Mauaji ya mtoto wangu

Mauaji ya mtoto wangu

Duuh! Pole sana Mkuu. Kwa kuwa moyo wako umekukataza na kuona kulipiza kisasi ni kumkosea Mungu basi endelea hivyo hivyo.

Ganga yajayo Mkuu kwani kulizungumzia jambo hadharani kiasi hiki ni moja ya kuutua mzigo ambao ulikuwa umeubeba.

Hivyo endelea na maisha mengine pia inabidi uamini ipo siku utapata mtoto mwingine.
Asante sana mkuu nipo najaribu kuganga yajayo japo bado maana hata mwezi haujaisha sasa.
 
Mtoto hana hata mwezi unamgawa ? Utalala usingizi kabisa ?
Wewe unamshangaa kumgawa tu? wakati hata kumuona yenyewe kaja mara mbili tu kwa umri huo wa mwaka na miezi tisa?

Nilikuwa namuambiwa huyo mtoto kiutani kuwa hana mama hapo...japo alikuwa haelewi ninamuambia nini.
 
Tumetofautiana mioyo unaanzaje kumgawa mtoto wa siku 20 yaani siwezi, huyo mama kachangia kifo cha mwanae labda angebaki nae yasingetokea.
Angebaki naye huenda ndio angekufa mapema zaidi.

Umbali aliokuwa anaishi na mtoto alipolelewa ilikuwa kama 10km na kaja mara mbili tu baada ya kumuacha, kwa umri wa mwaka mmoja na miezi tisa.
 
Daah! Kisa kimoja cha kustaajabisha sana. MUNGU akaendelee kuwa upande wako daima Mkuu. Apumzike kwa amani Malaika ktk jina LA YUSU Mnazareth.
Kwa kweli hiki kisa kimekuwa kigumu hata namna ya kusimulia mtu ninashindwa.

Yaani mimi mwenyewe nilikuwa ninaota ndoto.
 
Asee ngoja nitulie aseer

Humu duniani kumbe kuna watu wapo ili matukio yajirudie


Hili tukio kama lilivyo nimelishuhudia miaka ya nyumabkidogo huko mkoani morogoro miaka ya 1989 kama sijakosea mitaa ya msufini asee


Mungu akutie nguvu
Ilikuwa vipi mkuu kuhusu hilo tukio.
 
Dah pole sana mkuu Mungu atakulipia hivi huyo mwanamke mtoto alimzaa kweli yy unawezaje kumwachia baba mtoto mtoto hata mwezi hana na huko alipo alikuwa anaishi kwa raha kabisa au alipewa bure huyo mtoto
Ndio mama wa ajabu kupata kutokea, yaani mimi mpaka kukubali kuchukua huyo mtoto niliona kuwa mwanangu atapata tabu sana, maana hapo pemyewe tu alipokuwa chini ya uangalizi wangu alikuwa amekuja mara mbili tu, kwa umri wa mtoto wa miaka tisa.

Hata kwenye mazishi hakutokea, sijui alikuwa anafanya nini.
 
Ndio mama wa ajabu kupata kutokea, yaani mimi mpaka kukubali kuchukua huyo mtoto niliona kuwa mwanangu atapata tabu sana, maana hapo pemyewe tu alipokuwa chini ya uangalizi wangu alikuwa amekuja mara mbili tu, kwa umri wa mtoto wa miaka tisa.

Hata kwenye mazishi hakutokea, sijui alikuwa anafanya nini.
Hee sasa milioni aliitaka nani na kwa lipi?
 
Ulikamatwa na kuwekwa mahabusu kwa kuvunja sheria ipia? Maana sijaelewa kigezo kilichopelekea polisi wakukamte
Anyway, pole sana mkuu
Nahisi kigezo ni kuwa ndugu wa mzazi mwenzake Wana ndugu askari,
Mbona hiyo ipo sana huku kwetu kitaa
 
Hee sasa milioni aliitaka nani na kwa lipi?
Walitaka wa upande wao wote baba wa binti, mama, shangazi na wengine wengi.

Nafikiri huyo mtoto walikuwa na mpango wa kuniuzia kwa hela, sasa nafikiri amefariki wao la kwao bado likiwa halijatimia.

Sasa wanadai laki nane bado na wanawatumia wale ndugu zao maaskari, kunibana nitoe hiyo pesa, na mimi sina kitu mbona watanirudisha polisi mara nyingine.
 
Walitaka wa upande wao wote baba wa binti, mama, shangazi na wengine wengi.

Nafikiri huyo mtoto walikuwa na mpango wa kuniuzia kwa hela, sasa nafikiri amefariki wao la kwao bado likiwa halijatimia..
Wakuuzie mwanao wakati upo nae? Ni kabila gani Mkuu?
 
Pole sana mkuu, haya maisha kuna watu wanapitia magumu kiasi magumu unayo pitia ukajiona mwenyewe una afadhali.. Pole sana
Kuna muda unakuaga na busara zako mwenyewe.... lol.
 
Wanaijua milioni?
Yaani ni hivi, nadhan waliona kwangu ni nafasi ya wao kupata hela kupitia mimi, maana mtoto alivokuwa kule kwa hizo wiki tatu nilishatuma si chini ya laki mbili.
 
Yaan hiyo milioni moja ni kama fidia ya kumzalisha mtoto wao, hiyo laki mbili inatosha wasijitie bangi hapa....

Pole sana, kua na ujasiri umalize masomo salama na utapata mke mzuri na watoto wengi.
 
Duuh! Pole sana Mkuu. Kwa kuwa moyo wako umekukataza na kuona kulipiza kisasi ni kumkosea Mungu basi endelea hivyo hivyo.

Ganga yajayo Mkuu kwani kulizungumzia jambo hadharani kiasi hiki ni moja ya kuutua mzigo ambao ulikuwa umeubeba.

Hivyo endelea na maisha mengine pia inabidi uamini ipo siku utapata mtoto mwingine.
Miss you my dada...
 
Back
Top Bottom