Matangazo ya vifo Radio One

Matangazo ya vifo Radio One

Bata batani

JF-Expert Member
Joined
Nov 11, 2011
Posts
3,256
Reaction score
3,892
wakuu kama kichwa cha habari kinavyojieleza mara nyingi nikipata wasaa wakusikiliza radio one hasa mida ya mchana, kwenye matangazo ya vifo kinachonishangaza ni kwamba majina na watu niwasikiao wamekufa ni wa mikoa ya Kilimanjaro na Arusha tu. Tena hasahasa kilimanjaro.

Sio kwamba lazima wawe wanaishi huko bali hata kama wanaishi mikoa mingineyo. mathalani jana nikiwa kwenye daladala mwanzo hadi mwisho wa matangazo hayo ni watu wa jamii ya huko.

Maswali:
1. Watu wa kanda nyingine hubaguliwa wakipeleka matangazo yao?
2. kuna gharama nafuu/priorities kwa jamii ya huko?

My take:
Si kuleta mgawanyiko, matusi au kebehi. Tujadili kwa amani na kuelimishana.

Nawasilisha.

Wadau kama kuna mtu huwa anasikiliza kipindi cha matangazo ya vifo cha Redio One kinachorushwa saa saba na saa kumi baada ya taarifa ya habali ila kinachonishangaza kila siku watu wanaotajwa wote wafiwa, marehemu na misiba ni watu wa Kaskazini.
 
Wadau kama kuna mtu huwa anasikiliza kipindi cha matangazo ya vifo cha redio one kinachorusha saa saba na saa kumi baada ya taarifa ya habali ila kinachonishangaza kila siku watu wanaotajwa wote wafiwa ,marehemu na misiba ni wachagga kwani hivi hiki kipindi jamaa wamenunua

Kwa sababu wengi wanaopeleka matangazo hayo huko ni wachaga
 
teh teh'ni radio ya wachaga mkuu'we unatoka mkoa gani? Anzisheni yenu''tehh tehh
 
Nahisi wachaga wanapunguzo la bei! Kwani hata bosi ni Mangi.
 
Wadau kama kuna mtu huwa anasikiliza kipindi cha matangazo ya vifo cha redio one kinachorusha saa saba na saa kumi baada ya taarifa ya habali ila kinachonishangaza kila siku watu wanaotajwa wote wafiwa ,marehemu na misiba ni wachagga kwani hivi hiki kipindi jamaa wamenunua

Basi assumptions zitakuwa wachaga:
  1. wanakufa sana
  2. wanapendelea redio inayosikilizwa sana kwao
  3. wanautamaduni wa kutangaza vifo vya ndugu zao
  4. wana hela ya kufanya hivyo
  5. wanadhani redi ya mengi ni yao
  6. mengi anawatangazia bure
  7. wanaushamba kwahiyo wao kumtangaza mtu ni kama kafika mbinguni
  8. wanasikiliza redio hiyo tu popote walipo
 
radio one inasikilizwa sana moshi ukilinganisha na redio zingine pengine ndo maana wanaopeleka matangazo wengi ni watu wa huko.
 
Sikiliza pia Radio Free Afrika na Tbc taifa utuambie wanatangaza vifo vya makabila ya mikoa ipi ukisha yafahamu nenda katafute dawa ya kukutibu virusi vya kuchukia wachagga.
 
hapana bwana mimi sichukii ila nilikuwa nataka kufahamu........inakuaje most of time ni moshi
 
me nilisha kaa Rombo saaana tuu, hakuna redio ya tz inayoshika vizur zaid ya R1, tbc saa 1 asubuh imesha anza kuchanganyikiwa, rfa haishiki mpaka saa kumi na 2 jion kweny AM au MW. Inayo jitaid ndio hiyo R1 tena kwenye AM na baadh ya sehemu kweny FM kama KWETU!!! Theee! theeeee!!
 
me nilisha kaa Rombo saaana tuu, hakuna redio ya tz inayoshika vizur zaid ya R1, tbc saa 1 asubuh imesha anza kuchanganyikiwa, rfa haishiki mpaka saa kumi na 2 jion kweny AM au MW. Inayo jitaid ndio hiyo R1 tena kwenye AM na baadh ya sehemu kweny FM kama KWETU!!! Theee! theeeee!!
aliyekuambia rombo ni tanzania ni nani? Kwanza redio zinazoshika vizur ni citizen, capital, kbc, et al zote za kenya, ukiwa rombo mitandao ya cm inakataa kushika na kuwa influenced na network za safaricom na kencell! Radio one na free maeneo meng ya rombo hazshiki totally!
 
wachaga wana utamaduni wa kuzika moshi.na wachaga wametapakaa kila kona ya nchi wakisaka maela.ili habari imfikie kila m2 lazima watumie redio.pia wachaga wana vyama vya kuzikana na moja ya kazi ya chama nikutangaza
 
Wadau kama kuna mtu huwa anasikiliza kipindi cha matangazo ya vifo cha redio one kinachorusha saa saba na saa kumi baada ya taarifa ya habali ila kinachonishangaza kila siku watu wanaotajwa wote wafiwa ,marehemu na misiba ni wachagga kwani hivi hiki kipindi jamaa wamenunua

jibu ni simple tu "wachaga wengi wana utamaduni wa kupeleka matangazo ya vifo redio one"
 
ni kwakuwa wana umoja ndo maana wanatangaza ili kupeana taarifa
ndo maana wachagga watabaki kuwa tishio tanzania daima dumu
kabila gani lina utamaduni wa kukutana walau mara moja kwa mwaka [worldwide]????? WACHAGGA
labda ungeuliza kwa nini matangazo mengi ya biashara karibu radio zote yanatumia lafudhi ya kichagga???/

:violin::violin::violin:
 
Back
Top Bottom