Matangazo CNN: Tumelala?

Mfalme

Member
May 11, 2009
14
0
Siku hizi naona sana kwenye CNN watani zetu (wakenya) na nchi nyingine za Afrika kama vile Angola na Afrika ya kusini wakijitangaza sana tu kwa matangazo waliyoyatayarisha maalum na mazuri sana kama lile Tangazo la "Malaysia truly Asia". Wakenya wanasema "The magic of Africa".
Sisi sijui viongozi wetu wanasubiri kudra za mwezimungu?.
 
Wanasubiri Nyerere aje atwambie kama kupata watalii ni lazima uitangaze nchi yako.

Maneno yako ni kweli TZ imelala, mie natokea visiwani hapo zama za kale nilidhani mlima Kilimanjaro uko Kenya jinsi tulivyolala jinsi na jinsi Kenya walivyoutangaza na kuingiza hela kibao kupitia mgongo wa mlima huo.

TZ haswa bado ina usingizi wa Nyerere, na sijuwi lini tutaamka...labda kiama :confused:

Maana mambo ni mengi ambayo tumelala, likiwemo na suala zima la kiswahili, TZ haitakiwi kutumia English mashuleni inatakiwa kutumia kiswahili...lakini iyo iko nje ya maada ....ooops:rolleyes:
 
Kuitanganza tanzania sio kupitia CNN tu mkuu.Kuna njia nyingi sana za kuitangaza mimi na wewe ndio hasa tuna paswa kuitangaza nchi yetu sio swala la kusubiria serikali ifanye hivyo.Wananchi Wakenya wamejitolea sana kuitangaza nchi yao kila kona ya dunia,kwa njia tofauti zikiwepo kwa njia ya Internet n'k...sasa sisi tunapo hiachia serikali kila kitu na kuitupia lawama lukuki kwamba imelala ingali sisi wanachi wenyewe ndiyo tulio lalal.



Bonyeza hapahttps://www.jamiiforums.com/habari-...tuitangaze-tanzania-yetu-kwenye-mitandao.html
 
wakiweka tangazo moja kwenye london taxi wanajipiga na picha wenyewe....
hizo hela zinatolewa na zinaliwa tuuu
wakenya wameanza kujitangaza siku nyingi na magical kenya, nilikua naona matangazo yao kwenye TV uk miaka 6 iliyopita
 
Nimemwona MiNISTER of tourism wa kenya leo on CNN..Yupo busy kuuza nchi yake!
sIKU ZA NYuma Iliniuma sana niliposikia for world cup 2010 kuna tourists watalala mauritius and will be jetted to and from the games...TANZANIA TUPOOOOOO???
 
Siku hizi naona sana kwenye CNN watani zetu (wakenya) na nchi nyingine za Afrika kama vile Angola na Afrika ya kusini wakijitangaza sana tu kwa matangazo waliyoyatayarisha maalum na mazuri sana kama lile Tangazo la "Malaysia truly Asia". Wakenya wanasema "The magic of Africa".
Sisi sijui viongozi wetu wanasubiri kudra za mwezimungu?.
Usiwe na wasi mkuu, jamaa nafikiri wanatafuta "muwekezaji" wa kutoa matangazo hayo, maana siku hizi ndio fashion serikalini.
Na atakapopatikana huyo "muwekezaji" si ajabu kupata madudu mengine kama ufisadi katika vitalu vya uwindaji
 
Wanasubiri Nyerere aje atwambie kama kupata watalii ni lazima uitangaze nchi yako.

Maneno yako ni kweli TZ imelala, mie natokea visiwani hapo zama za kale nilidhani mlima Kilimanjaro uko Kenya jinsi tulivyolala (sic nisivoelimika!)jinsi na jinsi Kenya walivyoutangaza na kuingiza hela kibao kupitia mgongo wa mlima huo.

TZ haswa bado ina usingizi wa Nyerere, na sijuwi lini tutaamka...labda kiama :confused:

Maana mambo ni mengi ambayo tumelala, likiwemo na suala zima la kiswahili, TZ haitakiwi kutumia English mashuleni inatakiwa kutumia kiswahili...lakini iyo iko nje ya maada ....ooops:rolleyes:

Mkuu ulisoma chini ya mwembe upi hadi kutojua elimu simple ya jiografia ya Tanzania
 
Kuna kipindi nilisikia kwamba serikali imetenga fungu la pesa kwa jili ya matangazo CNN,na kwa kuanza walianzia na CNN local (abayo inaonekana marekani tu) sijui imekuwaje mpaka leo wameshindwa kuyatangaza upande wa CNN International,ambayo ndio inatizamwa na dunia nzima.
 
Matangazo yaongeza watalii nchini
habarileo
Oscar Mbuza

Wednesday,July 02, 2008 @00:04

Idadi ya watalii wanaotembelea Tanzania inaongezeka siku hadi siku kutokana na Mkakati wa serikali kujitangaza kupitia vyombo vya habari vya kimataifa kama Kituo cha Televisheni cha CNN na magazeti ya Marekani.

Ofisa Mfawidhi wa Idara ya Utalii katika Wizara ya Maliasili na Utalii, Philip Chitaunga, aliyasema hayo jana kwenye Maonyesho ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam.

Chitaunga alisema mkakati wa serikali wa kuvitumia vyombo vya habari vya Marekani, umefanya watalii wengi kutoka Marekani kuja nchini kutembelea maeneo mbalimbali ya kitalii. "Zamani watalii wengi walikuwa wanatoka Uingereza lakini sasa soko la utalii limebadilika na watalii wengi sasa wanatoka Marekani," alisema Chitaunga.

Katika hatua nyingine, alisema pamoja na nia ya Tanzania ya kuongeza idadi ya hoteli za kitalii ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, lakini mpango huo unafanyika wakati kuna tahadhari muhimu kuhusu mazingira na uhai wa wanyama.

Alisema ingawa Tanzania imepania kuona Hifadhi ya Serengeti inakuwa na hoteli nyingi za kitalii kama ilivyo kwa upande wa pili wa Mbuga ya Masai Mara nchini Kenya, ili kuongeza mapato yatokanayo na utalii, lakini suala la mazingira halijafumbiwa macho.

"Lengo letu ni kuwa na watalii wachache watakaotuingizia fedha nyingi na si kuwa na watalii wengi kupita uwezo wetu wa kuweza kuwahudumia kwa viwango vinavyotakiwa," alisema. Alisema mkakati uliopo hivi sasa ni kutangaza utalii wa asili utakaoiwezesha Tanzania kuwa na utalii wa aina tofauti na hivyo kuwafanya watalii kuona ulazima wa kuja kujionea utalii huu.
imepita mwaka sasa tangu nilipo soma hii habari.
 
Dhana kuu ya fikra zangu, iko katika namna tunavyoweza kutumia rasilimali yetu ya uwanja mpya wa michezo uliopo jijini Dar es Salaam kwa manufaa ya kuendeleza utalii nchini.
Hapana shaka katika ukanda huu waAfrika Mashariki, uwanja huu ni mkubwa na unastahili kutumika kwa hadhi inayostahili kuvuta utalii. Kwa maana hiyo tulicho nacho ni mali.
Naamini tukioanisha suala la michuano ya kombe la dunia kufanyika nchini Afrika Kusini, zipo timu za soka zitakazofika nchini kufanya mazoezi na watakapokuwa humu watabaini vivutio vilivyopo.
Cha muhimu kwa wadau wa michezo wa kigeni watakapofika nchini kufanya mazoezi kwa ajili ya maandalizi ya michuano hiyo ya kombe la dunia ambayo iko usoni, tunahitaji kuwekeza mikakati yetu humo humo nasi tufaidike.
Kama ilivyokuwa katika mkutano wa Sullivan uliofanyika mjini Arusha mwaka huu, nasi tulitakiwa kuelekeza mikakati kwa wageni hawa wanaofika kufanya mazoezi nchini, kuhakikisha tunapata faida ya kujitangaza katika utalii.
Sasa hivi si haba. Nilifurahi nilipomsikia Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, alipotamka Bungeni kwamba juhudi za kujitangaza zimechukua sura ya mafanikio.
Mfano mojawapo aliyoutoa ni kwamba, nchini Marekani vivutio vya kitalii vimetangazwa katika televisheni maarufu ya CNN na matokeo yake yanaonekana, kwamba kuna watalii wengi wanaomiminika kutoka huko.
Nionavyo, hiyo ndio namna hata kwa wageni watakaofika kufanya mazoezi katika viwanja vyetu kwa ajili ya michuano ya kombe la dunia, mambo ya namna hiyo tutayashuhudia na utalii wetu ukawa na manufaa kwetu sote.
Inastahili sasa hivi wadau wakakuna ubongo juu ya aina gani mikakati wanayopaswa kuweka na aina yote ya fursa zilizoko kutumika na hatimaye hatua iliyopigwa ionekane.
Hebu tuthubutu ili tuweze.
 
Back
Top Bottom