Regia Mtema
R I P
- Nov 21, 2009
- 2,970
- 864
- Thread starter
-
- #81
Kuna lile la kumteua mtu kuwa mkuu wa wilaya wakati ana kesi ya jinai mahakamani. Kama sikosei huyu alikuwa mbunge wa zamani wa Biharamulo. Uteuzi ulisitishwa baadae wakati anakwenda kuripoti.
Hotuba yake kwa ajili y a kujibu wafanyakazi akieleza mgomo ni Fake kisheria; yeye ni hakimu au mahakama; au yuko juu ya sheria; au ndio double standards; anatishia watu kuwapiga na virungu au hata anaweza kumaanisha kuua kwa ajili ya kudai haki zao; mie naona kajidhalilisha kabisa hapa kuliko mahala pengine popopte tena iingizwe na kuwa 10 maana hii ina nguvu sana
2. Kujiuzulu kwa Waziri Mkuu-Edward Lowassa
Kwa kuwa Waziri Mkuu anateuliwa na Rais tena wakati mwingine bila kushauriana na mtu kitendo cha Lowassa kulazimika kujiuzulu baada ya kashfa ya Richmond ilikuwa ni pigo jingine kwa Rais. Hii inamaanisha kuwa Rais wetu hayuko makini katika teuzi zake ndio maana anateua watu ambao sio viongozi wasafi wasio na dhamira ya dhati ya kuongoza taifa hili. Hii ni aibu nyingine kwa Rais kwani mtendaji wake mkuu aliyempenda kuliko Mawaziri wote kumuangusha kwa utendaji wake mbovu hivyo kulazimisha kuvunjwa kwa baraza la Mawaziri na kumteua mtu mwigine ambaye hakuwahi kumfikiria kuwa Waziri Mkuu
HII MBONA iko vice versa? siyo kuwa JK alipata heshima sana nje ya nchi kuwa na waziri mkuu anayekubali kuwajibika?
Pili je Kudhalilika huko huko utawapa kila rais dunia hii? watu wanabadilika sana, na Rais kamwe hayuko kuwa kama Mola wa kuweza kujua yajayo.
Then Nyerere alidhalilika Mwinyi alipojiuzulu? No sitaki kuikubali sana hii point labda ungeandika kivingine
...du hii ya arusha ..wengine tulikuwa hatujaipata na mkutanoni tulikuwepo full time....tumtendee haki muungwana kwa kumpa tuhuma za kweli....ie...kushambuliwa mwanza,kuanguka jangwani,kuzidiwa mwanza ...etc....hii ya arusha inaweza kuwa kweli lakini haina ushahidi....kama inavyosadikika pia kuwa huzidiwa mara kwa mara ....inakuwa haina ushahidi....
Mkuu hivyo ndivyo ilivyo kujiuzulu hua kunamuondolea heshma fulani mteuzi kama huna khabari ndio maana wakati mwingine mteuzi huwa anakataa maombi ya kujiuzulu ili asipatwe na aibu hiyo. Hivi kama JK angekubali maombi yote ya waliotaka kujiuzulu leo hii wangekua wamemuabisha wangapi? Kujiuzulu humaanisha mtu aliyeteuliwa si sahihi na alikubali uteuzi akijua kua yeye si sahihi lakini baada ya kuvurunda na kuonyesha kuwa haku-fit ktk uteuzi wake ndo anajiuzulu sasa mpaka hapo anayeumbuka nani? MKUU KUJIUZULU NI AIBU KWA MTEUZI SIKU ZOTE. Hata raisi akijiuzulu ni aibu kwa wapiga kura wake.
Alishawahi kusema eti hadi leo hii hajui kwnini Tanzania ni maskini kiasi hicho, shame on him!
Inasikitisha!, I know he has to make some tough decisions on his own but, he has advisors who could've done or say something to prevent some michemsho. This's ridiculous, and uzembe usio na akili.
Nakubaliana na wewe.Uko sahihi kabisa na haya ndio mdhara ya neportism,huharibu kabisa utendaji kazi.Neportism ilikuwa na mojawapo ya sababu za kufa kwa viwanda vyetu vingi kipindi cha Nyerere na Mwinyi.Kama uteuzi wenyewe anaufanya zaidi kwa misingi ya ushemeji, ujomba, uwifi, ukwe, na family friends wategemea kuna kuwajibishana kokote kwa dhahiri kutaja tokea kweli hapo?
Bila kusahau akamteua shahidi wa serikali na mkuu wa kitengo cha EPA kuwa Mkuu wa TIB! Akifikiri watanzania hawajui 1 + 1 = 2. Ndo huyu ataleta agricultural revolution? tuache utani!!11. Aliingilia shughuli ya Bunge, hivyo kuvunja Katiba aliyoapa kuilinda na kuitetea kwa kupanga matumizi ya fedha za EPA zilizorudishwa na wezi kwamba eti zingeelekezwa kwenye KILIMO kupitia Benki ya Raslimali (TIB)!
12. Aliagiza watoto wenye mimba na waliojifungua warudishwe shuleni huku akijua kwamba Sheria ya Elimu (The Education Act, 1978) hairuhusu wanafunzi wa aina hiyo kuwepo shuleni!
13. Aliagiza kwamba aliyekuwa Rais Mstaafu Benjamin W. Mkapa "aachwe apumzike" huku akijua kwamba alikuwa na tuhuma za kifisadi dhidi yake!
Bila kusahau akamteua shahidi wa serikali na mkuu wa kitengo cha EPA kuwa Mkuu wa TIB! Akifikiri watanzania hawajui 1 + 1 = 2. Ndo huyu ataleta agricultural revolution? tuache utani!!
Kusaini mkataba wa Afrika Mashariki kunapiku matukio yote ya kumdhalilisha Rais Kikwete, kwani anasaini kujiondolea mamlaka yake mwenyewe. Inasemekana Nyerere alitumia mbinu kumsainisha Karume mikataba ya muungano, kwa kumwachia Karume mkubwa misafara na jina la Urais ili ajione bado ni mtawala, na kwamba, Muungano 'utaishia Chumbe', kwa kile kinachosemekana kwamba Nyerere alikuwa mwerevu kumzidi Karume. Leo miaka hamsini baadaye, Kikwete anasaini mikataba ya kumnyang'anya madaraka yeye mwenyewe, na haoni tatizo, kwa kile kinachoonekana ni mbinu ileile ya zamani ya kumuachia aendelee na misafara na kutandikiwa mazulia mekundu, mpaka pale atakapobaini kwamba amebaki rais jina (hata Tenga ni rais wa TFF) bila madaraka ('power is nothing without control' -- tangazo).
Naona matukio yanazidi kuongezeka.