Masoud Kipanya alimaanisha nini kwenye mchoro huu?

To me: Hilo skeleton ni MZEE(r.i.p)
Draft ni serikali
Kete ni utawala
Mwanamke ni huyu()
Hilo jipu mkononi mwa Mwanamke
NI MATATIZO YA KIUTAWALA
GLASS ya wine(damu zilizomwagika
Kuna mzee hapa jirani yangu ananikata jicho na anamwonekano wa kikauzu ngoja niishie hapa kwanza....
 
Umesema kweli mkuu, huyu jamaa amepoteza mwelekeo, kazi iliyo baki ni kukashifu na kudhihaki, nadhani hii yote ni njaa, anaona bila kuchora katuni za kukashifu na kudhihaki hawezi kupata mafao ya kutosha.
sasa atajimaliza mwenyewe
mbona mnachachamaa vipi?
 
Nimeona mchoro huu nikajiuliza aliwaza nini kabla ya mdau kutoa ufafanuzi wake, Kama iko vivyo mdau alivyosema basi Kipanya ametukosea Sana watanzania, mtu akifa aachwe afe.

Kusema Samaia anajifunza ya JPM ni kukosea sana hasa ukisema anajifunza mabaya tu.

USSRView attachment 1959093
Kweli Kipanya ni akili kubwa sana! Hapa ni kuwa Rais Samia amewafufua wanyonya damu (wapigaji) walikuwa wameshakufa na kuoza (baki mifupa) na sasa kupitia kofia ya CCM wameanza kula maisha (vuta sigara na kunywa nao jasho la Watanzania/ damu kwenye glass) ! Rejea teuzi za January Makamba na Bodi ya ajabu ya TANESCO ambayo January amejaza " wapigaji" ambao Rais Magufuli alishawamaliza kabisa!
 
Wengi hamjaiona hiyo bangi kwenye draft upande wa huyo mwenye "SILAHA"

Hii picha ni kubwa sana, ukimsikiliza Gentamycine hapo juu "UNAPOTEA"

MUNGU Mwenyezi na ATUSAMEHE.
 
Binafsi nmekuwa mfatiliaji wa Katuni au Vikaragosi vya Mchora katuni Nguli pengine wa Muda wote hapa Tanzania. Kikaragosi akiongeii ila utoa taarifa fulani juu ya kitu. Kama zilivyo kazi ngingine za Sanaa Vikaragosi pia uburudisha na kufkirisha sana.

Hivyo kulingana na Unyeti wa Kazi hizi za huyu bwana mkubwa kumekuwepo na hali ya baadhi ya wanajamii kufungua nyuzi nyingi za kuongeleaa katuni au vikaragosi vya Masoud maarufu kama Kipanya.

Nimeona ni busara sasa tuwe na uzi ambao utakuwa ni mkusanyiko wa vikaragosi vya Masoud ilii kutoa nafasi ya kujadili kwa pamoja ni ujumbe gani ulikusudiwa na mtunzi na mchoraji wa Vikaragosi hivii.

Vikaragosii hivii utokaa kwenye gazeti la Mwananchi au kwenye kurasa rasmi za mitandao ya kijamii ya Masoudii....



Kwa kuanzia sasa ebu wanajamvii tuwaze hapa Kipanya alimaanisha nini.... KaribuniiView attachment 1959256

Modes msiunganishe huu huziii
Hapo Yanga na simba wanashindania makombe na pia hilo skeleton ni ile kesi iko CAS wakati wowote kinalipuka .
 
Hii ni katuni bora kabisa so far kutoka kwa Kipanya.

Natumaini kuna mahali anaandika na kutunza tafsiri zake za katuni anazochora. - Na anafuatilia juhudi za wadau wanaojitahidi kutoa tafsiri za kazi zake.
 
Kweli Kipanya ni akili kubwa sana! Hapa ni kuwa Rais Samia amewafufua wanyonya damu (wapigaji) walikuwa wameshakufa na kuoza (baki mifupa) na sasa kupitia kofia ya CCM wameanza kula maisha (vuta sigara na kunywa nao jasho la Watanzania/ damu kwenye glass) ! Rejea teuzi za January Makamba na Bodi ya ajabu ya TANESCO ambayo January amejaza " wapigaji" ambao Rais Magufuli alishawamaliza kabisa!
Kuna wanywa damu zaidi ya ccm ya 2015-2021?
 
Kuna makundi mawili ya CCM yaani ile ya sukuma gang ambayo inawakilishwa na kofia na headphone, kofia imepauka ikiwa na rangi ya kijani na mistari miwili ya njano kuonesha ni CCM inayoendelea kuamini falsafa za mwendazake,ile headphone inasadifu tabia ya mwendazake kuongoza kwa mkono wa damu na bila kusikiliza ushauri wa yeyote yule na ile inayovutwa ni bange ikionesha ubabe ubabe na ukosefu wa hekima na subra na ile bunduki ni mkonowa chuma.Lile draft linaonesha kuwa wote wawili yaani chief hangaya na mwendazake wanatumia CCM ambacho ni chama chao kuendelea kuitawala Tanzania bila kujali maslahi ya taifa bali ya CCM. Na ile glasi ambayo iko juu ya drafti upande wa mwendazake inaonesha jinsi utawala ule ulivyokuwa wa mabavu na hatimaye ukaishia njiani ndio maana glasi imepasuka.Zile kete tatu ni mambo matatu yaliyoitesa awamu ya tano ndio yanaendela kwa awamu ya sita kwa maana ya Katiba mpya,makundi ndani ya CCM na uwanja huru wa kuendesha siasa. Zamu ya mwendazake iliisha ndio maana unamuona chief Hangaya akifikiria acheze vipi kete ili ashinde game. Kipanya anashangaa na yanayoendelea ila yuko upande wa mama.
Naungana na wewe..nimetafsiri hivi pia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mama anacheza panga, pangua kuitokomeza Kambi ya marehemu mwendazake wakati hiyo Kambi haipo tena, ilibadirika na kuwa kitu kingine....
Chama kipya cha siasa chenye kumuenzi mbabe wa fitina za Tanzania soon kinakuja!

Chama kipya? Kitachukuaje mamlaka ya dola (polisi, jw, tiss, magereza, uhamiaji, Hazina/BOT) toka kwa CCM? Kitapindua nchi?

Bila hivyo kitaishia kuwa kama TLP au UDP.

Jeuri ya mbabe wa fitna iliwezeshwa na nyenzo za dola zinazomilikiwa na CCM. Bila hizo, nje ya CCM, angekuwa kama Mrema au Cheyo.
 
Nimtishe namuelekeza,kama ana ndugu wanampenda wamwambie,asije sema hakuambiwa,uhuru usitumike kuvuka mipaka

Ungekuwa unamfahamu kipanya, usingepoteza muda kumtolea kitisho cha aina yoyote. Ukiona katuni zake hazikufurahishi, just ignore him.
 
Ilo skeretoni ni rahisi kulihusisha na JPM cos alishafariki laiki ukitoa ilo hakuna kitu kingine ambacho unaweza kukihusisha na JPM hapo! Binafsi naona Mama yuko na Mafia fulani ndani ya chama chao.
Ni uyo uyo Jiwe.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom