Ukiona wanaenda basi hujue mafuta yanawasaidia,wasipoenda basi hujue mafuta hayawasaidii mambo yao.
Kwaiyo kitu ambacho hakina faida kwako basi jua kina faida kwa wengine!
Mimi binafsi nishayatumia Maji na Mafuta ya Mwamposa kwa kumwaga ndani ya nyumba niliyokuwa nimepanga,aisee kuna vitu vya ajabu niliviona ndani ya ile nyumba;kuanzia mlangoni ninapoingilia,nilikuta dawa imefungwa na imewekwa kwenye fremu ya geti na ndani kwangu chini ya uvungu kuna Nng'e amekufa!siku zote nilikuwa sivioni ila baada ya kumwaga mafuta na maji niliviona.
Tangu nimeishi Ile nyumba kila pesa ninayoshika sioni imefanya kitu gani,baada ya kuhama ile nyumba leo namiliki mashamba na viwanja kibao.
Sikatai wapo Wahuni lakini mimi binafsi nimesaidiwa na Mafuta ya Mwamposa tena Wala sikuenda Dar es salaam,Mimi naishi Mwanza.Alipokuwa anaomba kwenye TV yake akasema chukua Maji na Mafuta na uelekeze kwenye TV,na nilifanya hivyo na leo mambo yangu yapo safi.
Kwaiyo kejeli siyo nzuri,mtu anamponda Mwamposa alafu kesho anaamkia kwa Waganga kuroga,sasa uyo mtu yeye ana usafi gani!!