Hata sijachagua maswali ya kukujibu, ngoja niendelee...
- Nchi inakuwa chini ya uongozi wa VP, hili lipo kikatiba.
- Katiba inazungumzia pale Rais anapokuwa nje ya nchi, kwa shughuli za kikazi, ugonjwa au vinginevyo, Makamu wake ndie anashika hatamu. Au ulitaka Katiba iseme kitu kuhusu VP kutopewa taarifa za ugonjwa wa Hayati JPM?!
Nani kati yenu mwenye uhakika kama VP hakuwa anafahamu chochote kuhusu hali ya ugonjwa wa Hayati JPM, narudia tena zipo njia nyingine za mawasiliano kufikisha ujumbe kwa mhusika, wakati ambao Mabeyo hakuwepo, ndio maana nasisitiza mwenye jibu la mwisho kuhusu hili, ni Samia pekee.
Mabeyo kazungumzia aliyoyaona mwenyewe, mengine yaongelewe na wengine. Naamini hata PM nae akiulizwa kuhusu hili jambo atakuja na part yake tofauti ambayo Mabeyo hakuigusa, hivyo hivyo kwa VP na wengine.
- Suala la waratibu, hao mbona wanaonekana wazi, ukianza na Mabeyo mwenyewe kwa cheo chake, PM Majaliwa, waliokuwa eneo la tukio, na viongozi wengine serikalini inawezekana walishirikishwa kwa mbali, wasingeweza wote kujazana kwenye chumba cha mgonjwa.
- Uwepo wa Dr. Janabi eneo la tukio pia nimekwambia inaweza kuwa ni ushauri wake kitaalamu ndio uliohitajika eneo husika, kama hata Dr. binafsi wa Hayati Magufuli humfahamu mpaka unaniuliza ni nani hasa, mimi siwezi kukupa jibu kwasababu hata nami sikuwa namfahamu.
• Hapa nakushangaa, kama hukuwa ukimfahamu daktari wa Hayati Magufuli, kwanini ushangae kutokuwepo kwake?!
• Mtu ambaye hata hukuwa ukimfahamu, unaulizia vipi uwajibikaji wake?!
Hata kuhusu kifo cha kijana wa Mabeyo kwenye ajali { sikumbuki kilitokea wakati gani}, napo sioni cha kushangaza, hakuna karma pale; ni nani kati yetu asiyekufa? au wewe ndie hupanga nani afe lini? mimi sioni uzito wowote wa hoja zako.