Matangazo ya makampuni ni anasa katika nchi yetu masikini!

Matangazo ya makampuni ni anasa katika nchi yetu masikini!

Off topic! Ila naomba unijuze TCRA na wenyewe waliwalalamikia coca cola kuhusu lile tangazo au ni Kenya peke yao?

Hiyo habari siifahamu.

Ila nilitaka kusisitiza kwamba mleta mada ana hoja kwamba kuwepo na bodi inayoangalia standard za matangazo na, umuhimu na malengo yake na huwa inafanya kazi zake chini ya TCRA ambao ndio mama ya bodi hio.
 
jero halotel mb 700 kuna mtandao jero mb 100 na kibubu! bango la kibubu linakuja,,
 
Hapana mkuu mueleweshe tu ana hoja ya msingi.

Je tunayo bodi imara inayosimamia ushindani na matangazo?
Hakuna hoja hapo cuz' hata kungekuwa na regulatory authority bado ingetakiwa kusimama within marketing strategies! Kwa mfano, as a business firm huwezi kuniambia nipeleke matangazo only kwenye radio stations XYZ wakati my RESEARCH tells me in order to reach the largest possible target market ni lazima nitumie tv na radio bila kusahau billboards! Kama utaiambia nisitumie tv for instance; I'll ask you ni namna gani naweza kufikia target market isiyosikiliza radio ili nisipate hasara kwenye biashara yangu! As a business firm, huwezi kuniambia nisimtumie for instance Diamond Platnumz wakati nafahamu watu wanakesha kwenye page yake... na ukinitaka nisimtumie you've to give me the alternative ya kuifikia cyber community ili nisiingie hasara kwenye biashara yangu! Mifano ipo mingi but all conclude one thing: Promotional Mix is inevitable! Si ajabu hata wewe unaweza kukaa hata mwezi moja bila kuangalia tv lakini ukaona poa tu lakini ukawa usiwe tayari kutosikiliza radio! Inawezekana Clouds au EFM husikilizi kabisa lakini huambiwi kitu mbele ya Magic FM! So, gharama zinakuwa kubwa kutokana na ku-utilize hizi communication channels ili product campaign for instance, ikufikie kokote ambako utakuwa!
 
Mimi nakuelewa kamanda Chige, sidhani kama mleta mada atakuwa nawe.

Na hata ukitaka uwafikie Wahadzabe kuna mambo mengi kama logistics na malazi, chakula na vingine.

Lakini yeye ameoanisha kati ya matumizi ya hiyo pesa na kodi inayolipwa.

Sifahamu lengo lake hapo.

Ila matangazo yako ya aina nyingi ila yanayowika Zaidi ni haya ya matangazo ya kupitia media au "advertising messages" yaani kuanzia magazeti redio, runinga mpaka blogs na text messages.

Halafu kuna haya matangazo ambayo nafikiri ndiyo yanawika sana nchini kwetu ya commercial ads abayo yana lengo la kuongeza idadi ya wateja kwa kupanua huduma na na bidhaa yaani unafungua duka la na hapo hapo unagawa simu mbili tatu za bure na hii ndio inaitwa "Branding" yaani mteja anatumika na anatumiwa hapohapo kukuza jina la kampuni.

Sasa mara nyingi kunakuwa na sponsors kwa hii shughuli je sponsors huyu anafahamu gharama halisi ya shughuli za matangazo haya.

Nafikiri utanielewa kamanda maana wewe unaonekana unao utaalam wa hili eneo.
 
Hujanielewa mkubwa!
Mimi naongele matangazo ya kila siku ya makampuni ambayo kila iitwayo leo yanaboreshwa kufikia kiwango cha kimataifa ingawa yanawalenga watanzania asilimia sabini na zaidi wenye umasikini...ni kiasi gani wanatumia kwa mwaka kwenye matangazo ukilinganisha na misaada wanayotoa au kodi wanayolipa?
Kuboreshwa kufikia kiwango cha kimataifa au kutengeneza matangazo bora? Listen, people invest money to design yale matangazo kwahiyo lazima uhakikishe una design catchy ads ili ku-grab attention!!

Na hiyo unayoita matangazo ya kila siku; ningekushauri jiongezee maarifa kwenye kitu kinachoitwa Product Life Cycle! And am telling you, endapo kampuni za kibiashara zingekuwa na namna ya kukwepa marketing basi wangeshukuru ile mbaya cuz' marketing ni very expensive sema ndo vile haikwepeki in competitive environment!!

Halafu hizo habari za madawati na hospital kukosa dawa zinawahusu nini business firms? Provision of social services ni purely kazi ya serikali lakini sio ya Tigo wala Vodacom! Serikali si wanakusanya kodi? Hata hayo mapesa mengi yanayotumika kwenye matangazo si yanaenda kwenye other business entities ambako pia serikali inakusanya kodi?! Sasa how come tena ionekane uhaini mimi kuwafikia wateja wengi niwezavyo kv tu wewe serikali ( don't take it personal) umeshindwa kutimiza wajibu wako wakati wajibu wa kwangu mimi wa kukulipa kodi nimeshautimiza! And probably, on top of that nina corporate social responsibility program na kujitwisha majukumu uliyotakiwa kufanya wewe! Kama kodi haitoshi, the smart way sio kuniambia ni namna gani niwafikie wateja wangu bali nI wajibu wako wewe mwenyewe na timu yako kubuni vyanzo vingi zaidi vya mapato!
 
Tusifute matangazo bali turegulate fedha inayotumika ilihali nchi hii ni yamasikini.

Inashangaza kuona tangazo la kampuni likiwa la bei ghali sana huku wizara ya afya ikipewa msaada wa matangazo na wamarekani.


KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA

Wewe si kila siku unasema hii Serikali ya viwanda haihitaji msaada toka popote pale? Sasa inakuwaje tena hii post. Kuhusu matangazo zile ni binafsi mkuu wanauwezo wa kufanya vyovyote chamsingi wasikiuke sheria za nchi.
 
Nimejaribu kuangalia uwekezaji wa baadhi ya makampuni hasa haya makampuni ya simu nikaona kuwa yanatumia gharama kubwa sana.

Hii inanifanya nifikirie kuwa kuna umuhimu wa kuwa na regulatory body ya kufuatilia gharama hizi zinazotumiwa na makampuni kufanya matangazo ambayo hayana thamani na fedha inayorumika...

Ushauri wangu ni kuwa hizi fedha zinazotumika kwenye matangazo ni vyema zikaelekezwa kwenye ununuzi wa madawati ambapo tumeshuhudia kuna upungufu mkubwa.

Isitoshe makampuni haya yanawezekana kuwa yanatumia fedha nyingi sana katika matangazo badala ya kulipa kodi stahiki.

Hebu wabunge watunge sheria ya kudhibiti matumizi yasiyo na tija kwa makampuni haya ambayo yanalipa kodi kiduchu kulinganisha na wanachokipata.
Kama shida yako ni madawati basi nenda makao makuu ya ccm utakuta majina ya watu wote wanaosafirisha magogo nje ya nchi bila vibali .
 
Hujanielewa mkubwa!
Mimi naongelea matangazo ya kila siku ya makampuni ambayo kila iitwayo leo yanaboreshwa kufikia kiwango cha kimataifa ingawa yanawalenga watanzania asilimia sabini na zaidi wenye umasikini...ni kiasi gani wanatumia kwa mwaka kwenye matangazo ukilinganisha na misaada wanayotoa au kodi wanayolipa?

Jingalao, kwa mtazamo wangu ni kwamba serikali inaweza ku-intervene kwa upande wa faida lakini, sidhani kama Serikali inaweza kuingilia expenditure ya makampuni binafsi (e.g. Tigo, Voda e.t.c) kwa namna yeyote ile....nasema hivi kwa sababu kuu mbili: Kwanza kabisa, Marketing/Advertising ni moja kati ya nguzo kubwa kabisa katika uwekezaji ambao unafanywa na kampuni hizi.....jitihada zao katika ku-advertise huduma au bidhaa wanazozalisha ndiyo zinawawezesha kushawishi wananchi waweze kuzifahamu, kuzipenda na hatimaye kutumia huduma/bidhaa za makampuni haya na hivyo ndivyo faida inavyopatikana......kwa ufupi ni kuwa, "The more these companies advertise their products or services, the higher the chances of attracting more customers hence high profit"....na ndiyo sababu unaona wanawekeza kiwango kikubwa cha fedha katika component hii ya Marketing.

Kwa upande mwingine, hizi kampuni ni entity ambazo zinajitegemea kwa kila kitu including namna wanavyopata mitaji na namna ya kusimamia na kuendesha shughuli zao; hata hivyo, kila kampuni inawiwa kuzingatia sheria katika operation zake zote.....na katika hili la kuzingatia sheria inajumuisha kulipa kodi (Ambayo ndiyo inapaswa kutumika na serikali katika kuhudumia wananchi wake katika elimu, afya, miundombinu e.t.c.), vilevile **kisheria kampuni hizi zinapaswa kukidhi their corporate social responsibility (e.g. Kujenga shule, kuchangia madawati, kuhudumia makundi yenye mahitaji maalum e.t.c.) kwa jamii inayozunguka maeneo huduma inapotolewa.

Kwa mantiki hiyo Serikali ina jukumu la kusimamia sheria na kuhakikisha kuwa kampuni hizi zinalipa kodi stahiki kwa wakati na pia kuhakikisha kuwa zinadumisha na kuchangia maendeleo ya jamii zilizo karibu na eneo huduma inapotolewa.

Hapa kwenye kui-enforce Corporate Social Responsibility (CSR) ya makampuni ndipo penye tatizo kwa sababu, hadi kufikia mwaka 2014, Tanzania haikuwa na sheria zozote ambazo zinaweza kutumika kuzibana hizi kampuni ili ziweze kuchangia maendeleo ya jamii zinazowazunguka. Uamuzi wa kuchangia ama kutokuchangia maendeleo ya jamii husika umeachwa mikononi mwa kampuni zenyewe. Kipindi cha nyuma kidogo (Kati ya 2014/15) kulikuwa na mazungumzo ya chinichini kuwa huenda serikali ikaanzisha sheria ya kusimamia CSR ili kuwezesha wananchi waweze kunufaika na uwepo wa kampuni hizi kwenye maeneo yao....hata hivyo sina updates zozote kuhusiana na hilo...wenye ufahamu zaidi kuhusu hatua iliyofikiwa na serikali katika mjadala wa kuanzisha Corporate Social Responsibility Act waje hapa watujuze zaidi.

Sheria hiyo ikiwepo, itaiwezesha serikali kuwa na uwezo wa kufanya tathmini ya faida za makampuni kwa mwaka na kulinganisha na michango yao katika kufanikisha maendeleo ya jamii inayowazunguka. Vilevile, CSR Act, itaiwezesha serikali iweze kuweka mikakati ya muda mrefu ili kuweza kuimarisha mahusiano baina ya makampuni na jamii kwa ujumla.
 
Mtatuambia pia tuuze mpunga wetu tununue madawati. Maajabu ya mungu. Serikali INA Nazi gani?
 
Rejea mada yangu viziri...wewe unaona ni sawa kutumia milioni kumi kwenye matangazo wakati kuna watoto wanakaa chini?halafu matangazo yenyewe yanamlenga mtu anayelala njaa?
Hakika wewe ni jingalao... Hivi unaelewa unachoandika kweli??
 
Nimejaribu kuangalia uwekezaji wa baadhi ya makampuni hasa haya makampuni ya simu nikaona kuwa yanatumia gharama kubwa sana.

Hii inanifanya nifikirie kuwa kuna umuhimu wa kuwa na regulatory body ya kufuatilia gharama hizi zinazotumiwa na makampuni kufanya matangazo ambayo hayana thamani na fedha inayorumika...

Ushauri wangu ni kuwa hizi fedha zinazotumika kwenye matangazo ni vyema zikaelekezwa kwenye ununuzi wa madawati ambapo tumeshuhudia kuna upungufu mkubwa.

Isitoshe makampuni haya yanawezekana kuwa yanatumia fedha nyingi sana katika matangazo badala ya kulipa kodi stahiki.

Hebu wabunge watunge sheria ya kudhibiti matumizi yasiyo na tija kwa makampuni haya ambayo yanalipa kodi kiduchu kulinganisha na wanachokipata.
Hivi ni lazima Wajinga kama hawa waanzishe thread humu?
 
Aisee hay madawati sasa yatatupeleka pabaya,kama kila kitu tukifanyacho watu wana waza madawati tu hii ni shida kubwa
 
Tusifute matangazo bali turegulate fedha inayotumika ilihali nchi hii ni yamasikini.

Inashangaza kuona tangazo la kampuni likiwa la bei ghali sana huku wizara ya afya ikipewa msaada wa matangazo na wamarekani.


KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA

pesa zao wewe zinakuuma nini?!
sasa itafika mahala mtatupangia idad ya bia za kunywa, gharama za msosi, aina na gharama ya simu,nk afu hela inayobaki tuchangie madawati!, hayo madawati si mchonge tu! si mliomba kuongoza sasa mnalialia nini?! kama hamuwez pisheni
 
Kuboreshwa kufikia kiwango cha kimataifa au kutengeneza matangazo bora? Listen, people invest money to design yale matangazo kwahiyo lazima uhakikishe una design catchy ads ili ku-grab attention!!

Na hiyo unayoita matangazo ya kila siku; ningekushauri jiongezee maarifa kwenye kitu kinachoitwa Product Life Cycle! And am telling you, endapo kampuni za kibiashara zingekuwa na namna ya kukwepa marketing basi wangeshukuru ile mbaya cuz' marketing ni very expensive sema ndo vile haikwepeki in competitive environment!!

Halafu hizo habari za madawati na hospital kukosa dawa zinawahusu nini business firms? Provision of social services ni purely kazi ya serikali lakini sio ya Tigo wala Vodacom! Serikali si wanakusanya kodi? Hata hayo mapesa mengi yanayotumika kwenye matangazo si yanaenda kwenye other business entities ambako pia serikali inakusanya kodi?! Sasa how come tena ionekane uhaini mimi kuwafikia wateja wengi niwezavyo kv tu wewe serikali ( don't take it personal) umeshindwa kutimiza wajibu wako wakati wajibu wa kwangu mimi wa kukulipa kodi nimeshautimiza! And probably, on top of that nina corporate social responsibility program na kujitwisha majukumu uliyotakiwa kufanya wewe! Kama kodi haitoshi, the smart way sio kuniambia ni namna gani niwafikie wateja wangu bali nI wajibu wako wewe mwenyewe na timu yako kubuni vyanzo vingi zaidi vya mapato!
Una utaalaamu kwenye hii field ...huko siji...labda nikuulize swali ...je ulisikia lile sakata la kuzimwa mtambo wa kutambua idadi ya miito au huduma za simu?

Ilionekana jambo hilo limefanyika makusudi ili kuidanganya serikali na hivyo kukwepa kodi.

Mada yangu inalenga huu ukwepaji kodi halafu tunashuhudia a lot of investment kwenye matangazo ambayo kwa maoni yangu hayana kiwango cha thamani inayolipiwa.

Ni kweli wajibu wa kwanza wa kuhakikisha madawati yapo shuleni unamuhusu serikali lakini pia wajibu huo upo kwa wadau mbalimbali makampuni haya yakiwemo....yaani makampuni haya yarudishe sehemu ya faida ya uwekezaji kwa jamii.
 
pesa zao wewe zinakuuma nini?!
sasa itafika mahala mtatupangia idad ya bia za kunywa, gharama za msosi, aina na gharama ya simu,nk afu hela inayobaki tuchangie madawati!, hayo madawati si mchonge tu! si mliomba kuongoza sasa mnalialia nini?! kama hamuwez pisheni
Leo siko kiitikadi mdogo wangu...niko kijamii zaidi
 
Aisee hay madawati sasa yatatupeleka pabaya,kama kila kitu tukifanyacho watu wana waza madawati tu hii ni shida kubwa
Madawati ni mfano mmojawapo au ulitaka niseme madawa?
 
Hawa walevi wa Lumumba sijui walienda shule kusomea ujinga? Tangu lini serikali ikaingilia uendeshaji wa kampuni binafsi?
 
Jingalao, kwa mtazamo wangu ni kwamba serikali inaweza ku-intervene kwa upande wa faida lakini, sidhani kama Serikali inaweza kuingilia expenditure ya makampuni binafsi (e.g. Tigo, Voda e.t.c) kwa namna yeyote ile....nasema hivi kwa sababu kuu mbili: Kwanza kabisa, Marketing/Advertising ni moja kati ya nguzo kubwa kabisa katika uwekezaji ambao unafanywa na kampuni hizi.....jitihada zao katika ku-advertise huduma au bidhaa wanazozalisha ndiyo zinawawezesha kushawishi wananchi waweze kuzifahamu, kuzipenda na hatimaye kutumia huduma/bidhaa za makampuni haya na hivyo ndivyo faida inavyopatikana......kwa ufupi ni kuwa, "The more these companies advertise their products or services, the higher the chances of attracting more customers hence high profit"....na ndiyo sababu unaona wanawekeza kiwango kikubwa cha fedha katika component hii ya Marketing.

Kwa upande mwingine, hizi kampuni ni entity ambazo zinajitegemea kwa kila kitu including namna wanavyopata mitaji na namna ya kusimamia na kuendesha shughuli zao; hata hivyo, kila kampuni inawiwa kuzingatia sheria katika operation zake zote.....na katika hili la kuzingatia sheria inajumuisha kulipa kodi (Ambayo ndiyo inapaswa kutumika na serikali katika kuhudumia wananchi wake katika elimu, afya, miundombinu e.t.c.), vilevile **kisheria kampuni hizi zinapaswa kukidhi their corporate social responsibility (e.g. Kujenga shule, kuchangia madawati, kuhudumia makundi yenye mahitaji maalum e.t.c.) kwa jamii inayozunguka maeneo huduma inapotolewa.

Kwa mantiki hiyo Serikali ina jukumu la kusimamia sheria na kuhakikisha kuwa kampuni hizi zinalipa kodi stahiki kwa wakati na pia kuhakikisha kuwa zinadumisha na kuchangia maendeleo ya jamii zilizo karibu na eneo huduma inapotolewa.

Hapa kwenye kui-enforce Corporate Social Responsibility (CSR) ya makampuni ndipo penye tatizo kwa sababu, hadi kufikia mwaka 2014, Tanzania haikuwa na sheria zozote ambazo zinaweza kutumika kuzibana hizi kampuni ili ziweze kuchangia maendeleo ya jamii zinazowazunguka. Uamuzi wa kuchangia ama kutokuchangia maendeleo ya jamii husika umeachwa mikononi mwa kampuni zenyewe. Kipindi cha nyuma kidogo (Kati ya 2014/15) kulikuwa na mazungumzo ya chinichini kuwa huenda serikali ikaanzisha sheria ya kusimamia CSR ili kuwezesha wananchi waweze kunufaika na uwepo wa kampuni hizi kwenye maeneo yao....hata hivyo sina updates zozote kuhusiana na hilo...wenye ufahamu zaidi kuhusu hatua iliyofikiwa na serikali katika mjadala wa kuanzisha Corporate Social Responsibility Act waje hapa watujuze zaidi.

Sheria hiyo ikiwepo, itaiwezesha serikali kuwa na uwezo wa kufanya tathmini ya faida za makampuni kwa mwaka na kulinganisha na michango yao katika kufanikisha maendeleo ya jamii inayowazunguka. Vilevile, CSR Act, itaiwezesha serikali iweze kuweka mikakati ya muda mrefu ili kuweza kuimarisha mahusiano baina ya makampuni na jamii kwa ujumla.
Mkuu umeitendea haki thread hii ...kwa upande wangu naona makampuni haya yamejikita kwenye adverts kwa kiasi kikubwa ili kuwafikia wananchi...ingawa kwa mazingira ya nchi yetu bado kuna jamii kubwa iliyoko vijijini ambayo haina mawasiliano....sasa jiulize kipi ni sahihi kimaendeleo ...je kuwekeza mamilioni ya fedha kuwafikia wa mjini pekee au mamilioni ya kuwafikia na wavijijini.

Naona kama vile makampuni haya yameiga uzungu sana ....na hajaweza kuiga huo uzungu na kuumodify kwa mazingira halisi ya kitanzania.

Kuhusu kurudisha faida kwa jamii inayowazunguka hapo ndipo ninapoona usanii kwani kampuni unakuta inatoa madawati 40 halafu ukiuliza utaambiwa ni michango ya wafanyakazi wao kutoka mifukoni...!!

Kama sheria ipo basi ihuishwe na kama haipo itungwe ikiwa na makali.
 
Back
Top Bottom