Wadau nimerudi tena baada ya kimya kirefu kiasi..
Hili limenitokea naombeni maoni yenu.
Baada ya pilikapilika za shughuli Juzi,nkajilaza na nikaamka mida ya saa sita usiku kuupigia simu ubavu wangu wa pili.
Tukaongea vizuri tu,lakini ghafla nkaambiwa subiri,simu ikakatwa. Nikapiga tena,simu yake iko bize,tena na tena naambiwa waiting hatimaye nkachoka. Nkatuma msg ifuatayo.
"si umeamua kutupanga,na katika list mi sina umuhimu,usintafute tena"
Kisha nkazima simu. Asubuhi nkakuta msg amejibu hivi;
"kama unahisi nimewapanga poa hamna shida ila nlikua naongea na mtu kuhusu mchongo wa ajira"
Kiukweli sijajibu kwa sababu zifuatazo.
1.mchongo wa kazi wanajadili usiku wote huo?
2 na si mara ya kwanza kitu km hicho kutokea na nlishamkanya awe na mipaka ya kuongea na watu baki usiku
Basi sijajibu msg ile mpk sasa.Na kila akipiga sipokei. Leo kanitumia msg hii hapa.
"kuchuniwa raha we acha tu,ukipiga simu haipokelewi,text hazijibiwi,mbona watu watakoma mwaka huu?"
Sijajibu msg hii.Na mpk sasa namwona mzushi ananicheat. Je wewe unaonaje? Ungekua ww ungefanyaje?
Pole sana braza, kwa kifupi huyo mwenza wakao hana
nidhamu na mapenzi ya dhati kwako hawezi kukujibu majibu
kama hayo. kama unamoyo mpana unaweza kuendelea naye
lakini kama moyo wako hauna tundu,tulia kwanza na ufanye
shughuli za maendeleo. Then uombe Mungu atakuonyesha njia.