Matokeo ya Physics kitaifa sio mazuri,kwa nini?

Matokeo ya Physics kitaifa sio mazuri,kwa nini?

Mnyakatari

JF-Expert Member
Joined
Oct 25, 2010
Posts
2,111
Reaction score
1,920
Nimejaribu kupitia shule zilivyofanya vizuri sijaona A wala B za Physics!Hata aliyeongoza ni PCM mwenye A in Chemistry and Math na C ya Physics.Kumetokea nini kwenye hili somo wakuu?Mtihani ulikuwa mgumu?Walimu hawakuwaandaa vizuri wanafunzi?Wanafunzi hawakujiandaa vizuri?Format haikufuatwa in paper 1 and 2?Tatizo ni nini?Naomba tujadili wadau wa physics
 
Na ukilinganisha na masomo mengine ya sayansi,Physics ina F nyingi kuliko mengine!
 
na wanadai mtu wa kwanza kitaifa physics ana 64 hii yaani ni pamoja na paper 1,2 and 3.
 
mhu inankumbusha mbali sana ni kama ile physics ya 2007.ingawa nlimaliza 2012 ila ile paper yao naiheshimu mpaka leo.
 
Matokeo yafutwe ifanyike standardisation ili yapatikane matokeo mazuri hakuna ujanja, subiri Tume iundwe huo ndiyo muarobaini
 
Jibu ni rahisi sana. Hakuna walimu competent kwa masomo yote ya sayansi sio Pysics tu. mbona Hesabu, Chemistry na Biology hujaziangalia kwa makini?
Wengi wanaofanya vizuri masomo haya tunawapeleka Engineering na wale wa Division 3 na 4 ndio wanatengeneza vilaza kama wao.
Hata shule za msingi shida hiyo hiyo. Usitegemee muujiza mkuu. Mwakani zero zitaongezeka zaidi labda washushe zaidi alama za ufaulu.
 
Jibu ni rahisi sana. Hakuna walimu competent kwa masomo yote ya sayansi sio Pysics tu. mbona Hesabu, Chemistry na Biology hujaziangalia kwa makini?
Wengi wanaofanya vizuri masomo haya tunawapeleka Engineering na wale wa Division 3 na 4 ndio wanatengeneza vilaza kama wao.
Hata shule za msingi shida hiyo hiyo. Usitegemee muujiza mkuu. Mwakani zero zitaongezeka zaidi labda washushe zaidi alama za ufaulu.

Inawezekana unayosema ni kweli mkuu.Nimeangalia physics kwa sababu nimeona labda kuna kitu kingine zaidi ya huo "usayansi" na huo "ukilaza" wa walimu unaouzungumzia.Nimeona sio kawaida kwa somo hili kutotoa A wala B taifa zima!Chemistry na Biology ni kweli sio mazuri kama mengine ya arts lakini angalau zipo A's na B's kadhaa.Na hao incompetent teachers ndo haohao hata kwenye Chemistry na Biology wanapatikana.Unafikiri hakuwezi kuwa na tatizo zaidi ya hilo kwenye matokeo ya physics kwa mwaka huu mkuu?
 
Nimejaribu kupitia shule zilivyofanya vizuri sijaona A wala B za Physics!Hata aliyeongoza ni PCM mwenye A in Chemistry and Math na C ya Physics.Kumetokea nini kwenye hili somo wakuu?Mtihani ulikuwa mgumu?Walimu hawakuwaandaa vizuri wanafunzi?Wanafunzi hawakujiandaa vizuri?Format haikufuatwa in paper 1 and 2?Tatizo ni nini?Naomba tujadili wadau wa physics

Na ukitaka kuelewa ukubwa wa tatizo lilipo sasa ni kwamba kama ulikuwa haufahamu Degree ya Physics imefutwa UDSM, kwa maana nyingine TZ huwezi kusomea Physics!
Nchi ya watu milioni 40 hakuna Degree ya Physics!

Habari ndio hiyo!

 
Kusema kweli,ile paper ya physics haikuwa ngumu kiviiile na wengi walitegemea mabanda isitoshe paper 2 na 3 zilikuwa nyanya.Kwa upande wangu siyaamini matokeo ya physics kabisaa.Anyway,tatizo ni ukosefu wa walimu competent na vitabu maalum havieleweki(mara chand,mara nelkon,mara roger,mara UP,mara tom duncan)kitabu special kilicho kwenye system hakifahamiki kiasi kwamba unasoma kwa kutapatapa kama mfa maji.
 
Na ukitaka kuelewa ukubwa wa tatizo lilipo sasa ni kwamba kama ulikuwa haufahamu Degree ya Physics imefutwa UDSM, kwa maana nyingine TZ huwezi kusomea Physics!
Nchi ya watu milioni 40 hakuna Degree ya Physics!

Habari ndio hiyo!


Sina uhakika na kufutwa kwa Bsc Physics Udsm kama ndivyo unavyomaanisha kwa "degree ya physics".Lakini pia walimu wa physics sio hao wa degree ya physics ila ni watu wa Bsc Ed na Bed science ambazo zipo karibia kila chuo.Vilevile Tanzania bado kuna degree ya physics,i know for sure ipo Udom,kuna mdogo wangu yupo mwakatwa 3 anasoma Bsc Physics pale.Au cjakuelewa Kijakazi?
 
Last edited by a moderator:
Kusema kweli,ile paper ya physics haikuwa ngumu kiviiile na wengi walitegemea mabanda isitoshe paper 2 na 3 zilikuwa nyanya.Kwa upande wangu siyaamini matokeo ya physics kabisaa.Anyway,tatizo ni ukosefu wa walimu competent na vitabu maalum havieleweki(mara chand,mara nelkon,mara roger,mara UP,mara tom duncan)kitabu special kilicho kwenye system hakifahamiki kiasi kwamba unasoma kwa kutapatapa kama mfa maji.

Naungana na wewe kuyashangaa matokeo na kujiuliza zaidi kunani.

Lakini pia mkuu hudhani kama hizo sababu za incompetent teachers na mkanganyiko wa vitabu zimekuwepo miaka yote na bado hatujawahi kushuhudia ukosefu wa hizi A's na B's kwa miaka 10 nyuma?
 
Sina uhakika na kufutwa kwa Bsc Physics Udsm kama ndivyo unavyomaanisha kwa "degree ya physics".Lakini pia walimu wa physics sio hao wa degree ya physics ila ni watu wa Bsc Ed na Bed science ambazo zipo karibia kila chuo.Vilevile Tanzania bado kuna degree ya physics,i know for sure ipo Udom,kuna mdogo wangu yupo mwakatwa 3 anasoma Bsc Physics pale.Au cjakuelewa Kijakazi?

Ukweli ni kwamba degree ya physics imefutwa UDSM, kwa kifupi huwezi kusomea Bsc/ Msc Tanzania, hiyo ya Dodoma ni kwenye Education hivyo muulize Mdogo wako vizuri na atakwambia, siku zote Tz nzima UDSM peke yake ndio walikuwa wanatoa Degree (Bsc) Fizikia, na kwa kuwa sasa na hicho kidogo kilichokuwa kimebakia wamekiondoa pia ina maana TZ nzima huwezi kusoma Bsc ya Physics huo ndio ukweli!

 
Ukweli ni kwamba degree ya physics imefutwa UDSM, kwa kifupi huwezi kusomea Bsc/ Msc Tanzania, hiyo ya Dodoma ni kwenye Education hivyo muulize Mdogo wako vizuri na atakwambia, siku zote Tz nzima UDSM peke yake ndio walikuwa wanatoa Degree (Bsc) Fizikia, na kwa kuwa sasa na hicho kidogo kilichokuwa kimebakia wamekiondoa pia ina maana TZ nzima huwezi kusoma Bsc ya Physics huo ndio ukweli!


Najua ninachosema mkuu.Tayari kuna watu wamemaliza Bsc Physics udom,na bado kuna wengine wanasoma(mdogo wangu anasoma Bsc Physics mwaka wa 3 sasa) .

Hata hivyo mkuu,kukosekana kwa degree ya physics Tanzania(ingawa ipo) kunaathiri vp matokeo ya physics A level na hata kukosekana kwa single A or B?
 
Najua ninachosema mkuu.Tayari kuna watu wamemaliza Bsc Physics udom,na bado kuna wengine wanasoma(mdogo wangu anasoma Bsc Physics mwaka wa 3 sasa) .

Hata hivyo mkuu,kukosekana kwa degree ya physics Tanzania(ingawa ipo) kunaathiri vp matokeo ya physics A level na hata kukosekana kwa single A or B?

Nakwambia muulize mdogo wako vizuri Udom hakuna Bsc Physics (pure) kama ilivyokuwa UDSM, ipo wanayoiita ya physics ni Bsc Physics Education!

Swali la pili ni gumu kwangu kulijibu, kama unaona hakuna uhusiano na kutokuwepo kwa Degree ya Physics na ufaulu wa wanafunzi, basi tuishie hapo!
 
Nakwambia muulize mdogo wako vizuri Udom hakuna Bsc Physics (pure) kama ilivyokuwa UDSM, ipo wanayoiita ya physics ni Bsc Physics Education!

Swali la pili ni gumu kwangu kulijibu, kama unaona hakuna uhusiano na kutokuwepo kwa Degree ya Physics na ufaulu wa wanafunzi, basi tuishie hapo!

Hapana tusiishie hapo mkuu Kijakazi.Hilo la kwanza nitakuthibitishia nikiwa kwenye PC unaonekana hakuna maneno yoyote utakayoamini zaidi ya evidence.

Kwenye la pili jaribu kunielewa concern yangu.Tunazungumzia matokeo yasiyo ya kawaida kwenye somo la physics A Level.Wewe umegusia kitu kinachoitwa degree ya physics.Naomba unipe correlation ya hivyo vitu viwili kwa muono wako Kijakazi
 
Last edited by a moderator:
Kusema kweli,ile paper ya physics haikuwa ngumu kiviiile na wengi walitegemea mabanda isitoshe paper 2 na 3 zilikuwa nyanya.Kwa upande wangu siyaamini matokeo ya physics kabisaa.Anyway,tatizo ni ukosefu wa walimu competent na vitabu maalum havieleweki(mara chand,mara nelkon,mara roger,mara UP,mara tom duncan)kitabu special kilicho kwenye system hakifahamiki kiasi kwamba unasoma kwa kutapatapa kama mfa maji.

O level ulisoma wapi? seminar au wap?
 
Ukweli ni kwamba degree ya physics imefutwa UDSM, kwa kifupi huwezi kusomea Bsc/ Msc Tanzania, hiyo ya Dodoma ni kwenye Education hivyo muulize Mdogo wako vizuri na atakwambia, siku zote Tz nzima UDSM peke yake ndio walikuwa wanatoa Degree (Bsc) Fizikia, na kwa kuwa sasa na hicho kidogo kilichokuwa kimebakia wamekiondoa pia ina maana TZ nzima huwezi kusoma Bsc ya Physics huo ndio ukweli!


siyo kweli UDSM kuna MSc(Physics), unakaribishwa kusoma mitaa hiyo, na pia chuo kikiuu cha DSM na matawi yake kama CHANG`OMBE(DUCE) na MKWAWA(MUCE) wanaofa BSc(Ed) na Bed(Sc) ambazo zote unaweza kusoma somo la PHYSICS kwa ufasaha zaidi, kufeli kwa wanafunzi ni kawaida kwa Taifa hili kwa sasa kwa masomo yote.
 
Back
Top Bottom