Matangazo ya vifo Radio One

Matangazo ya vifo Radio One

Mimi wachaga wenzangu wananiachaga hoi pale nnapomsikia mtangazaji akisema habar zimfikie patirisia mushi akiwa uholanzi, yudatade mallya akiwa marekan na kanyewest temba akiwa uingereza !!#
wanasikiza online wala usishangae
 
Ngoja wewe ukifa wewe tutaenda kukutangaza bure
 
Habari zimfikie Aikael Somi akiwa Machame, Kokuberwa Rugaimukamu akiwa Bukoba, Msua Nakembetwa akiwa Singida, Chigwiyemisi Chilolo akiwa Dodoma, na jamaa wote wanaohusika.
 
wakuu kama kichwa cha habari kinavyojieleza mara nyingi nikipata wasaa wakusikiliza radio one hasa mida ya mchana, kwenye matangazo ya vifo kinachonishangaza ni kwamba majina na watu niwasikiao wamekufa ni wa mikoa ya Kilimanjaro na Arusha tu. Tena hasahasa kilimanjaro.

Sio kwamba lazima wawe wanaishi huko bali hata kama wanaishi mikoa mingineyo. mathalani jana nikiwa kwenye daladala mwanzo hadi mwisho wa matangazo hayo ni watu wa jamii ya huko.

Maswali:
1. Watu wa kanda nyingine hubaguliwa wakipeleka matangazo yao?
2. kuna gharama nafuu/priorities kwa jamii ya huko?

My take:
Si kuleta mgawanyiko, matusi au kebehi. Tujadili kwa amani na kuelimishana.

Nawasilisha.


Nionyeshe pia Bar yoyet maarufu na hata za uswahilini ambazo ni za wachaga na wanauza maji ya uhai,, always Kilimanjaro, hawa jamaa ''wazalendo'' aiseee
 
Duh! Kwahiyo ukipata kazi hapo kwa Mzee Machache ni lazima ujue kuyatamka majina na maeneo yenye asili ya kichagga kwa usahihi LA sivyo kazi huna
 
wakuu kama kichwa cha habari kinavyojieleza mara nyingi nikipata wasaa wakusikiliza radio one hasa mida ya mchana, kwenye matangazo ya vifo kinachonishangaza ni kwamba majina na watu niwasikiao wamekufa ni wa mikoa ya Kilimanjaro na Arusha tu. Tena hasahasa kilimanjaro.

Sio kwamba lazima wawe wanaishi huko bali hata kama wanaishi mikoa mingineyo. mathalani jana nikiwa kwenye daladala mwanzo hadi mwisho wa matangazo hayo ni watu wa jamii ya huko.

Maswali:
1. Watu wa kanda nyingine hubaguliwa wakipeleka matangazo yao?
2. kuna gharama nafuu/priorities kwa jamii ya huko?

My take:
Si kuleta mgawanyiko, matusi au kebehi. Tujadili kwa amani na kuelimishana.

Nawasilisha.

Wewe kwanini watu wa Kilimanjaro wakati wa X-mass ni wao tu wanakwenda nyumbani kusherehekea, embu tujadili swala hili

Maswali:
1.Watu wa kanda nyingine hunyimwa na serikali kwenda kusherehekea christmass?
2.Kuna unafuu zaidi wa nauli kwa jamii ya Kilimanjaro kuliko maeneo mengine?

Tujadili kwa amani na kuelimishana
 
Watu wa kilimanja to ni wepesi kulipia matangazo redioni,hakuna aliyezuiwa kupeleka matangazo ya msiba redioni

Siyo wepesi tu kulipia bali ni watu wanaoheshimiana na kuheshimu wapendwa wao pindi wanapofariki. Makabila mengine hayafanyi hivyo na inashangaza sana kusikia wakilalamika juu ya hili!
 
Mimi wachaga wenzangu wananiachaga hoi pale nnapomsikia mtangazaji akisema habar zimfikie patirisia mushi akiwa uholanzi, yudatade mallya akiwa marekan na kanyewest temba akiwa uingereza !!#

Radio one inasikika kupitia mtandao mahali popote duniani sasa unashangaa nini hapo!
 
Leo katika mizunguko yangu bahat mbaya au nzur nkasema acha nisikilze Radio nikajikuta tu nmeweka Radio Fulan nisingependa kuitaja.
Kwanza niseme tu mie huwa nasikiliza mara chache sana hyo radio so sitak kuwa na jibu la jumla kuhusu nilichokisikia.
Kipindi nachagua station mida ya saa nne kwenda tano bas nkajikuta tu nimeweka hyo radio kwa coincedence tu na sio kwamba ilipangwa iwe hvyo.
Bahat mbaya au nzur nikakuta ni muda wa matangazo ya vifo so nikawa interested kidogo kwa maana ni kitu ambacho nimekisikia zaman sana enz za Radio Tanzania ile saa 10 baada ya taarifa ya habar.
Likatajwa jina la kwanza sikuwa na shida nkasikia msiba uko Moshi, likatajwa la pili Nikasikia same la tatu ni wilaya za Mkoa wa Kilimanjaro mpka anakuja kumaliza majina yote, Wafiwa wote ni watu wa Mkoa wa Kilimanjaro.
Nikapata maswali ina maana watu wa Kilimanjaro ndio pekee wanaopeleka majina yao hyo radio au Radio hyo inatangaza majina ya watu wa mkoa huo tu.
Sijataka kuweka jibu la jumla kwa maana sijasikilza radio uhuru/Tbc Fm kwa muda mrefu sana so sijajua kwa upande wao wakoje.
Neno langu lisitumike kama hukumu ya jumla ila kwa wale wanaosikilza hyo radio mara kwa mara hii kitu ni imetokea leo by coincedece au huwa iko hvyo tu.
 
Kaskazini huwa ndio hufiwa tu. Au wengine hawana fedha za kutangaza... yote mawili yanawezekana
 
Ni utamaduni wao , zamani mtu akifa wao ndio walikuwa wakitangaza sana sababu ya kuwa mikoa mingine ya nje kwa wingi na kuwa na extended family zenye strong bonds, refer wanaenda pia nyumbani kwa wingimwisho wa mwaka naona ikawa ndio mazoea mpaka leo hii wanatangaza ...si unajua old habits die hard
 
Kuna sababu tofauti
1. Kutokana na kutapakaa sehemu mbalimbali za nchi na duniani
2. Kuna vikundi vya kikoo, kikanda, kimkoa na hivyo kundi kupeleka taarifa ili itangazwe. Kuna baadhi ya makabila hayana vikundi vya kufa na kuzikana
 
Wadau kama kuna mtu huwa anasikiliza kipindi cha matangazo ya vifo cha Redio One kinachorushwa saa saba na saa kumi baada ya taarifa ya habali ila kinachonishangaza kila siku watu wanaotajwa wote wafiwa, marehemu na misiba ni watu wa Kaskazini.
Duuu hadi matangazo ya wafu redioni mnajadili! Kwa taarifa yako hii radio usikivu wake kaskazini na tanzania nzima ni wa uhakika haina noise interference kama radio zingine pia watu wa huko wana mapenzi nayo. Mpaka hapo kuna ubaya kutangaza habari za wafu wao R1? Kumbuka haya matangazo siyo bure ni PESA yako tuuu.
 
Wakuu leo nimeleta huu uzi tujadili kidogo hiki kipindi cha matangazo ya vifo kinachorushwa na redio one sterio nimeanza kukisikia muda mrefu sana,lakini niligundua ni kwanza asilimia 95 ya watu ambao wanatangazwa au kutangaziwa vifo ni wachaga,ina maana wao ndio wanapenda sana kujua taarifa zao wengine hapana au inakuaje? wachaga njoeni hapa na ninyi mtueleze.
 
Wakuu leo nimeleta huu uzi tujadili kidogo hiki kipindi cha matangazo ya vifo kinachorushwa na redio one sterio nimeanza kukisikia muda mrefu sana,lakini niligundua ni kwanza asilimia 95 ya watu ambao wanatangazwa au kutangaziwa vifo ni wachaga,ina maana wao ndio wanapenda sana kujua taarifa zao wengine hapana au inakuaje? wachaga njoeni hapa na ninyi mtueleze.

kama uko mkoa "A" na radio inayosikika zaidi hapo ni radio "X" huwezi peleka tangazo lako radio "Y" ambayo inasikika zaidi mkoa "B".
 
Basi assumptions zitakuwa wachaga:
  1. wanakufa sana
  2. wanapendelea redio inayosikilizwa sana kwao
  3. wanautamaduni wa kutangaza vifo vya ndugu zao
  4. wana hela ya kufanya hivyo
  5. wanadhani redi ya mengi ni yao
  6. mengi anawatangazia bure
  7. wanaushamba kwahiyo wao kumtangaza mtu ni kama kafika mbinguni
  8. wanasikiliza redio hiyo tu popote walipo
namba 4
 
Back
Top Bottom