Niliwahi kuwa na mahusiano ya muda mfupi na binti mmoja hivi yapata mwaka sasa umepita. Na tangu wakati huo tumekuwa na mawasiliano ya mbali sana yaani tunaweza kuwasiliana mara moja baada ya miezi kadhaa, sasa jana ilikuwa moja ya siku hizo na ndipo stori inapoanzia,
Nilipokea simu mchana kutoka kwa huyu binti akidai alitaka kunipa hi tu, tukaongea kidogo na nikaahidi kwamba nikipata nafasi nitamtembelea siku moja. Usiku nikiwa tayari nimeshalala nikapokea simu tena kutoka kwa huyu binti na akaniuliza kama nilikuwa nimeshalala nikamjibu ndio akanitakia usiku mwema akakata simu.
Baada ya muda nikapokea tena simu ikitokea kwenye namba ya huyo binti tena ila nikaamka nikaipokea ila sasa sauti ikatoka ya kiume, sauti hiyo ikaniuliza kama nilikuwa namfahamu huyo binti (ikitaja jina lake) nikamjibu ndio akaniuliza ni nani kwangu nikamjibu huo ulikuwa usiku mwingi sana na sikuwa kwenye mood ya kujibu maswali ya aina hiyo, nikakata simu.
Baada ya dakika kadhaa simu yangu nyingine ikaita tena na nilipopokea nikakuta ni yule yule bwana na ananiuliza maswali yaleyale, Ah i got mad...........................................................