Kaka, nipo. I mean, just letting you know kwamba nipo mtaa huu.
Haya, napita.
...ha ha ha.... nimeipenda hiyo 'abiria chunga mzigo wako'
...lolz....awakening The Kundalini ni sawa na stimulating to the max the The Gräfenberg Spot....yaani, unaweza mfanya mtu akamkumbuka mpaka "babu mzaa bibi yake!.."
Nasikia kuna massage ya kiungo kimoja kimoja, mwenye kujua atuhabarishe....
Yaani Mbu, entorage yangu kawaida ina 'mabodyguard' wasiopungua 20 hapa.....hakuna kufurukuta wala kusogelewa lol
Hehehehe Mbu bwana!!
Ndio hapo watu wataanza "ohhh fulani kapewa libwata, ye weekend yote nyumbani mwanaume gani yule.". . . kumbe mwenzao anapata ile kitu roho inapenda kwa namna ya kipekee!!
@Lizzy, nakutizama tu na huyu jg.
Nimefunga mdomo hadi arudi.
jG anataka massage TU. . . lolz!!
Sasa ruhusa unatoa au. . . . ?
lolz,...you crack me up!...nishaanza kusahau hivi vitu, si unajua maudhi maudhi ya kila siku [ndani ya nyumba] hata hamu ya ku practice inapotea? Sshhhh...natafuta volunteer...
LOL Naona Mule mule tu....sasa hebu nitafutie BJ alipo anijibu msg yangu apo juu, Kingasti nimemtuma 'dukani' na bunduki kaniachia....
Sure thing.
Ila namna mtu aliyojitayarisha kiakili ndio itaamua vipi mwili wake utarespond.
lolz,...you crack me up!...nishaanza kusahau hivi vitu, si unajua maudhi maudhi ya kila siku [ndani ya nyumba] hata hamu ya ku practice inapotea? Sshhhh...natafuta volunteer...
Hahahaa!!
Alafu kabla ya kutafuta ujiandae kabisa kuhamia maana waweza jikuta unasahau kua una kwako. Na taarifa utoe kabla hujarepotiwa umepotea. . lolz
Hhhmmm umeelewa nini?
Hehehehe we hushangai wenzako hua wanajenga na kujenga wakati mkewe bado anapanda daladala ye akiwa mbali na gari? Ndio ujue sasa. . . . mwanaume kubembelezwa kwa maneno, mikono na matendo laini babu wee!!Lolz....dahhh, mbona unan'tisha tena....
siri ya nyumba ndogo karibu itatoka hadharani,...
kunogewa mwiko!
Massage inaweza kutumika kumsaidia mtu kukabiliana na maumivu ya mwili (misuli mostly), relieve tension na kumfanya a-relax pia inaweza ikatumika kumsisimua mtu.
Kama nia ni kuondoa maumivu ya misuli ni vizuri zaidi ukatumia kitaulo na maji ya moto kiasi kumkanda badala ya mikono mikavu. Kwa nia ya kumfanya mtu arelax/asisimke tumia mafuta ya maji(yaweza kuwa brand yoyote ile, just make sure mhusika sio alergic na hicho kilochotumika kutengeneza hayo mafuta) yaliyopashwa kidogo.Sio yawe ya moto kiasi cha mwenzio kulalamika au wewe kuungua mikono bali kiasi tu.
Msihi mwenzako atulie na ujitahidi kuwa gentle. . usitumie nguvu.
Anza kwa kuweka mafuta mkononi alafu fikicha kidogo ili usimpake yakiwa na moto. Anzia shingoni kupaka mafuta taratiibu kisha shuka mpaka mabegani. Mkande kande na kumsugua taratibu shingoni, bega la kushoto na kulia alafu katikati. Rudia tena mara tatu huku ukiongeza pressure kila mara so you can get through those sore muscles if he/she has any.
Baada ya hapo paka mafuta mgongoni all the way mpaka kiunoni. Alafu anza kummassage mgongoni. . taratiiiibu on the sides na katikati huku ukiteremka taratibu mpaka kiunoni. Hapo waweza tulia for a few seconds alafu kama hutaki kumgusa vile chora mstari wa zig zag katikati ya mgongo wake three- four times. . .Down,Up and Down again.
Anza tena kumkanda toka chini kuelekea juu, huku pressure nayo ikiongezeka. Ile sehemu ya katikati yenyewe ibinye na vidole gumba vyote viwili kwa pamoja. Baada ya kurudia hiyo mara tatu,nne unganisha kwanzia shingoni mpaka kiunoni.
Next inama kidogo kwahiyo ukipumua anakua anahisi pumzi yako and you can smell the scent of his/her skin wakati unammassage upande wa juu wa mikono yake gently . . . Ukiinuka hapo teremka chini kabisa, piga magoti katikati ya miguu yake ili ummassage kwenye mapaja kidogo na miguuni.
Mpaka hapo mwili utakua umesharelax ila bado sehemu moja muhimu. Wewe ndo unakua mto wake. Kichwa chake anakiegemeza kwenye mabega yako, shingo zinakutana alafu unammassage kifuani gently.
Mahusiano yanaendeshwa kwa ushirikiano. . . usiwe mbinafsi.