Matokeo yangu yamekosewa NACTE, nimehangaika sijapata msaada

UZZIMMA

JF-Expert Member
Nov 20, 2014
406
456
Habari yenu katika ujenzi wa maisha yenu. Nimehitimu chuo 2020 stashahada ya uhandisi majengo katika chuo fulani cha serikali hapa nchini.

Tatizo kubwa matokeo yangu yamekosewa katika mfumo wa NACTE na hii imekuwa ni kikwazo nisiweze kuendelea na masomo.

JITIHADA NILIZOZIFANYA KWA SUALA HILO
Baada ya kuthibitisha matokeo yangu yamekosewa NACTE mimi nikafwata uongozo wa chuo upande wa academic. Nikaambiwa niandike barua ya maombi yangu.

Baada ya kuandika barua nikakaa kama mwezi mmoja nikaenda chuo kusikilizia ombi langu. Nikaambiwa chuo kimeandika barua NACTE kuhusu swala langu. Nikasubiri kama miezi mitatu huku nikiulizia chuoni kama barua ilioandikwa kwenda NACTE imejibiwa.

Kiukweli siku zote nilizowasiliana na chuo changu nikaambiwa barua haijajibiwa.

Nikaamua kwenda kwenye ofisi za NACTE kusikilizia swala langu. Baada ya kwenda nilienda na matokeo yaliomo kwenye ststem halisi ya chuo.

Majibu nikaambiwa NACTE hawajapokea barua yoyote inayohusu madai yangu kutoka chuoni.

Na ili nisaidiwe ni lazima CHUO HUSIKA ndio watume barua.

Baada ya kurudi chuo tena kueleza yaliojiri NACTE chuo kinadai kimetuma barua NACTE, ila kwa kuwa haijashughulikiwa watatuma barua nyengine.

Imepita takeiban miezi minne tangu niende chuoni kufwatilia madai yangu kwa mara ya mwisho, leo hii nimeongea nao wakanimbia barua ya pili wameshaituma NACTE ila majibu hawajapata.

Jamani naombeni msaada tafadhali niipate haki yangu. Bado sijakata tamaa kutafuta haki yangu.

Ni mimi binadamu mwenye uchungu wa elimu.
 
Aisee nenda mwenyewe nacte. Hizi mambo za vyuo wameandika barua si za kuamini sana
 
Bro Pole sana kwa Hilo ila Kuna Jambo moja umeshindwa kulitekeleza , tusikatae uhalisia wa nchi yetu siku zote mkono mtupu haulambwi ko jitathmin tafta kitu nenda Baraza kabsa then ongea na mmja wa watendaji wa Baraza pale inawezekana chuo kinatuma barua ndio sema siku zote pesa kwanza
 
Matokeo yako hayakukosewa, wewe ni mchemkaji.

Jina la baraza la mitihani ni NATIONAL EXAMINATION COUNCIL OF TANZANIA

NECTA
nchi ngumu sana hii hapo kajiona yeye ndo yeye anajua taasisi za elimu kuliko mhusika mwenyew hahahaha hii comments ni ya form four leaver nadhan
 
Mkuu hapo jitahidi kuongeza ufatiliaji, usiruhusu kukaa muda mrefu bila kuwasumbua. Wakikwambia mwezi we baada ya wiki rudi uliza maendeleo. Wasumbue hadi wakikuona wakuzoee. Jitahidi pia mkono ukue mrefu.

Ila taasisi za kiserikali bado zinaishi kwenye zama za kuandika barua na kupitia barua kwa ajili ya kujibu. Wakati dunia imeshaamia digital unatuma email with hours au ndani ya mida mfupi unapata majibu

Wabadirike
 
Nilimaliza Chuo Mwaka 2020 Kada ya Afya. Mwaka 2022 Aprili Nikaomba maombi ya Transcript na Niliomba Niippokelee Mwanza ambapo ni Jirani. Cha ajabu nikaambiwa kuwa Nitaikuta Mwanza. Nimeenda Ofisi ya Mwanza Wakaniambia kuwa haipo. Nikaenda Dodoma wakaniambia haipo. Nikaenda Ofisi za Dar Wakaniambia haipo ipo Mwanza. Nimerudi Mwanza Wakaniambia Haipo.



Hii ni zaidi ya Mwaka mzima nasubiri Watu wa Ofisi ya Mwanza wanipigie simu sijapata Msaada.



Je Kwanini NACTE wanaweka urasimu wa mtu kumpatia Cheti Cha transcripts. Kwanini Kama Cheti unapata Chuoni Kwanini vyeti visitumwe Chuoni.

Mpaka Sasa Sina msaada wowote na gharama za kutoka Mkoa kwenda Mkoa kufuatilia Transcripts imekuwa changamoto. Kama Kuna mtu ana msaada wa mawasiliano ya Moja Kwa moja anisaidie Ndugu zangu
 
Back
Top Bottom