga cha miezi 6 kuomba omba barabarani ili watu wamhurumie mtoto yeye apate pesa.
Anaona akikaa nae kivulini watu hawatatoa pesa
 
Wapo tayari kukaa kwenye jua kali na kichanga cha miezi 6 kuomba omba barabarani ili watu wamhurumie mtoto yeye apate pesa.
Anaona akikaa nae kivulini watu hawatatoa pesa
Niliwahi sikia hili jambo ila sikulitilia maana.

Ila limedhihirika.
 
Mungu akutie Nguvu, lakini hao upande wa mama mtoto walifanya kosa sana kukunyanyasa kupitia ndugu yao police maana hapakua na kosa la kukupeleka wewe huko lakini Mungu ndio hakimu anae hukumu kwa haki ipo siku yao
 
Pole sana. Mungu akutie nguvu katika wakati huu mgumu ulioao
 
Binadamu ni wanyama wenye roho mbaya kuliko wanyama wote duniani.

Pole sana mkuu.

Mkuu hivi hushawai jiuliza, hizo siraha za nyuklia katengenezewa nani...? ni Bin-Adam, Binadamu huyu huyu anayekuwekea plastic smile halafu behind the scene anakumaliza taratibu taratibu.
 
Pole sana mkuu!
Hakika inasikitisha.roho ya mwanao ipate rehema kwa Mungu apumzike kwa amani.
 
Nadhani ni tamaa ya pesa iliwaingia.

Mkuu pole sana,
Tunajifunza kutokana na makosa, wakati mwingine kuwa makini na mtu wa kumimbisha.

Naamini rangi nyeupe ndiyo iliyokukanganya , lakini "ku-google" ni muhimu sana hasa nyakati hizi za .com

Wanaume tumeumbwa mateso, pambana!!

"Don't involve yourself with something you can't handle"

Shukrani..!
 
Mkuu pole sana,
Tunajifunza kutokana na makosa, wakati mwingine kuwa makini na mtu wa kumimbisha.

Naamini rangi nyeupe ndiyo iliyokukanganya , lakini "ku-google" ni muhimu sana hasa nyakati hizi za .com

Wanaume tumeumbwa mateso, pambana!!

"Don't involve yourself with something you can't handle"

Shukrani..!
Shukrani sana mkuu
 
Nimeumia jamani mtt mdogo hivyo kamkosea nini. Pole sana mkuu Mungu atamuadhibu kadiri ya matendo yake.
 
Nimesoma ujumbe wako umenitoa machozi kwa kweli. Mungu anamipango na wanadamu kweli kila mwanadamu na daraja analopitia. Pole sana broo
 
Kufiwa na mtoto ni maumivu ambayo sipendi kabisa mtu mwingine apitie,nina miaka 2 sasa tokea kijana wangu atangulie ghafla tu ila bado naona kama ni jana tu ni kumbukumbu inayoumiza na ni kipindi pekee ambacho niliwahi kumkufuru Mungu wangu na kumuona si lolote.
Pole sana swahiba ila hakika Mungu ni mfariji hakika ule mlango uliosahau kuufunga ndio faraja yako itatumia kuingia kwako weka imani yako juu Mungu anajua jinsi ya kufariji.
 
Kufiwa na mtoto ni maumivu ambayo sipendi kabisa mtu mwingine apitie,nina miaka 2 sasa tokea kijana wangu atangulie ghafla tu ila bado naona kama ni jana tu ni kumbukumbu inayoumiza na ni kipindi pekee ambacho niliwahi kumkufuru Mungu wangu na kumuona si lolote.
Pole sana swahiba ila hakika Mungu ni mfariji hakika ule mlango uliosahau kuufunga ndio faraja yako itatumia kuingia kwako weka imani yako juu Mungu anajua jinsi ya kufariji.
Amina.
 
Mkuu hivi hushawai jiuliza, hizo siraha za nyuklia katengenezewa nani...? ni Bin-Adam, Binadamu huyu huyu anayekuwekea plastic smile halafu behind the scene anakumaliza taratibu taratibu.


Yani ni hatari sana.
 
Back
Top Bottom