Massage Parlours/madanguro

Massage Parlours/madanguro

uporoto01

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2008
Posts
4,698
Reaction score
1,428
Wiki iliopita nilianza kuumwa mgongo na nikashauriwa na rafiki yangu nikafanyiwe massage itasaidia.Nikaenda kwenye massage moja iliopo namanga.

Baada ya kunifanyia massage yule msichana akaniambia wanatoa huduma ingine pia. Nikamuuliza huduma gani? Akasema ngono kwa elfu 20,kwahiyo massage 20 na ngono 20.Nikamwambia nina dozi ya malaria labda siku nyingine.

Jioni tukiwa kisimani [bar] nikawaambia wenzangu kisa kile, wakasema mbona ndio kawaida ya massage zote za dar. Nikaambiwa massage nyingi za Sinza, Kijitonyama, Kinondoni, Namanga, Msasani hata kwenye sehemu za mazoezi na hoteli kubwa hii extra baada ya massage ipo na tafauti inakua katika bei tu.
 
Hiyo si biashara kama biashara nyingine tu hao wamesajiliwa na wanalipa kodi kodi hiyo inasemesha watoto zako an babu zako huko vijijini na kuwajengea zahanati na barabara na kuboresha maisha yao tuache kuwanyanyasa watu hawa tuwaache wafanye kazi zao kwa uhuru
 
Mi wala sipingi utoaji wa huduma hii na hapa nilikua nawajulisha wale waliopinga sana utambuaji wa ukahaba kama huduma nyingine.Hawa wakina dada wameona mahitaji ya huduma hii na kuamua kuitoa.
 
Mara nyingi Massage Parlours huwa na huduma ya ziada na hasa huwa kupigishwa ngunga, hii nimeona sehemu nyingi.. lakini huduma yoyote ya ziada katika sehemu hizo mara nyingi huwa ni kati ya mwajili na mwajiliwa. Hivyo basi ni biashara haramu na inayokwenda kinyume na leseni. Serikali inajua hilo lakini inafumbia macho au inachelea kuchuka hatua yoyote ama kutokana na ugumu wa maisha na sababu zingine wazijuazo.

Cha msingi huu unaweza kuwa Mwanzo wa kurudi kwa madanguro yanayotambuliwa na serikali.
 
Last edited:
Haya ni maendeleo pia wanatakiwa wapewe leseni zao na wafanye kazi hii kwa haki kabisa kama wengine wote na wawe na vyama vyao tuweze kuwatambua kabisa hakuna kulala mpaka kieleweke .
 
Hiyo si biashara kama biashara nyingine tu hao wamesajiliwa na wanalipa kodi kodi hiyo inasemesha watoto zako an babu zako huko vijijini na kuwajengea zahanati na barabara na kuboresha maisha yao tuache kuwanyanyasa watu hawa tuwaache wafanye kazi zao kwa uhuru

Maneno haya kutoka kwako SHY?Unamaanisha ukahaba ni biashara kama biashara nyingine?Massage parlours hazijasajiliwa kutoa huduma za danguro (in fact sheria zinakataza baishara za madanguro) bali kutoa huduma hiyo ya massaging.Pia sidhani kama mtoa hoja ameonyesha dalili ya kuwanyanyasa watu hawa bali ameonyesha mshangao,na kila mtu mwenye busara zake anapaswa kufanya hivyo.
 
Mlalahoi kuna biashara inaitwa ukahaba kila mtu amebariki hilo hata viongozi wa dini serikali wanajua wao ndio wateja wakubwa wa hawa makahaba kila sehemu wapo tumezoea kuwaona wengine wako na ndoa zao ila ndoa zinatunzwa na kazi hii ya ukahaba kwanini tusiuhalalishe basi watalipa kodi na mambo mengine watatambulika watakuwa na saccoss zao na vyama vingine vingi
 
Tatizo makahaba wengi hawajasoma na wapweke lakini wengi wangekuwa na elimu zao nzuri naamini wangeandika kitu kuhusu kuhalalishwa biashara yao hii -- tuwatambue hawa ni binadamu kama sisi jamani
 
ndoa zinatunzwa na .kazi hii ya ukahaba kwanini tusiuhalalishe basi watalipa kodi na mambo mengine watatambulika watakuwa na saccoss zao na vyama vingine vingi

Tafadhali fafanua kwa faida ya wasomaji! HUU NI MSEMO MZITO SANA
 
Nimesema kuna watu wako katika ndoa na wake zao ni makahaba mjini hapa wanajulikana -- kwahiyo wanatunza ndoa hizo kwa kipato wanachojipatia pamoja na kuendesha mambo mengine katika maisha yao wao wenyewe .

Siku moja niliwahi kuona watu wanandoa wanagombana mwanamke akamwambia mwanaume mimi nauza k.. Ili wewe uishi mjini hapa na unajua hilo
 
Sema katika makahaba kuna grades zinazojulikana mimi huwezi kunipeleka kinondoni makaburini wakati hadhi yangu ni new afrika , hata ukienda hapo new afrika ukigonga tu muulize yule mhudumu wadada wazuri wako wapi atakupa namba ya simu au atakuelekeza atakapo kuwa muda huo uende

so kuna wanaojiuza njiani , wengine wako majumbani hawa ni self service wako wengi katika mitandao kama katika jukwaa la mapenzi tunawajua na aina mbali mbali
 
Sasa mbona jina la Parlour umelibana??! Tutajuaje pa kwenda? lol!
 
Kitu ambacho kiliniumiza nilipoingia kuna mwanafunzi wa kike[secondari]alievaa unifomu alikua amekaa na wahudumu,nilipotoka akawa amebadilisha nguo na amekaa pale pale. Sasa sijui kama nae alikua anabangaiza pale,ni hatari tupu.
 
wengine kweli ni wanafunzi lakini wenginepia wanatumia nguo za wanafunzi kuonyesha kwamba wao wabichi wanafaa ili kuvutia wateja si unajua tena wanafunzi na nini
 
Mlalahoi kuna biashara inaitwa ukahaba kila mtu amebariki hilo hata viongozi wa dini serikali wanajua wao ndio wateja wakubwa wa hawa makahaba kila sehemu wapo tumezoea kuwaona wengine wako na ndoa zao ila ndoa zinatunzwa na kazi hii ya ukahaba kwanini tusiuhalalishe basi watalipa kodi na mambo mengine watatambulika watakuwa na saccoss zao na vyama vingine vingi

Overgeneralization ni hatari katika kujenga hoja.Unaposema KILA MTU amebariki ukahaba,nashindwa kukuelewa.Labda useme baadhi ya watu (wengi au kidogo,inategemea mtazamo) wamebariki ukahaba kutokana na ushiriki wao kwenye shughuli hiyo (makahaba wenyewe,pimps,watumia huduma hiyo,etc).Na washiriki pia wanaweza kugawanywa katika makundi ya wanaofanya hivyo kutokana na sababu za kiuchumi na wale wanaofanya kwa starehe zao.

Ukisema "hata viongozi wa dini wanajua hilo" basi hata ufisadi,ujambazi,utumiaji madawa ya kulevya,ulawiti,na madhambi yooote tunayoyajua pia yanajulikana kwa viongozi wa dini.But,kujulikana hakumaanishi kuhalalisha.Kujua kwamba kuna ufisadi Tanzania hakumaanishi kuhalalisha ufisadi.Na kujua kuwa kuna kuna watu wanaua maalbino hakumaanishi kuhalalisha vifo vya maalbino.Kimsingi,viongozi wa dini wanapaswa kujua kuhusu madhambi kama ukahaba ili waweze kuwaongoza waumini wao ipasavyo.Kujua huko hakumaanishi kuhalalisha dhambi hiyo.Usafi au uchafu wa viongozi hao ni suala tofauti na halihusiani na sifa stahili za kiongozi wa dini.Baadhi ya viongozi wa dini kuwa wateja wa makahaba hakumaanishi kuwa dini inaruhusu ukahaba,just like kukithiri kwa rushwa Tanzania hakumaanishi kuwa rushwa ni halali.

Again,kuwepo kwa makahaba kila sehemu hakumaanishi kuwa ukahaba ni halali just like kuwepo kwa ukimwi duniani kote hakumaanishi kuwa ukiwmi sasa si ugonjwa.Au kuwepo wa biashara ya unga takriban kila kona ya dunia hakumaanishi kuwa biashara hiyo ni halali.Same could be saidi about kutapakaa kwa ujambazi,rushwa,ubaguzi wa rangi,utumikishwaji wa watoto,na maovu mengine katika jamii.Yapo takriban kila sehemu,lakini hiyo sio sababu ya maovu hayo kuwa halali.Uhalali wa kitu sio kutapakaa au kuenea kwake bali kuendana na mila,desturi,sheria na taratibu za jamii husika.

Ukahaba unawawezesha makahaba kutunza familia zao,lakini hata ufisadi nao unawawezesha watu kutunza familia zao,so does ujambazi,biashara ya madawa ya kulevya,utapeli,ukabaji,nk.Je hivyo navyo vihalalishwe kwa vile tu vinawawezesha watu kutunza familia zao?

Na tukishawatambua makahaba kisha tukawatoza kodi,what about hao watenda maovu wengine katika jamii?
 
wengine kweli ni wanafunzi lakini wenginepia wanatumia nguo za wanafunzi kuonyesha kwamba wao wabichi wanafaa ili kuvutia wateja si unajua tena wanafunzi na nini

Its mind bogling that school kids may be used this way.
 
Pole sana,kama umekwenda kwenye massage parlor,siku nyingine watakuteka kwenye danguro.Rafiki huyo sio rafiki mwema.Dawa ya tatizo lako ni mazoezi ya kutosha, wala sio massage.
 
Back
Top Bottom