Matokeo ya Jimbo la Bumbuli yana Utata

Matokeo ya Jimbo la Bumbuli yana Utata

Status
Not open for further replies.
Jimbo la Bumbuli matokeo ya Ubunge yanaonesha kuwa waliopiga kura ni watu 20,512 ambapo January Makamba amepata kura 17,805. Lakini cha ajabu kwenye matokeo ya Urais jimbo hilohilo la Bumbuli waliopiga kura ni watu 44,011 ambapo Magufuli anadaiwa kupata kura 35,801.

Sasa jiulize imekuaje waliopiga kura za mbunge wawe watu 20,512 halafu kura za Rais wawe 44,011. Yani kuna watu 24,000 walienda vituoni kupiga kura za Rais tu lakini hawakupiga za Mbunge.

Haya ni maajabu ya dunia. Haihitaji degree kujua kwamba Tume imeongeza wapiga kura hewa 24,000 na kura zote hizo wakampa Magufuli.

Unyumbu ulipaswa uuache baada ya kampeni, sasa ni kazi tu!
Muombe Mbowe au Lowasa wakutumie scanned copy waliyopokea toka Bumbuli huiambatanishe na hiyo ya tume, kisha tuanze mjadala! Vinginevyo hizo ni fununu tu na hatuwezi kupoteza muda kuzungumzia hisia za watu!
Mlikuwa mnajitekenya na vijitafiti vyenu vya uzushi na mnakataa utafiti wenye tija wa TWAWEZA na synovate mlidhani huu ni wakati wa propaganda!
 
Am sick and tired,I hate my country!

Sijawahi kupata kitu cha kujivunia kutokana na nchi yangu. Kila kitu hovyo, tunaitia aibu hii dunia! Tupo tupo tu. watu wanatetea ujinga, demokrasia hakuna. Ni vile tu sina uwezo vinginevyo ningekuwa nimeisha hamia hata Somalia maana hata wakifanya ujinga sitaumia kwa kuwa nipo ugenini
 
Tumeshampata Kivuitu wa Zanzibar, tunasubiri kumpata wa Tanzania! Pole sana mzee Lubuva ulidhani wasimamizi wa majimbo watatenda haki kumbe wapi.
Msaada mmoja tu kwako, je unajihakikishiaje kuwa matiokeo unayotumiwa toka majimboni ni sahihi?Yana ukubalifu wowote wa mawakala wa majumuisho?
 
mmmmmh! hiii kali ya mwaka! walipoteza kumbukumbu kwenye kuedit! na si hilo tu. Birashaka sehem nyingi watakuwa wamefanya mchezo huo huo!!!!


hapa kazi tu!
 
Mimi Mtanzania halisi halisia! Nilikuwa mwanachama wa Tanu Youth League, mwanachama wa TANU, nilishiriki kutafuta jina la chama kipya na hatimaye kikaitwa CCM, nikawa mwanachama wa CCM, nilikwenda JKT mujibu wa sheria, nilishiriki mapambano ya kukomboa nchi za Afrika Kusini, nilikuwa mwalimu wa siasa, nilishiriki vita ya kumuondoa nduli Iddi Amin na mengine mengi. Kama mimi si Mtanzania halisi, basi wengine wote pia si Watanzania!

ujitetea kwako kumezidi kunifanya niamini kuwa wewe si mtanzania kabisaaaa, hata jina lenyewe Dingiswayo ni la west africa. Nyie ndo mnaoomba machafuko yaingie Tanzania ili tuwe kama nchi zenu mlikotoka maana mmezoea kuona damu inamwagika mnaona rahaaaaa
 
Uko sahihi 100% Chapa Nalo Jr.
Tanzania tumekuwa na uchaguzi uliojaa mawaa na bado tunajinadi kuwa ni kisiwa cha amani na eti tunaendesha uchaguzi wetu kidemokrasia! Chukulia mfano yanayotokea Zanzibar katika kila uchaguzi!!
Sasa uchaguzi huu hali imekuwa mbaya sana bara kasoro ni nyingi sana na za wazi ikiwemo upendeleo wa upande mmoja!
NEC ni msukule wa ccm na si vinginevyo!

Ni huzuni ambayo sioni vipi watanzania watajitoa kwenye minyororo ya ccm. Hao waangalizi wa kimataifa wanafiki tu, wamejifungia Dar mahotelini kula posho tu, wala field hawaendi kivile, sasa sijui hizo ripoti zao huwa wanamkodi nani awaandikie. Ok, basi tumuachie Mungu tu, watanzania kwa kweli ni wapole sana.
 
Last edited by a moderator:
Yani moto utawaka tu. Tume na chama kilicho ndani ya tume wanalikoroga sana.
 
Kiukweli tume imeonyesha dhairi kushindwa kusimamia vizuri zoezi hili kwani takwimu zao znamapungufu mengi. Watanzania tuhungane kupinga matokeo haya.
 
Wale jamaa wa lumumba wako wapi waweke sawa hili au wameingia mitini
 
ujitetea kwako kumezidi kunifanya niamini kuwa wewe si mtanzania kabisaaaa, hata jina lenyewe Dingiswayo ni la west africa. Nyie ndo mnaoomba machafuko yaingie Tanzania ili tuwe kama nchi zenu mlikotoka maana mmezoea kuona damu inamwagika mnaona rahaaaaa

Naona hata kiwango chako cha elimu ni duni!
 
Uchaguzi umekwisha; watanzania wanataka kuanza kazi rasmi za kujiletea maendeleo. Uzushi uzushi huu hautamsaidia yeyote. Maeneo yote mliyoshinda hamna shida. Shida ipo kule tu mlikoshindwa. tumieni busara kidogo tu kuona kuwa mmeshindwa kihalali!!
 
Tafuta matokeo ya kura za maoni ya CCM ya Bumbuli halafu linganisha na ulichokisema, kikiwa sawasawa jitafakari upya na ulichoandika.
 
Wapiga kura urais 44,011 ubunge 20,522 tofauti 23,489 .Hawa watu zaidi 23,489 waliompigia magufuli wametoka wapi?
 

Attachments

  • 1446107765417.jpg
    1446107765417.jpg
    21.4 KB · Views: 139
  • 1446107789277.jpg
    1446107789277.jpg
    38 KB · Views: 110
[QUJimbo la Bumbuli matokeo ya Ubunge yanaonesha kuwa waliopiga kura ni watu 20,512 ambapo January Makamba amepata kura 17,805. Lakini cha ajabu kwenye matokeo ya Urais jimbo hilohilo la Bumbuli waliopiga kura ni watu 44,011 ambapo Magufuli anadaiwa kupata kura 35,801.

Sasa jiulize imekuaje waliopiga kura za mbunge wawe watu 20,512 halafu kura za Rais wawe 44,011. Yani kuna watu 24,000 walienda vituoni kupiga kura za Rais tu lakini hawakupiga za Mbunge.

Haya ni maajabu ya dunia. Haihitaji degree kujua kwamba Tume imeongeza wapiga kura hewa 24,000 na kura zote hizo wakampa Magufuli.
]

Tafuta matokeo ya kura za maoni ya Bumbuli halafu linganisha na ulichokiandika halafu uje tena umu
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom