Matangazo ya makampuni ni anasa katika nchi yetu masikini!

Matangazo ya makampuni ni anasa katika nchi yetu masikini!

Kwa maneno mengine ni kwamba mtoa mada anajaribu kusema kwamba MPANGAJI hatakiwi "kula wali kuku" kila siku kwa sababu MWENYE NYUMBA ameshindwa kuwalipia wanae ada ya shule ilhali mpangaji analipa kodi ya nyumba kama kawaida.
Swadakta... hiki ndo hasa anachojaribu kusema!
 
Kwa maneno mengine ni kwamba mtoa mada anajaribu kusema kwamba MPANGAJI hatakiwi "kula wali kuku" kila siku kwa sababu MWENYE NYUMBA ameshindwa kuwalipia wanae ada ya shule ilhali mpangaji analipa kodi ya nyumba kama kawaida.
Ukirejea katiba ya JMT na ukatambua hili ni taifa la namna gani kikatiba...basi utagundua ni ukiukwaji mkubwa wa kikatiba kujineemesha pengine kwa kuhujumu wengi na baadaye unafanya anasa badala ya maendeleo..

Pia jaribu kufikiria inakuaje tuonewe huruma na mzungu kutoka marekani na kupewa msaada halafu hawa wazungu koko waliopo hapa hapa wasiwajibike kuchangia ustawi wa taifa???

Inakuwaje kama Taifa tushangilie miss Tanzania kupewa vitita vya fedha na mazagazaga kibao halafu mwanafunzi wa kwanza kitaifa kwenye somo flani la sayansi akaishia kupigiwa makofi bungeni??

Kampuni ni lazima zibadili mtazamo na zisipotaka basi zishurutishwe kubadili mtazamo vivyo hivyo kwa viongozi na jamii kwa ujumla.
 
Naona unataka kuhamishia lawama kwenye Broadcasting na media companies ...nashukuru umeikumbusha serikali kuhusu kuifuatilia hii aina ya kodi ambayo naamini haitozwi na ndio maana makampuni haya yanajiachia.....

Jaribu kunielewa tena na tena ....unadhani ni sawa kwa makampuni haya kuifikia audience kwa style hii wanayoitumia keeping in mind kwamba audience hii ni ya kitanzania?

Is there an alternative to reach even larger audience by using a new strategy, let say by improving your network at peripheral areas??

Kwa mfano jenga mnara kijijini na uchangie madawati kijijini hapo na ikiwezekana tengeneza wakala wako hapo kijijini....hili naliona ni sahihi kwa kampuni,Serikali na jamii ya kijiji husika.

Sioni sababu ya kuwa na makampuni meengi yasiyokuwa na impact kwenye maendeleo ya jamii yetu....

Ama kama yanataka kujidai ni ya "kimataifa zaidi" basi hizo adverts zao zilenge masoko ya kongo,Kenya,Burundi,Rwanda n.k na sio kutupigia mikelele.
Kivipi natuma lawama media companies? You and I both know kwamba ni media platforms ndizo zinatumika na advertisers kufikia target markets! Na hizo media companies hizo ndo kazi zao na ndio source kuu ya mapato yao! Kwahiyo it's all about business, no offense! Kama rates zao ni kubwa possibly inatokana na gharama ambazo nao wanaingia!

"Unauliza, je ni sahihi kuifikia audience kwa style wanayotumia?" Kwa staili ipi hasa? Ikiwa kwa kutumia media especially tv + radio the answer is 101% YES! Hiyo ndiyo njia efficient zaidi kuliko nyingine yoyote ile! Western countries, siku hizi kuna significant shift from traditional advertising platforms like radio + tv to digital... kv use of social media! Kwa mazingira ya Tanzania, hiyo alternative haiwezi kuwa efficient... unaitumia tu as a part of promotional or marketing mix ili kuifikia cyber community! Unaweza kuifanya social media kuwa platform yako kuu endapo tu; umejiridhisha your target market ni social networkers!

Kwamba uweke Mawakala Vijijini; si tu kwamba hiyo ni completely ineffective and inefficient way ya kufikia target market like pia at the end of the day unaweza kukuta ni VERY EXPENSIVE compared to traditional means! Assume, a maximum 100 villages zinahitaji Wakala 50, One Agency kwa kila vijiji 2 zinazokugharibu 50 Million per month! The very same 50 Million ukizipeleka Radio Free Africa; matangazo yao yatafika kwa vijiji zaidi ya 5000! Sasa i wapi hapo rationale ya kutumia Mawakala?!

Hoja yako ya kwamba ikiwa yanataka kujidai ya kimataifa cjui unakusudia nini hasa! Hebu toa mfano wa tangazo moja na ueleze ni nini hasa hakikutakiwa kufanyika kwenye tangazo husika! Anyway, ngoja niweke hivi: Assume wewe ndo Head wa Marketing wa kampuni ya tangazo husika... ungefanya nini kinyume na kinachofanyika bila kuathiri lengo kuu la kwanza la kuifikia audience kubwa zaidi kwa kuzingatia your target market!
 
Tusifute matangazo bali turegulate fedha inayotumika ilihali nchi hii ni yamasikini.

Inashangaza kuona tangazo la kampuni likiwa la bei ghali sana huku wizara ya afya ikipewa msaada wa matangazo na wamarekani.


KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA
Tatizo si fedha inayotumika, tatizo ni mazoea mliokuwa nayo..Uwekezaji wa maana ni gharama na si masikhara ndo maana fedha inatumika nyingi..Ndo maana hata shirika lenu limezidiwa kwa kuwa matangazo yake ni ya bei chee....Maendelea ni gharama babu, wale ni wawekezaji na wanaleta teknolojia nchini kwako..Jifunze na si kuwapangia....
 
Ukirejea katiba ya JMT na ukatambua hili ni taifa la namna gani kikatiba...basi utagundua ni ukiukwaji mkubwa wa kikatiba kujineemesha pengine kwa kuhujumu wengi na baadaye unafanya anasa badala ya maendeleo..

Pia jaribu kufikiria inakuaje tuonewe huruma na mzungu kutoka marekani na kupewa msaada halafu hawa wazungu koko waliopo hapa hapa wasiwajibike kuchangia ustawi wa taifa???

Inakuwaje kama Taifa tushangilie miss Tanzania kupewa vitita vya fedha na mazagazaga kibao halafu mwanafunzi wa kwanza kitaifa kwenye somo flani la sayansi akaishia kupigiwa makofi bungeni??

Kampuni ni lazima zibadili mtazamo na zisipotaka basi zishurutishwe kubadili mtazamo vivyo hivyo kwa viongozi na jamii kwa ujumla.

Labda useme tuwapandishie kodi, lakini kwa mfumo wa sasa wa kibepari unachokisema hakiwezekani. Yaani kampuni ilazimike kutatua kero za wananchi wakati hili ni jukumu la serikali. Labda tu uwe wazi kwamba unapenda tuwanyang'anye matajiri kile walichonacho tukawape masikini (kama bwana Yesu alivyotaka wakati huo).
 
Nimejaribu kuangalia uwekezaji wa baadhi ya makampuni hasa haya makampuni ya simu nikaona kuwa yanatumia gharama kubwa sana.

Hii inanifanya nifikirie kuwa kuna umuhimu wa kuwa na regulatory body ya kufuatilia gharama hizi zinazotumiwa na makampuni kufanya matangazo ambayo hayana thamani na fedha inayorumika...

Ushauri wangu ni kuwa hizi fedha zinazotumika kwenye matangazo ni vyema zikaelekezwa kwenye ununuzi wa madawati ambapo tumeshuhudia kuna upungufu mkubwa.

Isitoshe makampuni haya yanawezekana kuwa yanatumia fedha nyingi sana katika matangazo badala ya kulipa kodi stahiki.

Hebu wabunge watunge sheria ya kudhibiti matumizi yasiyo na tija kwa makampuni haya ambayo yanalipa kodi kiduchu kulinganisha na wanachokipata.

Hizo nikampuni na ziko kwenye ushindani wa kibiashara, unachemka sana wanunue madawati? Jukumu lao ni kulipa kodi stahiki kwa mjibu wa sheria, kama watachangia madawati ni sawa kupitia Corporate social responsibility, au unafikiri hizo kampuni zinaendeshwa kwa kodi zako? Duniani kote biashara inaendeshwa kwa matangazo, angalia kwenye viwanja vya michezo makampuni yanavyojitangaza, una mawazo ya kiujamaa jamaa na kijima sana.
 
Kivipi natuma lawama media companies? You and I both know kwamba ni media platforms ndizo zinatumika na advertisers kufikia target markets! Na hizo media companies hizo ndo kazi zao na ndio source kuu ya mapato yao! Kwahiyo it's all about business, no offense! Kama rates zao ni kubwa possibly inatokana na gharama ambazo nao wanaingia!

"Unauliza, je ni sahihi kuifikia audience kwa style wanayotumia?" Kwa staili ipi hasa? Ikiwa kwa kutumia media especially tv + radio the answer is 101% YES! Hiyo ndiyo njia efficient zaidi kuliko nyingine yoyote ile! Western countries, siku hizi kuna significant shift from traditional advertising platforms like radio + tv to digital... kv use of social media! Kwa mazingira ya Tanzania, hiyo alternative haiwezi kuwa efficient... unaitumia tu as a part of promotional or marketing mix ili kuifikia cyber community! Unaweza kuifanya social media kuwa platform yako kuu endapo tu; umejiridhisha your target market ni social networkers!

Kwamba uweke Mawakala Vijijini; si tu kwamba hiyo ni completely ineffective and inefficient way ya kufikia target market like pia at the end of the day unaweza kukuta ni VERY EXPENSIVE compared to traditional means! Assume, a maximum 100 villages zinahitaji Wakala 50, One Agency kwa kila vijiji 2 zinazokugharibu 50 Million per month! The very same 50 Million ukizipeleka Radio Free Africa; matangazo yao yatafika kwa vijiji zaidi ya 5000! Sasa i wapi hapo rationale ya kutumia Mawakala?!

Hoja yako ya kwamba ikiwa yanataka kujidai ya kimataifa cjui unakusudia nini hasa! Hebu toa mfano wa tangazo moja na ueleze ni nini hasa hakikutakiwa kufanyika kwenye tangazo husika! Anyway, ngoja niweke hivi: Assume wewe ndo Head wa Marketing wa kampuni ya tangazo husika... ungefanya nini kinyume na kinachofanyika bila kuathiri lengo kuu la kwanza la kuifikia audience kubwa zaidi kwa kuzingatia your target market!
Kwa nini unahisi kuwekeza kwa wakala itakugharimu hiyo 50 M ?? Hivi mawakala wa MPESA wanaigharimu voda 50M kwa kila wakala?

Nasema wanajaribu kuwa wa kimataifa kwa audience ambayo ni ya kibongobongo....

Jibu kuhusu kujenga minara huko vijijini....haisaidii kulifikia soko kubwa compare to hawa wachache wa mjini?

Unataka kuniambia makampuni haya hayana mipango yoyote ya kuendeleza jamii au kuukuza uchumi...yaani lengo lao ni kunenepesha matumbo yao na kuwekeza Dubai which is more expensive ukilinganisha na kijijini kwetu Kikonga.
 
Tatizo si fedha inayotumika, tatizo ni mazoea mliokuwa nayo..Uwekezaji wa maana ni gharama na si masikhara ndo maana fedha inatumika nyingi..Ndo maana hata shirika lenu limezidiwa kwa kuwa matangazo yake ni ya bei chee....Maendelea ni gharama babu, wale ni wawekezaji na wanaleta teknolojia nchini kwako..Jifunze na si kuwapangia....
Ni bahati mbaya sana sijaona teknolojia ya maana waliyoileta zaidi ya kutumia existing Gov infrustructures kuvuna fedha.

Ingekuwa wanalenga soko la nje ya Tanzania ningewapa mkono lakini they are too local to use such expenses
 
Hizo nikampuni na ziko kwenye ushindani wa kibiashara, unachemka sana wanunue madawati? Jukumu lao ni kulipa kodi stahiki kwa mjibu wa sheria, kama watachangia madawati ni sawa kupitia Corporate social responsibility, au unafikiri hizo kampuni zinaendeshwa kwa kodi zako? Duniani kote biashara inaendeshwa kwa matangazo, angalia kwenye viwanja vya michezo makampuni yanavyojitangaza, una mawazo ya kiujamaa jamaa na kijima sana.
Kiasi wanachotumia kwenye CSR ni kidogo mno kulinganisha na kipato wanachopata...

Kodi wanayolipa ni ndogo mno kulinganisha na wanachokipata ...hata kwenye top ten ya walipaji kodi hawaingii

Gharama wanazotumia kwenye matangazo na matamasha yasiyo na tija kwao na kwa jamii ni kubwa mno...

Gharama wanazotutoza kama wateja ni kubwa kulinganisha na maeneo mengi duniani...

Nadhani hoja yangu kwa uchache inalenga hayo maeneo niliyoyataja.
 
Sasa madawati na matangazo vinahusianaje... tizeni kodi stahiki muyaache makampuni yafanye biashara..
 
Mawazo mgandoi .....tzt umelishwa nini? Kwenye bongo zetu?
 
Dah! Mkuu wangu Richard cjakusoma, it's a if nimeamka na hangover!

Swali lako naona ni kama lime-base kwenye paragraphs zako 3 za mwisho (ndivyo nilivyoelewa kwahiyo unaweza kunirekebisha if am wrong) kwamba, assume nimefungua duka la kuuza saruji lakini kila mteja anayekuja; nampa na box moja la tiles FREE but hizi tiles nami nimepata free toka kwa sponsor anayelenga kuitangaza hiyo bidhaa yake ya tiles.

Kwahiyo unachouliza ni ikiwa huyo sponsor anafahamu gharama halisi za matangazo ya hizo tiles; au? Btw, gharama zipi hasa cuz' ikiwa mzigo umetoka kwenye stock yake it's obvious atafahamu! Anyway, hebu liweke swali lako vizuri!

Yes, sawasawa ni huyo sponsor.

Mimi kwa uelewa nafikiri watoa matangazo huwa wanakuwa third parties chini ya Sponsor ambae ndie mhusika mkuu.

Swali langu ni la kiufundi kidogo.
 
Jingalao
Ufahamu wako wa biashara ni big fat ZERO
Unadhani mtu anatangaza biashara yake bila manufaa yoyote?
Wanatumia fedha nyingi kweli lakinl manufaa wanayaona
Bila matangazo hayo usingeliona Tv na FM radio hata moja ikifanya kazi nchini
Baki na kuisifu CCM mambo ya ki professional tuachie
 
Jingalao
Ufahamu wako wa biashara ni big fat ZERO
Unadhani mtu anatangaza biashara yake bila manufaa yoyote?
Wanatumia fedha nyingi kweli lakinl manufaa wanayaona
Bila matangazo hayo usingeliona Tv na FM radio hata moja ikifanya kazi nchini
Baki na kuisifu CCM mambo ya ki professional tuachie
Tatizo umechefukwa bila kuielewa hoja yangu!
 
A man who stops advertising to save money is like a man who stops a clock to save time
 
Kumbuka uwepo wa hayo matangazo ni sehemu ya ajira...na jinsi yanavyokuwa mengi na ya gharama kubwa basi ndivyo watu wananufaika zaidi.......sasa kwa hizo dua zako shindwa na ulegee.
 
Matangazo yao hayana thamani inayotumika!!
Umetumia mbinu gani ya kupima matokeo ya pr na adverts zinazofanywa na makampuni hayo ya simu ukilinganisha na fedha zinazolipwa na hayo makampuni kwenye vyombo vya habari?
 
sasa hata wakifanya tangazo ka 10m badala ya 100m sasa hiyo 90m inaingia kwa mfumo upi kwenye madawati?!
 
Rejea mada yangu viziri...wewe unaona ni sawa kutumia milioni kumi kwenye matangazo wakati kuna watoto wanakaa chini?halafu matangazo yenyewe yanamlenga mtu anayelala njaa?
Hata hueleweki! Ina maana hata hujui kwamba hayo makampuni yanafanya kitu kinaitwa CSR-Corporate Social Responsibility na yamekuwa yakichangia sana tu madawati kwa ajili ya wanafunzi na hata vyakula kwa wenye njaa kupitia vituo vya watoto yatima. Na ni kwanini umeamua kuiondolea serikali wajibu wake na kuuhamishia kwa makampuni ya simu? Kwanini usiilaumu serikali au wakala wake, kwa mfano, kwa kutumia fedha kulipa "vijana wa mtandaoni" wanaoshangilia lolote hata lisilo na maslahi kwa nchi, badala ya fedha hizo kufanya yale ambayo unataka makampuni ya simu yafanye badala ya kutangaza products zake?
 
Back
Top Bottom