Matokeo ya Maalim Seif Kumtambua Karume

Mwanzo mzuri.Labda Tanganyika yetu na sisi itarudi.Wacha tuje tukabane makoo wenyewe kwa wenyewe!

Mimi ndo nach subiri.....wazenji wametuchosha. Tukiwa na Tanganyika yetu huenda tutaweza badili mambo na kwatimua akina khatibu.
 
Mkuu unaamini CCM ni wa kweli? mara ngapi wameenda kinyume na makubaliano na muafaka? Kimebadilika nini sasa?

Changa la macho!
Wokovu umeingia kwenye nyumba ya Masatu. Leo hata wewe unafunua true colors za li chama lako? Kumbe wenda wazimu wako huwa wa muda.

Naamini CCM si wakweli...mkutano wa Seif na Karume...mbali na kuwa ni presha za wafadhili lakini ni hitaji la Wazanzibari...mara hii wamekubali kuwa watahukumu wenyewe.Kwa kuwa weshachoka na shida za maisha zinazosababishwa na misuguano ya kisiasa isiyokwisha...wakati wenzetu huko wanatafunana.

Siasa za Zanzibar zinamazonge mengi ndg kila nafasi lazima ipewe advantage,hatubahatishi, na tunajuwa kilichotokea kaitka muwafaka 1&2,lakini hatuwezi kusema kuwa kwa matokeo hayo yote,tusiipe nafasi hatua hii kwa maendeleo ya demokrasia
Wewe unacheza sikilizeni ushauri wa architect wa mbinu chafu za CCM personal secretary wa RA by the name Masatu.
Wakati wewe unakuja hapa na propaganda zako tazama kilichotokea huko kwenye mkutano: http://www.dailynews.co.tz/home/?n=5175&cat=home
 
wanachojaribu kupanga Zanzibar ni cha hatari sana; ni jaribio kubwa zaidi la maamuzi ya Kikwete kama kiongozi. Baada ya Kikwete kushindwa kuleta muafaka Wazanzibar wameamua kufanya wenyewe kwa namna yao; matokeo yake wameamua kumfanya Kikwete kuwa irrelevant which he truly is.
 
Insha-Allah kheri tunayo omba kila siku kwa Mola wetu lakini wasiwasi wangu jee hawa CCM na SMZ ni wa kweli? Isiwe yale yaleeeee ya kina Makamba changa la macho!!!!!! kwa msemo mwengine kuchezwa shere!!!!!

Kwa kweli vita c vizuri tukiangalia sote ni ndugu
 
Insha-Allah kheri tunayo omba kila siku kwa Mola wetu lakini wasiwasi wangu jee hawa CCM na SMZ ni wa kweli? Isiwe yale yaleeeee ya kina Makamba changa la macho!!!!!! kwa msemo mwengine kuchezwa shere!!!!!

Kwa kweli vita c vizuri tukiangalia sote ni ndugu

Bi Fatma; sijui ni kwa kiasi gani Karume ameamua kujipanga na CUF.. lakini vyovyote vile ilivyo kupatana kwao kutamuondolea JK ujiko wa aina yoyote. Hawezi kusema "tulitafuta muafaka tukapata"! Kwani juhudi zake ziliharibiwa na kina Makamba na wenzake.

Kama kilichofanyika ni cha dhati basi Wazanzibari kweli wamefungua ukurasa mpya. Lakini sijasoma manung'uniko ya CUF kama yameshughulikiwa ila ninachoweza kusema ni kuwa sasa Wazanzibar watadai nafasi yao katika Muungano kwa sauti moja na kimsingi CUF wamempa nguvu Karume kwani itakapotokea a showdown kati ya Bara na Muungano, Zanzibar will be unified under one leader... JK ataiachilia Zanzibar.
 
Bi Fatma; sijui ni kwa kiasi gani Karume ameamua kujipanga na CUF.. lakini vyovyote vile ilivyo kupatana kwao kutamuondolea JK ujiko wa aina yoyote. Hawezi kusema "tulitafuta muafaka tukapata"! Kwani juhudi zake ziliharibiwa na kina Makamba na wenzake.

Kama kilichofanyika ni cha dhati basi Wazanzibari kweli wamefungua ukurasa mpya. Lakini sijasoma manung'uniko ya CUF kama yameshughulikiwa ila ninachoweza kusema ni kuwa sasa Wazanzibar watadai nafasi yao katika Muungano kwa sauti moja na kimsingi CUF wamempa nguvu Karume kwani itakapotokea a showdown kati ya Bara na Muungano, Zanzibar will be unified under one leader... JK ataiachilia Zanzibar.

Kama kweli JK ataiachia zanzibar iondoke ktk muungano anatuletea hatari kubwa. islamic extremists watatusumbua kwa kuwa tumeisha ona mfano wa yule mzenji aliyekuwa member wa al qaeda.

Nadhani kinacho takiwa ni ku-renegotiate terms za muungano ila la kusisitiza hata kwa UN ni security conerns, lazima zanzibar hata wakijitenga wasiwe na jeshi.
 
If you cant beat them, join them, isije ikawa kama Raila alivyofanya kwa KANU huko Kenya, a political move ambayo watu wengi walimshangaa, lakini baadaye akafanya maajabu.
 
Wewefikiria tuu Maalim karudishiwa Kila kitu cha Serikali wewe Huoni tu kwa Ndani si mwanachama Hai wa CUF ila kwa nje wanachama wa CUF. Je mambo gani yaliojadiliwa au amedanganywa atapea Urais? Maalim kuwa makini utueleze kwa kina au Wana JF watapata maongezi yenu tuyaweke hapa jamvini tuyajadili
 
Huyu Maalim Seif si inasemekana amefanyiwa fujo na baadhi ya wanachama wa CUF mara baada ya kutangaza kuwa CUF imeamua kumtambua Rais Karume "de facto?" Mimi naona bado kuna mambo mengi yaliyojificha nyuma ya pazia, time will tell!
 
Wana CUF need to get rid of Maalimu na kumpa Juna Duni usukani hapo CUF kitakuwa chama vinginevyo kwisha kabisa
 
hili ni time bomb wait 2 explode, na lita explode wakati wa uchaguzi, nahisi hawa jamaa wana unify against bara, maana hapa karibuni wamekuwa wana ichallenge sana bara na kuonyesha wazi wazi wakitetea uzanzibari, sasa subirini muone
 
Wakishajitenga watagundua kuwa hakuna watu wanaoitwa Wazanzibari! Watakuta kuna Wazanzibari na Wazanzibara, Wapemba na Waunguja! Dhambi ya ubaguzi itaendelea kuwatafuna na inastahili iwatafune hasa! Historia ndivyo ilivyo!
 
Mkuu FMES,
Katiba ya Zanzibar inamtaka rais wa ZnZ ateue angalau wawakilishi wawili kwenye toka CUF kwenye ZEK na Barazani baada ya majadiliano na uongozi wa CUF.
Baada ya uchaguzi 2005, CUF ikapeleka majina yake 4 kwa Karume ili achague mawili ya barazani. Karume akawaita CUF wajadiliane majina yapi, CUF wakakataa kwa kushikilia msimamo hawamtambua Karume.

Karume nae ni jeuri, kiburi, ukijumlisha na whisky kichwani, akagoma katakata kuteua. Just stalmate. Huku wawakilishi wa CUF wakiiingia barazani kushiriki vikao mpaka kuipongeza serikali ya Zanzibar kuwa ni De-Facto (serikali ya kinyume na sheria) na sio De-jure (Serikali kwa mujibu wa Sheria).

Hili tangazo la leo ndilo la kwanza la CUF kuithibitisha serikali ya Karume kuwa ni De-jure. Hivyo kauli ya jino kwa jino imefutika rasmi pamoja na zile kelele zao zote za kupokwa tonge mdomoni, yaani CUF wamekubali walishindwa na mshindi ni Karume, hivyo uhasama wote kwisha.

Mambo yangu yakiwa mazuri, next week natinga ZnZ, Pemba specifically kupima upepo wa impact ya utambuzi huu, na insha-allah nitawaletea nitakayo yashuhudia.

Mkuu nitakuwepo huko weekend ya kabla ya Xmas kupima upepo na nafasi yoyote itakayojitokeza baada ya muafaka huu.

Ma opportunists tupo kibao.
 
wanachojaribu kupanga Zanzibar ni cha hatari sana; ni jaribio kubwa zaidi la maamuzi ya Kikwete kama kiongozi. Baada ya Kikwete kushindwa kuleta muafaka Wazanzibar wameamua kufanya wenyewe kwa namna yao; matokeo yake wameamua kumfanya Kikwete kuwa irrelevant which he truly is.


Wewe nawe???? LOL.

Kilichopo hapo ni umoja wa wa Zanzibar kisha kuanza kudai Currency yao (Mafuta etc) na muungano kuanza kumeguka.

Believe me something fishy is behind this move.

Mie wa Mbagala sina tatizo na hili, nataka kwenda kuangalia namna ya ku exploit opportunities that might arise ...
 
Seif ni mwanasiasa mwadilifu kuliko wanasiasa wote ambao nimewahi kuwajua Tanzania. Maalim Seif, mara zote anaweka mbele utaifa kuliko maslahi yake binafsi. Chochote ambacho watu wanasema kapewa ni stahili zake kama Waziri Kiongozi mstaafu.

Ameandika memoir yake, isomeni mpate maarifa na jinsi ambavyo mwanasiasa anapaswa kuwa mvumilivu. During difficult times, i always see him/ Makweta and learn and learn and grow!

Duni? Zanzibar itawaka moto. Fuatilieni kauli zake za kumwaga damu nk
 
Seif ni mwanasiasa mwadilifu kuliko wanasiasa wote ambao nimewahi kuwajua Tanzania. Maalim Seif, mara zote anaweka mbele utaifa kuliko maslahi yake binafsi. Chochote ambacho watu wanasema kapewa ni stahili zake kama Waziri Kiongozi mstaafu.

Ameandika memoir yake, isomeni mpate maarifa na jinsi ambavyo mwanasiasa anapaswa kuwa mvumilivu. During difficult times, i always see him/ Makweta and learn and learn and grow!

Duni? Zanzibar itawaka moto. Fuatilieni kauli zake za kumwaga damu nk


Zitto,

Thats changamoto, nitaitafuta. Ila mie binafsi siamini viongozi wengi wa TZ. Mfano wapinzani kwanini hawaachiani majimbo ya uchaguzi ?, kwanini hawashirikiani? ubinafsi wao unanipa mashaka kaka.

Thats all and Maalim is no exception!
 
Back
Top Bottom