Masikini Zitto Kabwe, umesahaulika kabisa

Masikini Zitto Kabwe, umesahaulika kabisa

Kwa mwana siasa au mfuatliaji wa siasa za hapa Tanzania jina la ZZK lilikuwa ni maarufu sana kupitia vyombo vya habari ikiwepo mitandao ya kijamii kipindi ZZK yupo ndani ya CHADEMA kwa kufuatilia mawazo na ushauri wake.

Lakini kwa sasa baada ya kuwa nje ya CHADEMA hatupati tena mawazo na ushauri wa aliyekuwa mwanasiasa mahiri mwenye hoja murua, nini kimekupata ZZK?

We uko bize kukusanya bodaboda wa kuchangamsha msafara wa huyo mzee ,,, utajuaje kinachoendelea kingine?
 
We uko bize kukusanya bodaboda wa kuchangamsha msafara wa huyo mzee ,,, utajuaje kinachoendelea kingine?

Kwakweli sijui kingine zaidi ya kuzomewa na kupopolewa kwa mawe kama vile tunduma,sumbawanga,geita,bukoba na juzi iringa na shinyanga kwa viongozi wenzake walivyo amua kuporomosha machozi mkutanoni
 
We uko bize kukusanya bodaboda wa kuchangamsha msafara wa huyo mzee ,,, utajuaje kinachoendelea kingine?

Wewe vipi ndiyo yule afande hasiyejua kutumia kompyuta msaidizi wa zzk?
 
Unajikuta unahangaika kumchafua ZZK huku yeye anahangaika kuimarisha chama chake,,,,,,na humkuti kuwazungumzia cdm kama nyie msivopumua kumzungumzia.

Nenda kwenye acc zake za fb utaona
 
Vipi unataka umfuate Makongoro Bro wako?
Njoo UKAWA tutakuweka sawa at least muenzi legacy ya Baba wa Taifa sababu mnamdhalilisha Baba wa Taifa kwa kuendelea kushabikia ccm.

Atakuelewa huyo,
 
Yupo anawinda na mawindo yake yaliangukia kwa Abwao akaona amepata bonge la mbunge
 
KABWE yuko shambani bado analima utamuona akiingia sokoni tulia kaka

Mwaka huu act itabidi warudishe mshiko wa ccm maana wameshindwa kazi waliyopewa
 
Unauhakiaka gani na hilo wale wako na ujenzi wao au ubabaishaji?
 
Kwa mwana siasa au mfuatliaji wa siasa za hapa Tanzania jina la ZZK lilikuwa ni maarufu sana kupitia vyombo vya habari ikiwepo mitandao ya kijamii kipindi ZZK yupo ndani ya CHADEMA kwa kufuatilia mawazo na ushauri wake.

Lakini kwa sasa baada ya kuwa nje ya CHADEMA hatupati tena mawazo na ushauri wa aliyekuwa mwanasiasa mahiri mwenye hoja murua, nini kimekupata ZZK?

Wahanga wa maamuzi ya mbowe wako wengi,
huyo zito bora yeye yupo hai kisiasa,
mbona humuzungumzii huyu katibu mkuu wa cdm dr slaa,Raisi wa mioyo yetu kaambiwa akae kimya asithubutu kuongea chochote.
Siasa ngumu sana.
 
Wahanga wa maamuzi ya mbowe wako wengi,
huyo zito bora yeye yupo hai kisiasa,
mbona humuzungumzii huyu katibu mkuu wa cdm dr slaa,Raisi wa mioyo yetu kaambiwa akae kimya asithubutu kuongea chochote.
Siasa ngumu sana.

Wewe ulifikiri siasa ni lelemama?
 
Wewe ulifikiri siasa ni lelemama?

Bado wewe kama unafuatilia siasa au ni mwanasiasa mwenye wadhifa au unatarajia kugombea nafasi yoyote kisiasa unawezajikuta unapotea hata jf ukaiona kama kituo cha police.
 
Bado wewe kama unafuatilia siasa au ni mwanasiasa mwenye wadhifa au unatarajia kugombea nafasi yoyote kisiasa unawezajikuta unapotea hata jf ukaiona kama kituo cha police.

Siasa ni mojawapo ya burudani ya moyo kama ilivyo soka ili mradi ujue kucheza
 
Tatizo la ZZK ni kutaka kuishi maisha ya NJOZI za mchana, eti kuwa kama akina mwl nyerere, Nelson Mandela au kwame nkuruma. Msaniii! Maisha na mitazamo ya wazee hawa hakuna atakaye yaweza kwa kizazi hichi!
 
Back
Top Bottom