Matokeo ya Jimbo la Bumbuli yana Utata

Matokeo ya Jimbo la Bumbuli yana Utata

Status
Not open for further replies.
MODS turudishieni kitufe cha LIKE;

Kwani wengine tumeshachoka kuandika kwani tumesema mengi. Hivyo wakati mwingine tunasoma yaliyomo na yanatukosha sana hivyo hamtutendei haki kuondoa kitufe cha LIKE.


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Kabisa mkuu. Historia duniani kote ipo wazi kuwa kuwaondoa watawala dhalimu ni lazima kinuke. Lakini kwa hizi keyboard, sidhani! Yaani kutokana na upole wetu, ccm sasa wala hawaiibi tena bali inapora ushindi kweupe huku tunaona, nasi tunasema, hewala baba ccm!?

Lazima ife ukawa kama ilivotabiriwa na mtabiri maarufu. Sidhani kama wewe ni mtanzania halisi
 
Ningekuwa Invisible , hii comment ningeipandisha hapo juu kwenye uzi huu.

Lakini aliyo yasema hapo hayana ukweli wowote kama watu mbalimbali walivyokanusha tena kwa ushahidi.

Kuhusu kuharibika au kutoharibika kwa kura kwa kweli kimahesabu ni kuwa namba ya kura zitakazoharibika inaanzia 0 hadi idadi ya kura zote zilizopigwa. Nimechunguza na kuona kuwa ni majimbo mengi tu yanasema hakuna kura zilizoharibika siyo Bumbuli na Bukoba peke yake.
 
January makamba aliiba mtihani galanos leo hii wanampa jukumu la kuiba kura bumbuli hesabu hakajui kale
 
Huyu January ana akili sana, hivi matokeo yake pale Galanos secondary yalikuwa vipi?
 
Kabisa mkuu. Historia duniani kote ipo wazi kuwa kuwaondoa watawala dhalimu ni lazima kinuke. Lakini kwa hizi keyboard, sidhani! Yaani kutokana na upole wetu, ccm sasa wala hawaiibi tena bali inapora ushindi kweupe huku tunaona, nasi tunasema, hewala baba ccm!?

Uko sahihi 100% Chapa Nalo Jr.
Tanzania tumekuwa na uchaguzi uliojaa mawaa na bado tunajinadi kuwa ni kisiwa cha amani na eti tunaendesha uchaguzi wetu kidemokrasia! Chukulia mfano yanayotokea Zanzibar katika kila uchaguzi!!
Sasa uchaguzi huu hali imekuwa mbaya sana bara kasoro ni nyingi sana na za wazi ikiwemo upendeleo wa upande mmoja!
NEC ni msukule wa ccm na si vinginevyo!
 
Last edited by a moderator:
Lubuva anajitia uchizi yani anapokea matokeo kutoka CCM ndiyo anatangaza.
hizi figisu ziko well observed very soon kitaumana.

Sijui kama ukombozi kwa watanzania utatokea

Labda hiki kizazi cha wezi siku kikifutika katika uso wa Tanzania .
 
Acheni kumtaja Mungu kwenye huu upuuzi wenu.

Yaani mnalalamikia vitu ambavyo havipo.

Msipende kubeba uzushi bila kufuatilia.
Mr. Junior sote tutatoa hesabu kwa Mungu siku itakapofika then tutajua kama haki ni upuuzi au sio kwa sasa enjoy!
 
Ina maana hakuna hata kura moja ilioharibika? Basi wasambaa wamesoma sana!
 
Jimbo la Bumbuli matokeo ya Ubunge yanaonesha kuwa waliopiga kura ni watu 20,512 ambapo January Makamba amepata kura 17,805. Lakini cha ajabu kwenye matokeo ya Urais jimbo hilohilo la Bumbuli waliopiga kura ni watu 44,011 ambapo Magufuli anadaiwa kupata kura 35,801.

Sasa jiulize imekuaje waliopiga kura za mbunge wawe watu 20,512 halafu kura za Rais wawe 44,011. Yani kuna watu 24,000 walienda vituoni kupiga kura za Rais tu lakini hawakupiga za Mbunge.

Haya ni maajabu ya dunia. Haihitaji degree kujua kwamba Tume imeongeza wapiga kura hewa 24,000 na kura zote hizo wakampa Magufuli.
Upande mmoja unaweka NEC Document lakini upande mwingine unaweka maelezo yasiyokuwa na reference... ndo aina gani ya uwasilishaji mada hiyo? Hivi akitokea mtu mwingine akaweka hiyo document ya NEC kisha akasema January ameshinda kwa kura 41,711 na mpinzani wake amepata kura 2300... je unaweza kukataa hayo maelezo? Na ikiwa utakataa, ni kwanini uharamu wake na nini uhalali wa matokeo yako hayo ya ubunge?! Weka reference---
 
Hii haina ukweli wowote ni uzushi tu. Jimbo la Bumbuli katika Ubunge zimepigwa kura 44,011 na kati ya hizo kura 167 zimeharibika kwa hiyo kura halali ni 43,844. Kati ya hizo January Makamba amepata kura 36,887 na David Changeghea (CHADEMA) kapata kura 6,957. Kura 20,512 ambazo unaziongelea ni kura zilizopigwa wakati wa Kura za Maoni za Chama cha Mapinduzi kuteua Mgombea wa Ubunge wa jimbo la Bumbuli. Watanzania tuepushane na uzushi usio na msingi ambao unaweza leta machafuko. Naambatanisha matokeo hayo ya Urais, Ubunge na Kura za maoni BUMBULI. View attachment 303258View attachment 303259View attachment 303260
Cookie Moderator Mhariri Active kwa ufafanuzi wa huyu mheshimiwa naomba bora muutoe huu upotoshaji wa mleta mada au athibitishe hizo kura 20,512 za Makamba kwenye uchaguzi mkuu kazitoa wapi ilhali zilikuwa ni kura ya maoni ndani ya CCM?Upotoshaji wa aina hii ndo unatakiwa kuwapigisha watu ban.
 
Last edited by a moderator:
Lazima ife ukawa kama ilivotabiriwa na mtabiri maarufu. Sidhani kama wewe ni mtanzania halisi
Mimi Mtanzania halisi halisia! Nilikuwa mwanachama wa Tanu Youth League, mwanachama wa TANU, nilishiriki kutafuta jina la chama kipya na hatimaye kikaitwa CCM, nikawa mwanachama wa CCM, nilikwenda JKT mujibu wa sheria, nilishiriki mapambano ya kukomboa nchi za Afrika Kusini, nilikuwa mwalimu wa siasa, nilishiriki vita ya kumuondoa nduli Iddi Amin na mengine mengi. Kama mimi si Mtanzania halisi, basi wengine wote pia si Watanzania!
 
Please..acheni kudanganya maaana munahatarisha maisha ya ndungu zenu na niny wenyewe
 
Mmmmh aisee hao wataalam wa IT nina mashaka nao, ni aina gani ya uchakachuaji wanayoitumia mbona inagundulika kiurahisi? Sifa ya kufoji ni kushindwa kutambua kiurahisi

Sio kwamba hawana utaalamu ila mungu kawatia upofu waumbuke na sisi tupate vidhibiti vya ICC, wachee wanajidai kuiamini tume..wote ni ma xxm. Aibu kweli malocki challii ila kabebwa..kama mimi ningekuwa yeye ningekacha kuwa raisi wa kubebwa!
 
January makamba, unaipeleka nchi kwenye giza nene kwa ajili ya tamaa zako kuwa waziri mkuu. Hatima yako na mkwere itakuwa the hegue soon!
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom