Bush Dokta
JF-Expert Member
- Apr 11, 2023
- 40,385
- 69,115
Achana na speculations wewe fata Taarifa rasmi zilizotolesa na serikali.Hatimae tumemsikia na kumshuhudia aliekuwa Chief of Defense Forces kupitia media na mtu ambae inaonekana ndie alikuwa kiongozi wa nchi kwa muda wa siku zote Marehemu JPM akiwa anapigania uhai wake na hatimae kuondoka Duniani!
Lakini maelezo yake yameongeza sintofahamu zaidi kuliko alivyotarajia!
Na kwa wengine hasa mimi binafsi....
Sasa nimeelewa maana ya "karma"
Muda mfupi baadae mtoto wa kiume wa Mabeyo aliekuwa Pilot pale Coastal Aviation alianguka na ndege uwanja wa Seronera akiwa yeye na rubani mwanafunzi wa vitendo (trainee) na wote walifariki Dunia.
Hili kwa sasa sintaliongelea sana ila nimeliweka hapa ili kuonyesha ukuu wa Mungu na Malipo yake kwa wale anaotaka kuwapa majibu ya matendo yao wakiwa bado hai.
Na wakati mjadala ukiendelea kuhusu mambo kadhaa ya kisiasa kutoka na hotuba ya Mstaafu Mabeyo!
Sisi wengine tunajiuliza....
Swali muhimu!
Ni kwa nini walituficha ugonjwa wa mpendwa Rais wetu JPM?
Tunajiuliza ...
Dk Janabi alikuwa pale muda wote akifanya nini ilhali yeye hakuwahi kuwa Daktari wa JPM,bali alikuwa ni Daktari wa familia ya Kikwete na pia swahiba ya JK?
Tunajiuliza ...ni kwa nini walikwenda kumficha pale Mzena badala ya kumpeleka kwenye hospitali nyingine yenye hadhi ikiwezekana hata nje ya nchi?
Tunajiuliza .... kama waziri mkuu alituficha!,Makamu wa Rais alituficha!
Ni nani au kikundi gani kilikuwa kinaratibu haya mambo?
Tunajiuliza....
Kama Mkuu wa majeshi aliambiwa na JPM awali kwamba wamrudishe nyumbani akafie huko.Ni kwa nini aligoma kutimiza takwa la Marehemu?
Na kwa nini hakuwashirikisha wengine ili wachukuwe maamuzi sahihi?
Je!
Magufuli aliugua ugonjwa gani huo ambao madaktari walikaa pembeni wakimshuhudia akipigania uhai wake akiwa kama mateka?Anasema alipofariki wao wakuu wa vyombo ndio waliwajulisha viongozi kama PM, CS na baadae makamu wa rais.. Tena wote hawakuwepo eneo la tukio...
Hatuoni mahala makamo wa Rais,mwanasheria mkuu, Wala jaji mkuu au spika wakiwa na maamuzi yeyote. Kila kitu kilipangwa na jeshi.
Huyu Mabeyo ameongea....
Iko siku na wengine wataanza kuongea!
Damu ya mtu huwa haipotei bure....
Kama kuna jambo lilipangwa na kufanywa na kikundi fulani,kinyume na tulivyoamishwa sisi wananchi!
Na kwa jinsi siku ya Jana ilivyopita bila hata serikali ya Saa100 kujishughulisha na lolote kuhusu kumbukumbu hii muhimu nchini.
Tutashuhudia taraatiiibu!
R.I.P Jemedari JPM!
Wameanza kuropoka huku!
Unaongelea Karma? Wewe voicer ndio umejua Karma leo?